1
Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema,
Once again, Jesus spoke to them in parables:
2
Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.
“The kingdom of heaven is like a king who prepared a wedding banquet for his son.
3
Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.
He sent his servants to call those he had invited to the banquet, but they refused to come.
4
Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng'ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.
Again, he sent other servants and said, ‘Tell those who have been invited that I have prepared my dinner. My oxen and fattened cattle have been killed, and everything is ready. Come to the wedding banquet.’
5
Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;
But they paid no attention and went away, one to his field, another to his business.
6
nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.
The rest seized his servants, mistreated them, and killed them.
7
Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.
The king was enraged, and he sent his troops to destroy those murderers and burn their city.
8
Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.
Then he said to his servants, ‘The wedding banquet is ready, but those I invited were not worthy.
9
Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.
Go therefore to the crossroads and invite to the banquet as many as you can find.’
10
Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.
So the servants went out into the streets and gathered everyone they could find, both evil and good, and the wedding hall was filled with guests.
11
Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.
But when the king came in to see the guests, he spotted a man who was not dressed in wedding clothes.
12
Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.
‘Friend,’ he asked, ‘how did you get in here without wedding clothes?’ But the man was speechless.
13
Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Then the king told the servants, ‘Tie him hand and foot, and throw him into the outer darkness, where there will be weeping and gnashing of teeth.’
14
Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.
For many are called, but few are chosen.”
15
Ndipo Mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri, jinsi ya kumtega kwa maneno.
Then the Pharisees went out and conspired to trap Jesus in His words.
16
Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu.
They sent their disciples to Him along with the Herodians. “Teacher,” they said, “we know that You are honest and that You teach the way of God in accordance with the truth. You seek favor from no one, because You pay no attention to external appearance.
17
Basi utuambie, Waonaje? Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo?
So tell us what You think: Is it lawful to pay taxes to Caesar or not?”
18
Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?
But Jesus knew their evil intent and said, “You hypocrites, why are you testing Me?
19
Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari.
Show Me the coin used for the tax.” And they brought Him a denarius.
20
Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii, na anwani hii?
“Whose image is this,” He asked, “and whose inscription?”
21
Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.
“Caesar’s,” they answered. So Jesus told them, “Give to Caesar what is Caesar’s, and to God what is God’s.”
22
Waliposikia, walistaajabu, wakamwacha, wakaenda zao.
And when they heard this, they were amazed. So they left Him and went away.
23
Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,
That same day the Sadducees, who say there is no resurrection, came to Jesus and questioned Him.
24
wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.
“Teacher,” they said, “Moses declared that if a man dies without having children, his brother is to marry the widow and raise up offspring for him.
25
Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.
Now there were seven brothers among us. The first one married and died without having children. So he left his wife to his brother.
26
Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.
The same thing happened to the second and third brothers, down to the seventh.
27
Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.
And last of all, the woman died.
28
Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.
In the resurrection, then, whose wife will she be of the seven? For all of them were married to her.”
29
Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.
Jesus answered, “You are mistaken because you do not know the Scriptures or the power of God.
30
Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni.
In the resurrection, people will neither marry nor be given in marriage. Instead, they will be like the angels in heaven.
31
Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema,
But concerning the resurrection of the dead, have you not read what God said to you:
32
Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.
‘I am the God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob’? He is not the God of the dead, but of the living.”
33
Na makutano waliposikia, walishangaa kwa mafunzo yake.
When the crowds heard this, they were astonished at His teaching.
34
Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja.
And when the Pharisees heard that Jesus had silenced the Sadducees, they themselves gathered together.
35
Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu;
One of them, an expert in the law, tested Him with a question:
36
Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
“Teacher, which commandment is the greatest in the Law?”
37
Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Jesus declared, “‘Love the Lord your God with all your heart and with all your soul and with all your mind.’
38
Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
This is the first and greatest commandment.
39
Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
And the second is like it: ‘Love your neighbor as yourself.’
40
Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.
All the Law and the Prophets hang on these two commandments.”
41
Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo?
While the Pharisees were assembled, Jesus questioned them:
42
Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.
“What do you think about the Christ? Whose son is He?” “David’s,” they answered.
43
Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,
Jesus said to them, “How then does David in the Spirit call Him ‘Lord’? For he says:
44
Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?
‘The Lord said to my Lord, “Sit at My right hand until I put Your enemies under Your feet.”’
45
Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?
So if David calls Him ‘Lord,’ how can He be David’s son?”
46
Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena.
No one was able to answer a word, and from that day on no one dared to question Him any further.