1
Yesu aliwaambia, Amin, amin, nawaambieni, Yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo, lakini akwea penginepo, huyo ni mwivi naye ni mnyang'anyi.
“Truly, truly, I tell you, whoever does not enter the sheepfold by the gate, but climbs in some other way, is a thief and a robber.
2
Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo.
But the one who enters by the gate is the shepherd of the sheep.
3
Bawabu humfungulia huyo, na kondoo humsikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kwa majina yao, na kuwapeleka nje.
The gatekeeper opens the gate for him, and the sheep listen for his voice. He calls his own sheep by name and leads them out.
4
Naye awatoapo nje kondoo wake wote, huwatangulia; na wale kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake.
When he has brought out all his own, he goes on ahead of them, and his sheep follow him because they know his voice.
5
Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni.
But they will never follow a stranger; in fact, they will flee from him because they do not recognize his voice.”
6
Mithali hiyo Yesu aliwaambia, lakini wao hawakuelewa na mambo hayo aliyowaambia.
Jesus spoke to them using this illustration, but they did not understand what He was telling them.
7
Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.
So He said to them again, “Truly, truly, I tell you, I am the gate for the sheep.
8
Wote walionitangulia ni wevi na wanyang'anyi; lakini kondoo hawakuwasikia.
All who came before Me were thieves and robbers, but the sheep did not listen to them.
9
Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
I am the gate. If anyone enters through Me, he will be saved. He will come in and go out and find pasture.
10
Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
The thief comes only to steal and kill and destroy. I have come that they may have life, and have it in all its fullness.
11
Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
I am the good shepherd. The good shepherd lays down His life for the sheep.
12
Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya.
The hired hand is not the shepherd, and the sheep are not his own. When he sees the wolf coming, he abandons the sheep and runs away. Then the wolf pounces on them and scatters the flock.
13
Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake.
The man runs away because he is a hired servant and is unconcerned for the sheep.
14
Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;
I am the good shepherd. I know My sheep and My sheep know Me,
15
kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
just as the Father knows Me and I know the Father. And I lay down My life for the sheep.
16
Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.
I have other sheep that are not of this fold. I must bring them in as well, and they will listen to My voice. Then there will be one flock and one shepherd.
17
Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.
The reason the Father loves Me is that I lay down My life in order to take it up again.
18
Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.
No one takes it from Me, but I lay it down of My own accord. I have authority to lay it down and authority to take it up again. This charge I have received from My Father.”
19
Kukaingia tena matengano kati ya Wayahudi, kwa ajili ya maneno hayo.
Again there was division among the Jews because of Jesus’ message.
20
Wengi wao wakasema, Ana pepo huyu, tena ana wazimu; mbona mnamsikiliza?
Many of them said, “He is demon-possessed and insane. Why would you listen to Him?”
21
Wengine wakasema, Maneno hayo siyo ya mtu mwenye pepo. Je! Pepo aweza kuwafumbua macho vipofu?
But others replied, “These are not the words of a man possessed by a demon. Can a demon open the eyes of the blind?”
22
Basi huko Yerusalemu ilikuwa Sikukuu ya Kutabaruku; ni wakati wa baridi.
At that time the Feast of Dedication took place in Jerusalem. It was winter,
23
Naye Yesu alikuwa akitembea hekaluni, katika ukumbi wa Sulemani.
and Jesus was walking in the temple courts in Solomon’s Colonnade.
24
Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.
So the Jews gathered around Him and demanded, “How long will You keep us in suspense? If You are the Christ, tell us plainly.”
25
Yesu akawajibu, Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia.
“I already told you,” Jesus replied, “but you did not believe. The works I do in My Father’s name testify on My behalf.
26
Lakini ninyi hamsadiki, kwa sababu hammo miongoni mwa kondoo wangu.
But because you are not My sheep, you refuse to believe.
27
Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.
My sheep listen to My voice; I know them, and they follow Me.
28
Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.
I give them eternal life, and they will never perish. No one can snatch them out of My hand.
29
Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna mtu awezaye kuwapokonya katika mkono wa Baba yangu.
My Father who has given them to Me is greater than all. No one can snatch them out of My Father’s hand.
30
Mimi na Baba tu umoja.
I and the Father are one.”
31
Basi Wayahudi wakaokota mawe tena ili wampige.
At this, the Jews again picked up stones to stone Him.
32
Yesu akawajibu, Kazi njema nyingi nimewaonyesha, zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe?
But Jesus responded, “I have shown you many good works from the Father. For which of these do you stone Me?”
33
Wayahudi wakamjibu, Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu.
“We are not stoning You for any good work,” said the Jews, “but for blasphemy, because You, who are a man, make Yourself out to be God.”
34
Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu?
Jesus replied, “Is it not written in your Law: ‘I have said you are gods’?
35
Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka);
If he called them gods to whom the word of God came—and the Scripture cannot be broken—
36
je! Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?
then what about the One whom the Father sanctified and sent into the world? How then can you accuse Me of blasphemy for stating that I am the Son of God?
37
Kama sizitendi kazi za Baba yangu, msiniamini;
If I am not doing the works of My Father, then do not believe Me.
38
lakini nikizitenda, ijapokuwa hamniamini mimi, ziaminini zile kazi; mpate kujua na kufahamu ya kuwa Baba yu ndani yangu, nami ni ndani ya Baba.
But if I am doing them, even though you do not believe Me, believe the works themselves, so that you may know and understand that the Father is in Me, and I am in the Father.”
39
Wakatafuta tena kumkamata; lakini akatoka mikononi mwao.
At this, they tried again to seize Him, but He escaped their grasp.
40
Akaenda zake tena ng'ambo ya Yordani, mpaka mahali pale alipokuwapo Yohana akibatiza hapo kwanza, akakaa huko.
Then Jesus went back across the Jordan to the place where John had first been baptizing, and He stayed there.
41
Na watu wengi wakamwendea, wakasema, Yohana kweli hakufanya ishara yo yote, lakini yote aliyoyasema Yohana katika habari zake huyu yalikuwa kweli.
Many came to Him and said, “Although John never performed a sign, everything he said about this man was true.”
42
Nao wengi wakamwamini huko.
And many in that place believed in Jesus.