Goodluck Gozbert - Ipo siku Yangu nibarikiwe Lyrics

Ipo siku Yangu nibarikiwe Lyrics

Ni mbali nimetoka Tena ni ajabu kuwa hai
Maana ningeshakufaga Ni mengi nimeona
Tena ya kuvunja moyo Labda ningeshamwacha Mungu

Kama ni misongo ya mawazo
Magonjwa mama, nimepitia, ninazoea
Maumivu ya kudharauliwa, umasikini
Ni kila siku, ninajipa moyo

Ipo siku yangu tu, Ipo Siku, siku
Ipo siku yangu tu
Nami niba niba nibarikiwe,

Nami nibarikiwe, nibarikiwe
niba, niba, nibarikiwe

Ingawa kwa sasa wananisema vibaya,
Nami sishangai – najua ni ya wanadamu hayo.
Ingawa sipati na ni kwa muda mrefu
Siachi kuomba; Mungu si kiziwi.
Binadamu wema, ukiwa nacho
Kwa sasa waniepuka sina rafiki wa dhati.

Ooh Kama ni misongo ya mawazo
Magonjwa mama, nimepitia, ninazoea
Maumivu ya kudharauliwa, umasikini
Ni kila siku, ninajipa moyo

Ipo siku yangu tu, Ipo Siku, siku
Ipo siku yangu tu
Nami niba niba nibarikiwe,

Nami nibarikiwe, nibarikiwe
niba, niba, nibarikiwe

Miaka imepita, unaombaga mtoto hupati
Vuta subira maana Yeye hachelewi
Ona biashara imeandamwa mikosi hupati
Usimwache Mungu, waganga watakuponza
Mpo kwa ndoa ila nyumbani amani hakuna
Msimwache Mungu – michepuko sio jibu
Umeugua tumaini la kupona hakuna
Usimtazame mwanadamu siku yako imekaribia.

Najua Ayaya, najua ayaya, najua ayaya

Misukosuko ya ndoa Mtoto anakusumbua
Giza likiingia unawaza wapi utalala
Masimango Mashemeji, ati huzai mtoto
Masimango mama wa kambo, Umemchosha nyumbani
Usiwaze usiumie, najua yote yatapita
Siku imekaribia, najua yote yatapita

Nawe ubarikiwe, nibarikiwe
Ubarikiwe, nibarikiwe
Nawe ubarikiwe
Uba, Uba, Ubarikiwe eh


Ipo siku Yangu nibarikiwe Video

Ipo siku Yangu nibarikiwe Lyrics -  Goodluck Gozbert

Goodluck Gozbert Songs

Related Songs