Yohana BSB

Yohana 1

John Chapter 1

1
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
In the beginning was the Word, and the Word was with God, and the Word was God.
2
Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
He was with God in the beginning.
3
Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
Through Him all things were made, and without Him nothing was made that has been made.
4
Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
In Him was life, and that life was the light of men.
5
Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.
The Light shines in the darkness, and the darkness has not overcome it.
6
Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
There came a man who was sent from God. His name was John.
7
Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye.
He came as a witness to testify about the Light, so that through him everyone might believe.
8
Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru.
He himself was not the Light, but he came to testify about the Light.
9
Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.
The true Light, who gives light to everyone, was coming into the world.
10
Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.
He was in the world, and though the world was made through Him, the world did not recognize Him.
11
Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.
He came to His own, and His own did not receive Him.
12
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
But to all who did receive Him, to those who believed in His name, He gave the right to become children of God—
13
waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.
children born not of blood, nor of the desire or will of man, but born of God.
14
Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.
The Word became flesh and made His dwelling among us. We have seen His glory, the glory of the one and only Son from the Father, full of grace and truth.
15
Yohana alimshuhudia, akapaza sauti yake akasema, Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Ajaye nyuma yangu amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.
John testified concerning Him. He cried out, saying, “This is He of whom I said, ‘He who comes after me has surpassed me because He was before me.’”
16
Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.
From His fullness we have all received grace upon grace.
17
Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.
For the law was given through Moses; grace and truth came through Jesus Christ.
18
Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.
No one has ever seen God, but the one and only Son, who is Himself God and is at the Father’s side, has made Him known.
19
Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?
And this was John’s testimony when the Jews of Jerusalem sent priests and Levites to ask him, “Who are you?”
20
Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.
He did not refuse to confess, but openly declared, “I am not the Christ.”
21
Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La.
“Then who are you?” they inquired. “Are you Elijah?” He said, “I am not.” “Are you the Prophet?” He answered, “No.”
22
Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako?
So they said to him, “Who are you? We need an answer for those who sent us. What do you say about yourself?”
23
Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.
John replied in the words of Isaiah the prophet: “I am a voice of one calling in the wilderness, ‘Make straight the way for the Lord.’”
24
Nao wale waliotumwa walikuwa wametoka kwa Mafarisayo.
Then the Pharisees who had been sent
25
Wakamwuliza, wakamwambia, Mbona basi wabatiza, ikiwa wewe si Kristo, wala Eliya, wala nabii yule?
asked him, “Why then do you baptize, if you are not the Christ, nor Elijah, nor the Prophet?”
26
Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi.
“I baptize with water,” John replied, “but among you stands One you do not know.
27
Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake.
He is the One who comes after me, the straps of whose sandals I am not worthy to untie.”
28
Hayo yalifanyika huko Bethania ng'ambo ya Yordani, alikokuwako Yohana akibatiza.
All this happened at Bethany beyond the Jordan, where John was baptizing.
29
Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
The next day John saw Jesus coming toward him and said, “Look, the Lamb of God, who takes away the sin of the world!
30
Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.
This is He of whom I said, ‘A man who comes after me has surpassed me because He was before me.’
31
Wala mimi sikumjua; lakini kusudi adhihirishwe kwa Israeli ndiyo maana mimi nalikuja nikibatiza kwa maji.
I myself did not know Him, but the reason I came baptizing with water was that He might be revealed to Israel.”
32
Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake.
Then John testified, “I saw the Spirit descending from heaven like a dove and resting on Him.
33
Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.
I myself did not know Him, but the One who sent me to baptize with water told me, ‘The man on whom you see the Spirit descend and rest is He who will baptize with the Holy Spirit.’
34
Nami nimeona, tena nimeshuhudia ya kuwa huyu ni Mwana wa Mungu.
I have seen and testified that this is the Son of God.”
35
Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake.
The next day John was there again with two of his disciples.
36
Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!
When he saw Jesus walking by, he said, “Look, the Lamb of God!”
37
Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.
And when the two disciples heard him say this, they followed Jesus.
38
Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?
Jesus turned and saw them following. “What do you want?” He asked. They said to Him, “Rabbi” (which means Teacher), “where are You staying?”
39
Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi.
“Come and see,” He replied. So they went and saw where He was staying, and spent that day with Him. It was about the tenth hour.
40
Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.
Andrew, Simon Peter’s brother, was one of the two who heard John’s testimony and followed Jesus.
41
Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo).
He first found his brother Simon and told him, “We have found the Messiah” (which is translated as Christ).
42
Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).
Andrew brought him to Jesus, who looked at him and said, “You are Simon son of John. You will be called Cephas” (which is translated as Peter).
43
Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate.
The next day Jesus decided to set out for Galilee. Finding Philip, He told him, “Follow Me.”
44
Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro.
Now Philip was from Bethsaida, the same town as Andrew and Peter.
45
Filipo akamwona Nathanaeli, akamwambia, Tumemwona yeye aliyeandikiwa na Musa katika torati, na manabii, Yesu, mwana wa Yusufu, mtu wa Nazareti.
Philip found Nathanael and told him, “We have found the One Moses wrote about in the Law, the One the prophets foretold—Jesus of Nazareth, the son of Joseph.”
46
Nathanaeli akamwambia, Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone.
“Can anything good come from Nazareth?” Nathanael asked. “Come and see,” said Philip.
47
Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake.
When Jesus saw Nathanael approaching, He said of him, “Here is a true Israelite, in whom there is no deceit.”
48
Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona.
“How do You know me?” Nathanael asked. Jesus replied, “Before Philip called you, I saw you under the fig tree.”
49
Nathanaeli akamjibu, Rabi, wewe u Mwana wa Mungu, ndiwe Mfalme wa Israeli.
“Rabbi,” Nathanael answered, “You are the Son of God! You are the King of Israel!”
50
Yesu akajibu, akamwambia, Kwa sababu nilikuambia, Nilikuona chini ya mtini, waamini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.
Jesus said to him, “Do you believe just because I told you I saw you under the fig tree? You will see greater things than these.”
51
Akamwambia, Amin, amin, nawaambia, Mtaziona mbingu zimefunguka na malaika wa Mungu wakikwea na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.
Then He declared, “Truly, truly, I tell you, you will all see heaven open and the angels of God ascending and descending on the Son of Man.”

Chagua Sura

1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21