Mathayo BSB

Mathayo 25

Matthew Chapter 25

1
Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.
“At that time the kingdom of heaven will be like ten virgins who took their lamps and went out to meet the bridegroom.
2
Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.
Five of them were foolish, and five were wise.
3
Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;
The foolish ones took their lamps but did not take along any extra oil.
4
bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.
But the wise ones took oil in flasks along with their lamps.
5
Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.
When the bridegroom was delayed, they all became drowsy and fell asleep.
6
Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.
At midnight the cry rang out: ‘Here is the bridegroom! Come out to meet him!’
7
Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
Then all the virgins woke up and trimmed their lamps.
8
Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.
The foolish ones said to the wise, ‘Give us some of your oil; our lamps are going out.’
9
Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.
‘No,’ said the wise ones, ‘or there may not be enough for both us and you. Instead, go to those who sell oil and buy some for yourselves.’
10
Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
But while they were on their way to buy it, the bridegroom arrived. Those who were ready went in with him to the wedding banquet, and the door was shut.
11
Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.
Later the other virgins arrived and said, ‘Lord, lord, open the door for us!’
12
Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.
But he replied, ‘Truly I tell you, I do not know you.’
13
Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.
Therefore keep watch, because you do not know the day or the hour.
14
Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake.
For it is just like a man going on a journey, who called his servants and entrusted them with his possessions.
15
Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri.
To one he gave five talents, to another two talents, and to another one talent—each according to his own ability. And he went on his journey.
16
Mara yule aliyepokea talanta tano akaenda, akafanya biashara nazo, akachuma faida talanta nyingine tano.
The servant who had received the five talents went at once and put them to work and gained five more.
17
Vile vile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida.
Likewise, the one with the two talents gained two more.
18
Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake.
But the servant who had received the one talent went off, dug a hole in the ground, and hid his master’s money.
19
Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.
After a long time the master of those servants returned and settled accounts with them.
20
Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida.
The servant who had received the five talents came and presented five more. ‘Master,’ he said, ‘you entrusted me with five talents. See, I have gained five more.’
21
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.
His master replied, ‘Well done, good and faithful servant! You have been faithful with a few things; I will put you in charge of many things. Enter into the joy of your master!’
22
Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida.
The servant who had received the two talents also came and said, ‘Master, you entrusted me with two talents. See, I have gained two more.’
23
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.
His master replied, ‘Well done, good and faithful servant! You have been faithful with a few things; I will put you in charge of many things. Enter into the joy of your master!’
24
Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
Finally, the servant who had received the one talent came and said, ‘Master, I knew that you are a hard man, reaping where you have not sown and gathering where you have not scattered seed.
25
basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako.
So I was afraid and went out and hid your talent in the ground. See, you have what belongs to you.’
26
Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;
‘You wicked, lazy servant!’ replied his master. ‘You knew that I reap where I have not sown and gather where I have not scattered seed.
27
basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.
Then you should have deposited my money with the bankers, and on my return I would have received it back with interest.
28
Basi, mnyang'anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.
Therefore take the talent from him and give it to the one who has ten talents.
29
Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa.
For everyone who has will be given more, and he will have an abundance. But the one who does not have, even what he has will be taken away from him.
30
Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
And throw that worthless servant into the outer darkness, where there will be weeping and gnashing of teeth.’
31
Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;
When the Son of Man comes in His glory, and all the angels with Him, He will sit on His glorious throne.
32
na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;
All the nations will be gathered before Him, and He will separate the people one from another, as a shepherd separates the sheep from the goats.
33
atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.
He will place the sheep on His right and the goats on His left.
34
Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;
Then the King will say to those on His right, ‘Come, you who are blessed by My Father, inherit the kingdom prepared for you from the foundation of the world.
35
kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;
For I was hungry and you gave Me something to eat, I was thirsty and you gave Me something to drink, I was a stranger and you took Me in,
36
nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.
I was naked and you clothed Me, I was sick and you looked after Me, I was in prison and you visited Me.’
37
Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?
Then the righteous will answer Him, ‘Lord, when did we see You hungry and feed You, or thirsty and give You something to drink?
38
Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?
When did we see You a stranger and take You in, or naked and clothe You?
39
Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?
When did we see You sick or in prison and visit You?’
40
Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.
And the King will reply, ‘Truly I tell you, whatever you did for one of the least of these brothers of Mine, you did for Me.’
41
Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;
Then He will say to those on His left, ‘Depart from Me, you who are cursed, into the eternal fire prepared for the devil and his angels.
42
kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;
For I was hungry and you gave Me nothing to eat, I was thirsty and you gave Me nothing to drink,
43
nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.
I was a stranger and you did not take Me in, I was naked and you did not clothe Me, I was sick and in prison and you did not look after Me.’
44
Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?
And they too will reply, ‘Lord, when did we see You hungry or thirsty or a stranger or naked or sick or in prison, and did not minister to You?’
45
Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.
Then the King will answer, ‘Truly I tell you, whatever you did not do for one of the least of these, you did not do for Me.’
46
Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.
And they will go away into eternal punishment, but the righteous into eternal life.”

Chagua Sura