Lyrics
Verse 1
Bwana u sehemu yangu, Rafiki yangu wewe
Katika safari yangu Tatembea na wewe
Pamoja na wewe, Pamoja na wewe
Katika safari yangu Tatembea na wewe
Verse 2
Mali hapa sikutaka, Ili niheshimiwe
Na yanikute mashaka Sawa sawa na wewe
Pamoja na wewe, Pamoja na wewe
Heri nikute mashaka Sawa sawa na wewe
Verse 3
Niongoze safarini, Mbele unichukue
Mlangoni kwa Mbinguni Niingie na wewe
Pamoja na wewe, Pamoja na wewe
Mlangoni kwa mbinguni, Niingie na wewe