Solomon Mukubwa - Futa Machozi Lyrics

Futa Machozi Lyrics

Nalimngoja Bwana kwa zaburi
Akaniinamia akanisikia kilio changu
Akanipandisha toka shimo, shimo la uharibifu
Akanisimamisha Bwana, toka udongo wa utelezi,
Akasimamisha miguu yako mwambani, Bwana wangu wee
Akazisimamisha hatua zangu, akazipanga sawa sawa
Ili nimtumikie ee eh, ndio sifa zake zimekaa midomoni mwangu
Ameweka wimbo mpya midomoni mwangu
Ndio maana ninaamba sifa zako Mungu wangu
Ndio maana kila siku nashuhudia wema wake Bwana

Futa futa machozi usilie tena, kibali kiko juu yako
Simama kama shujaa, ushambulie malango*
Sayuni imekukubali

Hatutaki kulia lia sana, hatutaki ukristo wa kulilia sana.
Sisi ni washindi, hata tupipitie moto haitatuchoma
Hata tukitupwa baharini, samaki haitatumaliza
Hata tupitie maji, haitatukarigisha, maaana sisi ni washindi. Mkristo simama kama shujaa, ushambilie malango
Umepewa mamlaka na kibali, mbona umeonelewa na adui
kiasi hii, ebu simama kama shujaa, mpingeni adui naye atawakimbia, sisi ni washindi zaidi ya washindi.

Futa futa machozi usilie tena, kibali kiko juu yako
Simama kama shujaa, ushambulie malango*
Sayuni imekukubali

" Lazima tujiamini lazima kujitwaa, tumepewa mamlaka
ya kukanyaga nyoka na yule ibilisi, na kila ufalme wa
ulimwengu wa giza, hazina mamlaka juu Yeu"

Futa futa machozi usilie tena, kibali kiko juu yako
Simama kama shujaa, ushambulie malango*
Sayuni imekukubali



Futa Machozi Video

Futa Machozi Lyrics -  Solomon Mukubwa

Solomon Mukubwa Songs

Related Songs