Mathayo 26 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mathayo 26 (Swahili) Matthew 26 (English)

Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake, Mathayo 26:1

It happened, when Jesus had finished all these words, that he said to his disciples,

Mnajua ya kuwa baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, na Mwana wa Adamu atasalitiwa asulibiwe. Mathayo 26:2

"You know that after two days the Passover is coming, and the Son of Man will be delivered up to be crucified."

Wakati ule wakuu wa makuhani, na wazee wa watu, wakakusanyika katika behewa ya Kuhani Mkuu, jina lake Kayafa; Mathayo 26:3

Then the chief priests, the scribes, and the elders of the people were gathered together in the court of the high priest, who was called Caiaphas.

wakafanya shauri pamoja, ili wamkamate Yesu kwa hila na kumwua. Mathayo 26:4

They took counsel together that they might take Jesus by deceit, and kill him.

Lakini wakasema, Isiwe wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu. Mathayo 26:5

But they said, "Not during the feast, lest a riot occur among the people."

Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma, Mathayo 26:6

Now when Jesus was in Bethany, in the house of Simon the leper,

mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya thamani kubwa alimkaribia akaimimina kichwani pake alipoketi chakulani. Mathayo 26:7

a woman came to him having an alabaster jar of very expensive ointment, and she poured it on his head as he sat at the table.

Wanafunzi wake walipoona, wakachukiwa, wakasema, Ni wa nini upotevu huu? Mathayo 26:8

But when his disciples saw this, they were indignant, saying, "Why this waste?

Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa fedha nyingi wakapewa maskini. Mathayo 26:9

For this ointment might have been sold for much, and given to the poor."

Yesu akatambua akawaambia, Mbona mnamtaabisha mwanamke? Maana ni kazi njema aliyonitendea mimi. Mathayo 26:10

But Jesus, knowing this, said to them, "Why do you trouble the woman? Because she has done a good work for me.

Kwa maana siku zote mnao maskini pamoja nanyi; lakini mimi hamnami siku zote. Mathayo 26:11

For you always have the poor with you; but you don't always have me.

Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu. Mathayo 26:12

For in pouring this ointment on my body, she did it to prepare me for burial.

Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake. Mathayo 26:13

Most assuredly I tell you, wherever this Gospel is preached in the whole world, what this woman has done will also be spoken of as a memorial of her."

Wakati huo mmoja wa wale Thenashara, jina lake Yuda Iskariote, aliwaendea wakuu wa makuhani, Mathayo 26:14

Then one of the twelve, who was called Judas Iscariot, went to the chief priests,

akasema, Ni nini mtakachonipa, nami nitamsaliti kwenu? Wakampimia vipande thelathini vya fedha. Mathayo 26:15

and said, "What are you willing to give me, that I should deliver him to you?" They weighed out for him thirty pieces of silver.

Tokea wakati huo akawa akitafuta nafasi apate kumsaliti. Mathayo 26:16

From that time he sought opportunity to betray him.

Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi wake wakamwendea Yesu, wakamwambia, Ni wapi utakapo tukuandalie uile Pasaka? Mathayo 26:17

Now on the first day of unleavened bread, the disciples came to Jesus, saying to him, "Where do you want us to prepare for you to eat the Passover?"

Akasema, Enendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie, Mwalimu asema, Majira yangu ni karibu; kwako nitafanya Pasaka pamoja na wanafunzi wangu. Mathayo 26:18

He said, "Go into the city to a certain person, and tell him, 'The Teacher says, "My time is at hand. I will keep the Passover at your house with my disciples."'"

Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaiandaa Pasaka. Mathayo 26:19

The disciples did as Jesus commanded them, and they prepared the Passover.

Basi kulipokuwa jioni aliketi chakulani pamoja na wale Thenashara. Mathayo 26:20

Now when evening had come, he was reclining at the table with the twelve disciples.

Nao walipokuwa wakila, alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu atanisaliti. Mathayo 26:21

As they were eating, he said, "Most assuredly I tell you that one of you will betray me."

Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja, Ni mimi, Bwana? Mathayo 26:22

They were exceedingly sorrowful, and each began to ask him, "It isn't me, is it, Lord?"

Akajibu akasema, Yeye aliyetia mkono wake pamoja nami katika kombe, ndiye atakayenisaliti. Mathayo 26:23

He answered, "He who dipped his hand with me in the dish, the same will betray me.

Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa. Mathayo 26:24

The Son of Man goes, even as it is written of him, but woe to that man through whom the Son of Man is betrayed! It would be better for that man if he had not been born."

Yuda, yule mwenye kumsaliti, akajibu, akasema, Ni mimi, Rabi? Akamwambia, Wewe umesema. Mathayo 26:25

Judas, who betrayed him, answered, "It isn't me, is it, Rabbi?" He said to him, "You said it."

Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu Mathayo 26:26

As they were eating, Jesus took bread, gave thanks for{TR reads "blessed" instead of "gave thanks for"} it, and broke it. He gave to the disciples, and said, "Take, eat; this is my body."

Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki; Mathayo 26:27

He took the cup, gave thanks, and gave to them, saying, "All of you drink it,

kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi. Mathayo 26:28

for this is my blood of the new covenant, which is poured out for many for the remission of sins.

Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu. Mathayo 26:29

But I tell you that I will not drink of this fruit of the vine from now on, until that day when I drink it anew with you in my Father's Kingdom."

Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni. Mathayo 26:30

When they had sung a hymn, they went out to the Mount of Olives.

Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika. Mathayo 26:31

Then Jesus said to them, "All of you will be made to stumble because of me tonight, for it is written, 'I will strike the shepherd, and the sheep of the flock will be scattered.'

Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya. Mathayo 26:32

But after I am raised up, I will go before you into Galilee."

Petro akajibu, akamwambia, Wajapochukizwa wote kwa ajili yako, mimi sitachukizwa kamwe. Mathayo 26:33

But Peter answered him, "Even if all will be made to stumble because of you, I will never be made to stumble."

Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, usiku huu kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Mathayo 26:34

Jesus said to him, "Most assuredly I tell you that tonight, before the rooster crows, you will deny me three times."

Petro akamwambia, Ijaponipasa kufa nawe, sitakukana kamwe. Na wanafunzi wote wakasema vivyo hivyo. Mathayo 26:35

Peter said to him, "Even if I must die with you, I will not deny you." All of the disciples also said likewise.

Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe. Mathayo 26:36

Then Jesus came with them to a place called Gethsemane, and said to his disciples, "Sit here, while I go there and pray."

Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka. Mathayo 26:37

He took with him Peter and the two sons of Zebedee, and began to be sorrowful and severely troubled.

Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami. Mathayo 26:38

Then he said to them, "My soul is exceedingly sorrowful, even to death. Stay here, and watch with me."

Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe. Mathayo 26:39

He went forward a little, fell on his face, and prayed, saying, "My Father, if it is possible, let this cup pass away from me; nevertheless, not what I desire, but what you desire."

Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? Mathayo 26:40

He came to the disciples, and found them sleeping, and said to Peter, "What, couldn't you watch with me for one hour?

Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu. Mathayo 26:41

Watch and pray, that you don't enter into temptation. The spirit indeed is willing, but the flesh is weak."

Akaenda tena mara ya pili, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwa haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisipokunywa, mapenzi yako yatimizwe. Mathayo 26:42

Again, a second time he went away, and prayed, saying, "My Father, if this cup can't pass away from me unless I drink it, your desire be done."

Akaja tena, akawakuta wamelala; maana macho yao yamekuwa mazito. Mathayo 26:43

He came again and found them sleeping, for their eyes were heavy.

Akawaacha tena, akaenda, akaomba mara ya tatu, akisema maneno yale yale. Mathayo 26:44

He left them again, went away, and prayed a third time, saying the same words.

Kisha akawajia wanafunzi wake, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike tazama, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anatiwa katika mikono ya wenye dhambi. Mathayo 26:45

Then he came to his disciples, and said to them, "Sleep on now, and take your rest. Behold, the hour is at hand, and the Son of Man is betrayed into the hands of sinners.

Ondokeni, twende zetuni! Tazama, yule anayenisaliti amekaribia. Mathayo 26:46

Arise, let's be going. Behold, he who betrays me is at hand."

Basi alipokuwa katika kusema, tazama, Yuda, mmoja wa wale Thenashara akaja, na pamoja naye kundi kubwa wenye panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu. Mathayo 26:47

While he was still speaking, behold, Judas, one of the twelve, came, and with him a great multitude with swords and clubs, from the chief priest and elders of the people.

Na yule mwenye kumsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni. Mathayo 26:48

Now he who betrayed him gave them a sign, saying, "Whoever I kiss, he is the one. Seize him."

Mara akamwendea Yesu, akasema, Salamu, Rabi, akambusu. Mathayo 26:49

Immediately he came to Jesus, and said, "Hail, Rabbi!" and kissed him.

Yesu akamwambia, Rafiki, fanya ulilolijia. Wakaenda, wakanyosha mikono yao wakamkamata Yesu. Mathayo 26:50

Jesus said to him, "Friend, why are you here?" Then they came and laid hands on Jesus, and took him.

Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio. Mathayo 26:51

Behold, one of those who were with Jesus stretched out his hand, and drew his sword, and struck the servant of the high priest, and struck off his ear.

Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga. Mathayo 26:52

Then Jesus said to him, "Put your sword back into its place, for all those who take the sword will die by the sword.

Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika? Mathayo 26:53

Or do you think that I couldn't ask my Father, and he would even now send me more than twelve legions of angels?

Yatatimizwaje basi maandiko, ya kwamba hivyo ndivyo vilivyopasa kujiri? Mathayo 26:54

How then would the Scriptures be fulfilled that it must be so?"

Saa ile Yesu akawaambia makutano, Je, mmetoka kama kumkamata mnyang'anyi, wenye panga na marungu, ili kunishika? Kila siku naliketi hekaluni nikifundisha, msinikamate. Mathayo 26:55

In that hour Jesus said to the multitudes, "Have you come out as against a robber with swords and clubs to seize me? I sat daily in the temple teaching, and you didn't arrest me.

Lakini haya yote yamekuwa, ili maandiko ya manabii yatimizwe. Ndipo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia. Mathayo 26:56

But all this has happened, that the Scriptures of the prophets might be fulfilled." Then all the disciples left him, and fled.

Nao waliomkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokuwa wamekutanika waandishi na wazee. Mathayo 26:57

Those who had taken Jesus led him away to Caiaphas the high priest, where the scribes and the elders were gathered together.

Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka behewa ya Kuhani Mkuu, akaingia ndani, akaketi pamoja na watumishi, auone mwisho. Mathayo 26:58

But Peter followed him from a distance, to the court of the high priest, and entered in and sat with the officers, to see the end.

Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua; Mathayo 26:59

Now the chief priests, the elders, and the whole council sought false testimony against Jesus, that they might put him to death;

wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi. Mathayo 26:60

and they found none. Even though many false witnesses came forward, they found none. But at last two false witnesses came forward,

Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu. Mathayo 26:61

and said, "This man said, 'I am able to destroy the temple of God, and to build it in three days.'"

Kisha Kuhani Mkuu akasimama akamwambia, Hujibu neno? Hawa wanakushuhudia nini? Mathayo 26:62

The high priest stood up, and said to him, "Have you no answer? What is this that these testify against you?"

Lakini, Yesu akanyamaza. Kuhani Mkuu akamwambia, Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu. Mathayo 26:63

But Jesus held his peace. The high priest answered him, "I adjure you by the living God, that you tell us whether you are the Christ, the Son of God."

Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni. Mathayo 26:64

Jesus said to him, "You have said it. Nevertheless, I tell you, henceforth you will see the Son of Man sitting at the right hand of Power, and coming on the clouds of the sky."

Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake; Mathayo 26:65

Then the high priest tore his clothing, saying, "He has spoken blasphemy! Why do we need any more witnesses? Behold, now you have heard his blasphemy.

mwaonaje ninyi? Wakajibu, wakasema, Imempasa kuuawa. Mathayo 26:66

What do you think?" They answered, "He is worthy of death!"

Ndipo wakamtemea mate ya uso, wakampiga makonde; wengine wakampiga makofi, Mathayo 26:67

Then they spit in his face and beat him with their fists, and some slapped him,

wakisema, Ewe Kristo, tufumbulie; ni nani aliyekupiga? Mathayo 26:68

saying, "Prophesy to us, you Christ! Who hit you?"

Na Petro alikuwa ameketi nje behewani; kijakazi mmoja akamwendea, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na Yesu wa Galilaya. Mathayo 26:69

Now Peter was sitting outside in the court, and a maid came to him, saying, "You were also with Jesus, the Galilean!"

Akakana mbele ya wote, akisema, Sijui usemalo. Mathayo 26:70

But he denied it before them all, saying, "I don't know what you are talking about."

Naye alipotoka nje hata ukumbini, mwanamke mwingine alimwona, akawaambia watu waliokuwako huko, Huyu alikuwapo pamoja na Yesu Mnazareti. Mathayo 26:71

When he had gone out onto the porch, someone else saw him, and said to those who were there, "This man also was with Jesus of Nazareth."

Akakana tena kwa kiapo, Simjui mtu huyu. Mathayo 26:72

Again he denied it with an oath, "I don't know the man."

Punde kidogo, wale waliohudhuria wakamwendea, wakamwambia Petro, Hakika wewe nawe u mmoja wao; kwa sababu hata usemi wako wakutambulisha. Mathayo 26:73

After a little while those who stood by came and said to Peter, "Surely you are also one of them, for your speech makes you known."

Ndipo akaanza kulaani na kuapa akisema, Simjui mtu huyu. Na mara akawika jogoo. Mathayo 26:74

Then he began to curse and to swear, "I don't know the man!" Immediately the rooster crowed.

Petro akalikumbuka lile neno la Yesu alilolisema, Kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Akatoka nje, akalia kwa majonzi. Mathayo 26:75

Peter remembered the word which Jesus had said to him, "Before the rooster crows, you will deny me three times." He went out and wept bitterly.