Yohana 8 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yohana 8 (Swahili) John 8 (English)

[Walikwenda kila mtu nyumbani kwake; naye Yesu akaenda mpaka mlima wa Mizeituni. Yohana 8:1

but Jesus went to the Mount of Olives.

Hata asubuhi kulipokucha akaingia tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; naye akaketi, akawa akiwafundisha. Yohana 8:2

Now very early in the morning, he came again into the temple, and all the people came to him. He sat down, and taught them.

Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati. Yohana 8:3

The scribes and the Pharisees brought a woman taken in adultery. Having set her in the midst,

Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini. Yohana 8:4

they told him, "Teacher, we found this woman in adultery, in the very act.

Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje? Yohana 8:5

Now in our law, Moses commanded us to stone such. What then do you say about her?"

Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Yohana 8:6

They said this testing him, that they might have something to accuse him of. But Jesus stooped down, and wrote on the ground with his finger.

Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. Yohana 8:7

But when they continued asking him, he looked up and said to them, "He who is without sin among you, let him throw the first stone at her."

Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Yohana 8:8

Again he stooped down, and with his finger wrote on the ground.

Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati. Yohana 8:9

They, when they heard it, being convicted by their conscience, went out one by one, beginning from the oldest, even to the last. Jesus was left alone with the woman where she was, in the middle.

Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia? Yohana 8:10

Jesus, standing up, saw her and said, "Woman, where are your accusers? Did no one condemn you?"

Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.] Yohana 8:11

She said, "No one, Lord." Jesus said, "Neither do I condemn you. Go your way. From now on, sin no more."

Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima. Yohana 8:12

Again, therefore, Jesus spoke to them, saying, "I am the light of the world. He who follows me will not walk in the darkness, but will have the light of life."

Basi Mafarisayo wakamwambia, Wewe unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako si kweli. Yohana 8:13

The Pharisees therefore said to him, "You testify about yourself. Your testimony is not valid."

Yesu akajibu, akawaambia, Mimi ningawa ninajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ndio kweli; kwa sababu najua nilikotoka na niendako; lakini ninyi hamjui nilikotoka wala niendako. Yohana 8:14

Jesus answered them, "Even if I testify about myself, my testimony is true, for I know where I came from, and where I am going; but you don't know where I came from, or where I am going.

Ninyi mwahukumu kwa kufuata mambo ya mwili; mimi simhukumu mtu. Yohana 8:15

You judge according to the flesh. I judge no one.

Nami nijapohukumu, hukumu yangu ni kweli; kwa kuwa mimi si peke yangu, bali ni mimi na yeye aliyenipeleka. Yohana 8:16

Even if I do judge, my judgment is true, for I am not alone, but I am with the Father who sent me.

Tena katika torati yenu imeandikwa kwamba, Ushuhuda wa watu wawili ni kweli. Yohana 8:17

It's also written in your law that the testimony of two people is valid.

Mimi ndimi ninayejishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenipeleka ananishuhudia. Yohana 8:18

I am one who testifies about myself, and the Father who sent me testifies about me."

Basi wakamwambia, Yuko wapi Baba yako? Yesu akajibu, Mimi hamnijui, wala Baba yangu hammjui; kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba yangu. Yohana 8:19

They said therefore to him, "Where is your Father?" Jesus answered, "You know neither me, nor my Father. If you knew me, you would know my Father also."

Maneno hayo aliyasema alipokuwa akifundisha hekaluni, katika chumba cha hazina; wala hakuna mtu aliyemkamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado. Yohana 8:20

Jesus spoke these words in the treasury, as he taught in the temple. Yet no one arrested him, because his hour had not yet come.

Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi mtakufa katika dhambi yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja. Yohana 8:21

Jesus said therefore again to them, "I am going away, and you will seek me, and you will die in your sins. Where I go, you can't come."

Basi Wayahudi wakasema, Je! Atajiua! Kwa kuwa asema, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja? Yohana 8:22

The Jews therefore said, "Will he kill himself, that he says, 'Where I am going, you can't come?'"

Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu. Yohana 8:23

He said to them, "You are from beneath. I am from above. You are of this world. I am not of this world.

Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu. Yohana 8:24

I said therefore to you that you will die in your sins; for unless you believe that I am he, you will die in your sins."

Basi wakamwambia, U nani wewe? Yesu akawaambia, Hasa neno lilo hilo ninalowaambia. Yohana 8:25

They said therefore to him, "Who are you?" Jesus said to them, "Just what I have been saying to you from the beginning.

Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu; lakini yeye aliyenipeleka ni kweli, nami niliyoyasikia kwake, ndiyo ninenayo katika ulimwengu. Yohana 8:26

I have many things to speak and to judge concerning you. However he who sent me is true; and the things which I heard from him, these I say to the world."

Wala hawakutambua ya kuwa anawatajia Baba. Yohana 8:27

They didn't understand that he spoke to them about the Father.

Basi Yesu akawaambia, Mtakapokuwa mmekwisha kumwinua Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa mimi ndiye; na ya kuwa sifanyi neno kwa nafsi yangu, ila kama Baba alivyonifundisha ndivyo ninenavyo. Yohana 8:28

Jesus therefore said to them, "When you have lifted up the Son of Man, then you will know that I am he, and I do nothing of myself, but as my Father taught me, I say these things.

Naye aliyenipeleka yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo. Yohana 8:29

He who sent me is with me. The Father hasn't left me alone, for I always do the things that are pleasing to him."

Naye alipokuwa akisema hayo, wengi walimwamini. Yohana 8:30

As he spoke these things, many believed in him.

Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; Yohana 8:31

Jesus therefore said to those Jews who had believed him, "If you remain in my word, then you are truly my disciples.

tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru. Yohana 8:32

You will know the truth, and the truth will make you free."

Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru? Yohana 8:33

They answered him, "We are Abraham's seed, and have never been in bondage to anyone. How do you say, 'You will be made free?'"

Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. Yohana 8:34

Jesus answered them, "Most assuredly I tell you, everyone who commits sin is the bondservant of sin.

Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote. Yohana 8:35

A bondservant doesn't live in the house forever. A son remains forever.

Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli. Yohana 8:36

If therefore the Son makes you free, you will be free indeed.

Najua ya kuwa ninyi ni uzao wa Ibrahimu lakini mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halimo ndani yenu. Yohana 8:37

I know that you are Abraham's seed, yet you seek to kill me, because my word finds no place in you.

Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo; nanyi vivyo hivyo mliyoyasikia kwa baba yenu ndiyo myatendayo. Yohana 8:38

I say the things which I have seen with my Father; and you also do the things which you have seen with your father."

Wakajibu, wakamwambia, Baba yetu ndiye Ibrahimu! Yesu akawaambia, Kama mngekuwa watoto wa Ibrahimu, mngezitenda kazi zake Ibrahimu. Yohana 8:39

They answered him, "Our father is Abraham." Jesus said to them, "If you were Abraham's children, you would do the works of Abraham.

Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo. Yohana 8:40

But now you seek to kill me, a man who has told you the truth, which I heard from God. Abraham didn't do this.

Ninyi mnazitenda kazi za baba yenu. Ndipo walipomwambia, Sisi hatukuzaliwa kwa zinaa; sisi tunaye Baba mmoja, yaani, Mungu. Yohana 8:41

You do the works of your father." They said to him, "We were not born of sexual immorality. We have one Father, God."

Yesu akawaambia, Kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma. Yohana 8:42

Therefore Jesus said to them, "If God were your Father, you would love me, for I came out and have come from God. For I haven't come of myself, but he sent me.

Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu. Yohana 8:43

Why don't you understand my speech? Because you can't hear my word.

Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo. Yohana 8:44

You are of your Father, the devil, and you want to do the desires of your father. He was a murderer from the beginning, and doesn't stand in the truth, because there is no truth in him. When he speaks a lie, he speaks on his own; for he is a liar, and the father of it.

Nami, kwa sababu nasema iliyo kweli, hamnisadiki. Yohana 8:45

But because I tell the truth, you don't believe me.

Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi? Nami nikisema kweli, mbona ninyi hamnisadiki? Yohana 8:46

Which of you convicts me of sin? If I tell the truth, why do you not believe me?

Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu. Yohana 8:47

He who is of God hears the words of God. For this cause you don't hear, because you are not of God."

Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je! Sisi hatusemi vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo? Yohana 8:48

Then the Jews answered him, "Don't we say well that you are a Samaritan, and have a demon?"

Yesu akajibu, Mimi sina pepo; lakini mimi namheshimu Baba yangu, na ninyi mwanivunjia heshima yangu. Yohana 8:49

Jesus answered, "I don't have a demon, but I honor my Father, and you dishonor me.

Wala mimi siutafuti utukufu wangu; yuko mwenye kutafuta na kuhukumu. Yohana 8:50

But I don't seek my own glory. There is one who seeks and judges.

Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele. Yohana 8:51

Most assuredly, I tell you, if a person keeps my word, he will never see death."

Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng'amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele. Yohana 8:52

Then the Jews said to him, "Now we know that you have a demon. Abraham died, and the prophets; and you say, 'If a man keeps my word, he will never taste of death.'

Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani? Yohana 8:53

Are you greater than our father, Abraham, who died? The prophets died. Who do you make yourself out to be?"

Yesu akajibu, Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu; anitukuzaye ni Baba yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu. Yohana 8:54

Jesus answered, "If I glorify myself, my glory is nothing. It is my Father who glorifies me, of whom you say that he is our God.

Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nalishika. Yohana 8:55

You have not known him, but I know him. If I said, 'I don't know him,' I would be like you, a liar. But I know him, and keep his word.

Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi. Yohana 8:56

Your father Abraham rejoiced to see my day. He saw it, and was glad."

Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? Yohana 8:57

The Jews therefore said to him, "You are not yet fifty years old, and have you seen Abraham?"

Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko. Yohana 8:58

Jesus said to them, "Most assuredly, I tell you, before Abraham came into existence, I AM."

Basi wakaokota mawe ili wamtupie; lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni. Yohana 8:59

Therefore they took up stones to throw at him, but Jesus was hidden, and went out of the temple, having gone through the midst of them, and so passed by.