Mathayo 23 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mathayo 23 (Swahili) Matthew 23 (English)

Kisha Yesu akawaambia makutano na wanafunzi wake, akasema, Mathayo 23:1

Then Jesus spoke to the multitudes and to his disciples,

Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa; Mathayo 23:2

saying, "The scribes and the Pharisees sat on Moses' seat.

basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi. Mathayo 23:3

All things therefore whatever they tell you to observe, observe and do, but don't do their works; for they say, and don't do.

Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao. Mathayo 23:4

For they bind heavy burdens that are grievous to be borne, and lay them on men's shoulders; but they themselves will not lift a finger to help them.

Tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu; kwa kuwa hupanua hirizi zao, huongeza matamvua yao; Mathayo 23:5

But all their works they do to be seen by men. They make their phylacteries broad, enlarge the fringes of their garments,

hupenda viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi, Mathayo 23:6

and love the place of honor at feasts, the best seats in the synagogues,

na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu, Rabi. Mathayo 23:7

the salutations in the marketplaces, and to be called 'Rabbi, Rabbi' by men.

Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu. Mathayo 23:8

But don't you be called 'Rabbi,' for one is your teacher, the Christ, and all of you are brothers.

Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni. Mathayo 23:9

Call no man on the earth your father, for one is your Father, he who is in heaven.

Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo. Mathayo 23:10

Neither be called masters, for one is your master, the Christ.

Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu. Mathayo 23:11

But he who is greatest among you will be your servant.

Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa. Mathayo 23:12

Whoever exalts himself will be humbled, and whoever humbles himself will be exalted.

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie. Mathayo 23:13

"Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! For you devour widows' houses, and as a pretense you make long prayers. Therefore you will receive greater condemnation.

[Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnakula nyumba za wajane, na kwa unafiki mnasali sala ndefu; kwa hiyo mtapata hukumu iliyo kubwa zaidi.] Mathayo 23:14

"But woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! Because you shut up the Kingdom of Heaven against men; for you don't enter in yourselves, neither do you allow those who are entering in to enter.{Some Greek manuscripts reverse the order of verses 13 and 14, and some omit verse 13, numbering verse 14 as 13.}

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnazunguka katika bahari na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja kuwa mwongofu; na akiisha kufanyika, mnamfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe. Mathayo 23:15

Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! For you travel around by sea and land to make one proselyte; and when he becomes one, you make him twice as much of a son of Gehenna as yourselves.

Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga. Mathayo 23:16

"Woe to you, you blind guides, who say, 'Whoever swears by the temple, it is nothing; but whoever swears by the gold of the temple, he is obligated.'

Wapumbavu ninyi na vipofu; maana ni ipi iliyo kubwa, ile dhahabu, au lile hekalu liitakasalo dhahabu? Mathayo 23:17

You blind fools! For which is greater, the gold, or the temple that sanctifies the gold?

Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga. Mathayo 23:18

'Whoever swears by the altar, it is nothing; but whoever swears by the gift that is on it, he is obligated.'

Vipofu ninyi; maana ni ipi iliyo kubwa, ile sadaka, au ile madhabahu iitakasayo sadaka? Mathayo 23:19

You blind fools! For which is greater, the gift, or the altar that sanctifies the gift?

Basi yeye aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hiyo, na kwa vitu vyote vilivyo juu yake. Mathayo 23:20

He therefore who swears by the altar, swears by it, and by everything on it.

Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo, na kwa yeye akaaye ndani yake. Mathayo 23:21

He who swears by the temple, swears by it, and by him who was living in it.

Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa yeye aketiye juu yake. Mathayo 23:22

He who swears by heaven, swears by the throne of God, and by him who sits on it.

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache. Mathayo 23:23

"Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! For you tithe mint, dill, and cumin,{ cumin is an aromatic seed from Cuminum cyminum, resembling caraway in flavor and appearance. It is used as a spice.} and have left undone the weightier matters of the law: justice, mercy, and faith. But you ought to have done these, and not to have left the other undone.

Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia. Mathayo 23:24

You blind guides, who strain out a gnat, and swallow a camel!

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang'anyi na kutokuwa na kiasi. Mathayo 23:25

"Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! For you clean the outside of the cup and of the platter, but within they are full of extortion and unrighteousness.{TR reads "self-indulgence" instead of "unrighteousness"}

Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi. Mathayo 23:26

You blind Pharisee, first clean the inside of the cup and of the platter, that the outside of it may become clean also.

Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote. Mathayo 23:27

"Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! For you are like whitened tombs, which outwardly appear beautiful, but inwardly are full of dead men's bones, and of all uncleanness.

Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi. Mathayo 23:28

Even so you also outwardly appear righteous to men, but inwardly you are full of hypocrisy and iniquity.

Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki, Mathayo 23:29

"Woe to you, scribes and Pharisees, hypocrites! For you build the tombs of the prophets, and decorate the tombs of the righteous,

na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii. Mathayo 23:30

and say, 'If we had lived in the days of our fathers, we wouldn't have been partakers with them in the blood of the prophets.'

Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii. Mathayo 23:31

Therefore you testify to yourselves that you are children of those who killed the prophets.

Kijazeni basi kipimo cha baba zenu. Mathayo 23:32

Fill up, then, the measure of your fathers.

Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? Mathayo 23:33

You serpents, you offspring of vipers, how will you escape the judgment of Gehenna?

Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji; Mathayo 23:34

Therefore, behold, I send to you prophets, wise men, and scribes. Some of them you will kill and crucify; and some of them you will scourge in your synagogues, and persecute from city to city;

hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu. Mathayo 23:35

that on you may come all the righteous blood shed on the earth, from the blood of righteous Abel to the blood of Zachariah son of Barachiah, whom you killed between the sanctuary and the altar.

Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki. Mathayo 23:36

Most assuredly I tell you, all these things will come upon this generation.

Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka! Mathayo 23:37

"Jerusalem, Jerusalem, who kills the prophets, and stones those who are sent to her! How often would I have gathered your children together, even as a hen gathers her chickens under her wings, and you would not!

Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa. Mathayo 23:38

Behold, your house is left to you desolate.

Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana. Mathayo 23:39

For I tell you, you will not see me from now on, until you say, 'Blessed is he who comes in the name of the Lord!'"