Mathayo 25 Swahili & English
Listen/Download AudioMathayo 25 (Swahili) | Matthew 25 (English) |
---|---|
Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi. Mathayo 25:1 |
"Then the Kingdom of Heaven will be like ten virgins, who took their lamps, and went out to meet the bridegroom. |
Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara. Mathayo 25:2 |
Five of them were foolish, and five were wise. |
Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao; Mathayo 25:3 |
Those who were foolish, when they took their lamps, took no oil with them, |
bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao. Mathayo 25:4 |
but the wise took oil in their vessels with their lamps. |
Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi. Mathayo 25:5 |
Now while the bridegroom delayed, they all slumbered and slept. |
Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki. Mathayo 25:6 |
But at midnight there was a cry, 'Behold! The bridegroom is coming! Come out to meet him!' |
Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao. Mathayo 25:7 |
Then all those virgins arose, and trimmed their lamps. |
Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. Mathayo 25:8 |
The foolish said to the wise, 'Give us some of your oil, for our lamps are going out.' |
Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie. Mathayo 25:9 |
But the wise answered, saying, 'What if there isn't enough for us and you? You go rather to those who sell, and buy for yourselves.' |
Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa. Mathayo 25:10 |
While they went away to buy, the bridegroom came, and those who were ready went in with him to the marriage feast, and the door was shut. |
Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie. Mathayo 25:11 |
Afterward the other virgins also came, saying, 'Lord, Lord, open to us.' |
Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi. Mathayo 25:12 |
But he answered, 'Most assuredly I tell you, I don't know you.' |
Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa. Mathayo 25:13 |
Watch therefore, for you don't know the day nor the hour in which the Son of Man is coming. |
Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake. Mathayo 25:14 |
"For it is like a man, going into another country, who called his own servants, and entrusted his goods to them. |
Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri. Mathayo 25:15 |
To one he gave five talents, to another two, to another one; to each according to his own ability. Then he went on his journey. |
Mara yule aliyepokea talanta tano akaenda, akafanya biashara nazo, akachuma faida talanta nyingine tano. Mathayo 25:16 |
Immediately he who received the five talents went and traded with them, and made another five talents. |
Vile vile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida. Mathayo 25:17 |
In like manner he also who got the two gained another two. |
Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake. Mathayo 25:18 |
But he who received the one went away and dug in the earth, and hid his lord's money. |
Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao. Mathayo 25:19 |
"Now after a long time the lord of those servants came, and reconciled accounts with them. |
Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida. Mathayo 25:20 |
He who received the five talents came and brought another five talents, saying, 'Lord, you delivered to me five talents. Behold, I have gained another five talents besides them.' |
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. Mathayo 25:21 |
"His lord said to him, 'Well done, good and faithful servant. You have been faithful over a few things, I will set you over many things. Enter into the joy of your lord.' |
Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida. Mathayo 25:22 |
"He also who got the two talents came and said, 'Lord, you delivered to me two talents. Behold, I have gained another two talents besides them.' |
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. Mathayo 25:23 |
"His lord said to him, 'Well done, good and faithful servant. You have been faithful over a few things, I will set you over many things. Enter into the joy of your lord.' |
Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya; Mathayo 25:24 |
"He also who had received the one talent came and said, 'Lord, I knew you that you are a hard man, reaping where you did not sow, and gathering where you did not scatter. |
basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako. Mathayo 25:25 |
I was afraid, and went away and hid your talent in the earth. Behold, you have what is yours.' |
Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; Mathayo 25:26 |
"But his lord answered him, 'You wicked and slothful servant. You knew that I reap where I didn't sow, and gather where I didn't scatter. |
basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake. Mathayo 25:27 |
You ought therefore to have deposited my money with the bankers, and at my coming I should have received back my own with interest. |
Basi, mnyang'anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. Mathayo 25:28 |
Take away therefore the talent from him, and give it to him who has the ten talents. |
Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa. Mathayo 25:29 |
For to everyone who has will be given, and he will have abundance, but from him who has not, even that which he has will be taken away. |
Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Mathayo 25:30 |
Throw out the unprofitable servant into the outer darkness, where there will be weeping and gnashing of teeth.' |
Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake; Mathayo 25:31 |
"But when the Son of Man comes in his glory, and all the holy angels with him, then he will sit on the throne of his glory. |
na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; Mathayo 25:32 |
Before him all the nations will be gathered, and he will separate them one from another, as a shepherd separates the sheep from the goats. |
atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto. Mathayo 25:33 |
He will set the sheep on his right hand, but the goats on the left. |
Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; Mathayo 25:34 |
Then the King will tell those on his right hand, 'Come, blessed of my Father, inherit the Kingdom prepared for you from the foundation of the world; |
kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; Mathayo 25:35 |
for I was hungry, and you gave me food to eat; I was thirsty, and you gave me drink; I was a stranger, and you took me in; |
nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia. Mathayo 25:36 |
naked, and you clothed me; I was sick, and you visited me; I was in prison, and you came to me.' |
Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha? Mathayo 25:37 |
"Then the righteous will answer him, saying, 'Lord, when did we see you hungry, and feed you; or thirsty, and give you a drink? |
Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika? Mathayo 25:38 |
When did we see you as a stranger, and take you in; or naked, and clothe you? |
Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia? Mathayo 25:39 |
When did we see you sick, or in prison, and come to you?' |
Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi. Mathayo 25:40 |
"The King will answer them, 'Most assuredly I tell you, inasmuch as you did it to one of the least of these my brothers{The word for "brothers" here may be also correctly translated "brothers and sisters" or "siblings."}, you did it to me.' |
Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake; Mathayo 25:41 |
Then he will say also to those on the left hand, 'Depart from me, you cursed, into the eternal fire which is prepared for the devil and his angels; |
kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe; Mathayo 25:42 |
for I was hungry, and you didn't give me food to eat; I was thirsty, and you gave me no drink; |
nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama. Mathayo 25:43 |
I was a stranger, and you didn't take me in; naked, and you didn't clothe me; sick, and in prison, and you didn't visit me.' |
Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie? Mathayo 25:44 |
"Then they will also answer, saying, 'Lord, when did we see you hungry, or thirsty, or a stranger, or naked, or sick, or in prison, and didn't help you?' |
Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi. Mathayo 25:45 |
"Then he will answer them, saying, 'Most assuredly I tell you, inasmuch as you didn't do it to one of the least of these, you didn't do it to me.' |
Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele. Mathayo 25:46 |
These will go away into eternal punishment, but the righteous into eternal life." |