Sifa Lyrics

Nipe by Goodluck Gozbert cover art

Goodluck Gozbert - Nipe Lyrics

Artist:
Goodluck Gozbert

Lyrics

Hata nikiwa sina chakula 


Isinifanye kusahau 


Ulinilisha nikasaza 


Hata nikiwa sina mavazi 


Isinifanye nifukuru 


Na kusahau umeniweka hai 


Ona wapo marafiki 


Wanakosa kula na kuvaa 


Hawalalamiki, wanakushukuru tu 


Mimi eh, nilikupa nini Baba 


Cha kunipa kibali


Kwa siku zilizofurahisha? 


Taabu kidogo zisinifanye nikusahau 


Umeshatenda mengi – nikiwa hapa 


Shida itapita, bado kidogo 


Ikiwa nitachoka niiunue 


Refrain:


Nipe kukumbuka wema  


Nipe kukumbuka wema 


Nipe kukumbuka wema 


Nipe kumbuka wema wako 


Hata kwenye bonde hili la mauti 


Nakumbuka nilikuita, 


Na wewe ukaitika Baba 


Kutegemea akili zangu, na mawazo yangu 


Kutanifanya niendelee 


niendelee kulalamika 


Kuna kipindi najisahau 


na kujivunia mafanikio 


Wengine naona takataka 


Nikumbushe mi ni mtu tu 


na dunia tunapita 


Uhai wangu si faida bila wewe 


Mungu wewe ni mkuu 


kuliko vile nakutazama Baba 


Unisamehe, unisamehe 


Kuna nyakati nadhani 


hii dunia labda ni ya ushindani 


Natumia akili zangu za ndani 


Ila bado nashindwa kuendelea 


Nikimbushe nisidhani 


Wakifanikiwa tuna upinzani 


Nifundishe kuwaombea amani 


Na utatenda kwa wakati 


Na ikiwa Kama nikisahau 


Unikumbushe mi mtoto wako 


Nipe kukumbuka wema  


Nipe kukumbuka wema 


Nipe kukumbuka wema 


Nipe kumbuka wema wako 


Video