Goodluck Gozbert - Nipe Lyrics

Nipe Lyrics

Hata nikiwa sina chakula 
Isinifanye kusahau 
Ulinilisha nikasaza 
Hata nikiwa sina mavazi 
Isinifanye nifukuru 
Na kusahau umeniweka hai 
Ona wapo marafiki 
Wanakosa kula na kuvaa 
Hawalalamiki, wanakushukuru tu 
Mimi eh, nilikupa nini Baba 
Cha kunipa kibali
Kwa siku zilizofurahisha? 

Taabu kidogo zisinifanye nikusahau 
Umeshatenda mengi – nikiwa hapa 
Shida itapita, bado kidogo 
Ikiwa nitachoka niiunue 

Refrain:
Nipe kukumbuka wema  
Nipe kukumbuka wema 
Nipe kukumbuka wema 
Nipe kumbuka wema wako 

Hata kwenye bonde hili la mauti 
Nakumbuka nilikuita, 
Na wewe ukaitika Baba 
Kutegemea akili zangu, na mawazo yangu 
Kutanifanya niendelee 
niendelee kulalamika 
Kuna kipindi najisahau 
na kujivunia mafanikio 
Wengine naona takataka 
Nikumbushe mi ni mtu tu 
na dunia tunapita 
Uhai wangu si faida bila wewe 

Mungu wewe ni mkuu 
kuliko vile nakutazama Baba 
Unisamehe, unisamehe 
Kuna nyakati nadhani 
hii dunia labda ni ya ushindani 
Natumia akili zangu za ndani 
Ila bado nashindwa kuendelea 
Nikimbushe nisidhani 
Wakifanikiwa tuna upinzani 
Nifundishe kuwaombea amani 
Na utatenda kwa wakati 

Na ikiwa Kama nikisahau 
Unikumbushe mi mtoto wako 

Nipe kukumbuka wema  
Nipe kukumbuka wema 
Nipe kukumbuka wema 
Nipe kumbuka wema wako 


Nipe Video

Nipe Lyrics -  Goodluck Gozbert

Goodluck Gozbert Songs

Related Songs