Yohana 13 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yohana 13 (Swahili) John 13 (English)

Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo. Yohana 13:1

Now before the feast of the Passover, Jesus knowing that his time had come that he would depart from this world to the Father, having loved his own who were in the world, he loved them to the end.

Hata wakati wa chakula cha jioni; naye Ibilisi amekwisha kumtia Yuda, mwana wa Simoni Iskariote, moyo wa kumsaliti; Yohana 13:2

After supper, the devil having already put into the heart of Judas Iscariot, Simon's son, to betray him,

Yesu, hali akijua ya kuwa Baba amempa vyote mikononi mwake, na ya kuwa alitoka kwa Mungu naye anakwenda kwa Mungu, Yohana 13:3

Jesus, knowing that the Father had given all things into his hands, and that he came forth from God, and was going to God,

aliondoka chakulani; akaweka kando mavazi yake, akatwaa kitambaa, akajifunga kiunoni. Yohana 13:4

arose from supper, and laid aside his outer garments. He took a towel, and wrapped a towel around his waist.

Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwatawadha wanafunzi miguu, na kuifuta kwa kile kitambaa alichojifunga. Yohana 13:5

Then he poured water into the basin, and began to wash the disciples' feet, and to wipe them with the towel that was wrapped around him.

Hivyo yuaja kwa Simoni Petro. Huyo akamwambia, Bwana! Wewe wanitawadha miguu mimi? Yohana 13:6

Then he came to Simon Peter. He said to him, "Lord, do you wash my feet?"

Yesu akajibu, akamwambia, Nifanyalo wewe hujui sasa; lakini utalifahamu baadaye. Yohana 13:7

Jesus answered him, "You don't know what I am doing now, but you will understand later."

Petro akamwambia, Wewe hutanitawadha miguu kamwe. Yesu akamwambia, Kama nisipokutawadha, huna shirika nami. Yohana 13:8

Peter said to him, "You will never wash my feet!" Jesus answered him, "If I don't wash you, you have no part with me."

Simoni Petro akamwambia, Bwana, si miguu yangu tu, hata na mikono yangu na kichwa changu pia. Yohana 13:9

Simon Peter said to him, "Lord, not my feet only, but also my hands and my head!"

Yesu akamwambia, Yeye aliyekwisha kuoga hana haja ila ya kutawadha miguu, bali yu safi mwili wote; nanyi mmekuwa safi, lakini si nyote. Yohana 13:10

Jesus said to him, "Someone who has bathed only needs to have his feet washed, but is completely clean. You are clean, but not all of you."

Kwa maana alimjua yeye atakayemsaliti; ndiyo maana alisema, Si nyote mlio safi. Yohana 13:11

For he knew him who would betray him, therefore he said, "You are not all clean."

Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena, akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea? Yohana 13:12

So when he had washed their feet, put his outer garment back on, and sat down again, he said to them, "Do you know what I have done to you?

Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo. Yohana 13:13

You call me, 'Teacher' and 'Lord.' You say so correctly, for so I am.

Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi. Yohana 13:14

If I then, the Lord and the Teacher, have washed your feet, you also ought to wash one another's feet.

Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo. Yohana 13:15

For I have given you an example, that you also should do as I have done to you.

Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka. Yohana 13:16

Most assuredly I tell you, a servant is not greater than his lord, neither one who is sent greater than he who sent him.

Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda. Yohana 13:17

If you know these things, blessed are you if you do them.

Sisemi habari za ninyi nyote; nawajua wale niliowachagua; lakini andiko lipate kutimizwa, Aliyekula chakula changu Ameniinulia kisigino chake. Yohana 13:18

I don't speak concerning all of you. I know whom I have chosen. But that the Scripture may be fulfilled, 'He who eats bread with me has lifted up his heel against me.'

Tangu sasa nawaambia kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa mimi ndiye. Yohana 13:19

From now on, I tell you before it happens, that when it happens, you may believe that I AM.

Amin, amin, nawaambieni, Yeye ampokeaye mtu ye yote nimpelekaye, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi; ampokea yeye aliyenipeleka. Yohana 13:20

Most assuredly I tell you, he who receives whomever I send, receives me; and he who receives me, receives him who sent me."

Naye alipokwisha kusema hayo, Yesu alifadhaika rohoni, akashuhudia akisema, Amin, amin, nawaambieni, Mmoja wenu atanisaliti. Yohana 13:21

When Jesus had said this, he was troubled in spirit, and testified, "Most assuredly I tell you that one of you will betray me."

Wanafunzi wakatazamana, huku wakiona shaka ni nani amtajaye. Yohana 13:22

The disciples looked at one another, perplexed about whom he spoke.

Na palikuwapo mmoja wa wanafunzi wake, ameegama kifuani pa Yesu, ambaye Yesu alimpenda. Yohana 13:23

One of his disciples, whom Jesus loved, was at the table, leaning against Jesus' breast.

Basi Simoni Petro akampungia mkono, akamwambia, Uliza, ni nani amtajaye? Yohana 13:24

Simon Peter therefore beckoned to him, and said to him, "Tell us who it is of whom he speaks."

Basi yeye, hali akimwelekea Yesu kifua chake, akamwambia, Bwana, ni nani? Yohana 13:25

He, leaning back, as he was, on Jesus' breast, asked him, "Lord, who is it?"

Basi Yesu akajibu, Ndiye mtu yule nitakayemtowelea tonge na kumpa. Akatowelea tonge, akalitwaa akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Yohana 13:26

Jesus therefore answered, "It is he to whom I will give this piece of bread when I have dipped it." So when he had dipped the piece of bread, he gave it to Judas, the son of Simon Iscariot.

Na baada ya hilo tonge Shetani alimwingia. Basi Yesu akamwambia, Uyatendayo yatende upesi. Yohana 13:27

After the piece of bread, then Satan entered into him. Then Jesus said to him, "What you do, do quickly."

Wala hakuna mtu katika wale walioketi chakulani aliyeijua sababu ya kumwambia hivyo. Yohana 13:28

Now no man at the table knew why he said this to him.

Kwa maana wengine walidhania, kwa kuwa Yuda huchukua mfuko, ya kwamba Yesu alimwambia kama, Nunua mnavyovihitaji kwa sikukuu; au kwamba awape maskini kitu. Yohana 13:29

For some thought, because Judas had the money box, that Jesus said to him, "Buy what things we need for the feast," or that he should give something to the poor.

Basi huyo, akiisha kulipokea lile tonge, akatoka mara hiyo. Nako kulikuwa ni usiku. Yohana 13:30

Therefore, having received that morsel, he went out immediately. It was night.

Basi huyo alipokwisha kutoka, Yesu alisema, Sasa ametukuzwa Mwana wa Adamu, naye Mungu ametukuzwa ndani yake. Yohana 13:31

When he had gone out, Jesus said, "Now the Son of Man has been glorified, and God has been glorified in him.

Mungu naye atamtukuza ndani ya nafsi yake; naye atamtukuza mara. Yohana 13:32

If God has been glorified in him, God will also glorify him in himself, and he will glorify him immediately.

Enyi watoto wadogo, bado kitambo kidogo nipo pamoja nanyi; mtanitafuta; na kama vile nilivyowaambia Wayahudi ya kwamba, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja; kadhalika sasa nawaambia ninyi. Yohana 13:33

Little children, I will be with you a little while longer. You will seek me, and as I said to the Jews, 'Where I am going, you can't come,' so now I tell you.

Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Yohana 13:34

A new commandment I give to you, that you love one another, just like I have loved you; that you also love one another.

Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi. Yohana 13:35

By this everyone will know that you are my disciples, if you have love for one another."

Simoni Petro akamwambia, Bwana, unakwendapi? Yesu akamjibu, Niendako huwezi kunifuata sasa; lakini utanifuata baadaye. Yohana 13:36

Simon Peter said to him, "Lord, where are you going?" Jesus answered, "Where I am going, you can't follow now, but you will follow afterwards."

Petro akamwambia, Bwana, kwa nini mimi nisiweze kukufuata sasa? Mimi nitautoa uhai wangu kwa ajili yako. Yohana 13:37

Peter said to him, "Lord, why can't I follow you now? I will lay down my life for you."

Yesu akamjibu, Je! Wewe utautoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin, nakuambia, Jimbi hatawika hata wewe utakapokuwa umenikana mara tatu. Yohana 13:38

Jesus answered him, "Will you lay down your life for me? Most assuredly I tell you, the rooster won't crow until you have denied me three times.