Luka 17

Luke Chapter 17

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!
He said to the disciples, "It is impossible that no occasions of stumbling should come, but woe to him through whom they come!
2
Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa.
It would be better for him if a millstone were hung around his neck, and he were thrown into the sea, rather than that he should cause one of these little ones to stumble.
3
Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.
Be careful. If your brother sins against you, rebuke him. If he repents, forgive him.
4
Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.
If he sins against you seven times in the day, and seven times returns, saying, 'I repent,' you shall forgive him."
5
Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani.
The apostles said to the Lord, "Increase our faith."
6
Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng'oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.
The Lord said, "If you had faith like a grain of mustard seed, you would tell this sycamore tree, 'Be uprooted, and be planted in the sea,' and it would obey you.
7
Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng'ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula?
But who is there among you, having a servant plowing or keeping sheep, that will say, when he comes in from the field, 'Come immediately and sit down at the table,'
8
Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa?
and will not rather tell him, 'Prepare my supper, clothe yourself properly, and serve me, while I eat and drink. Afterward you shall eat and drink'?
9
Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa?
Does he thank that servant because he did the things that were commanded? I think not.
10
Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.
Even so you also, when you have done all the things that are commanded you, say, 'We are unworthy servants. We have done our duty.'"
11
Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.
It happened as he was on his way to Jerusalem, that he was passing along the borders of Samaria and Galilee.
12
Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
As he entered into a certain village, ten men who were lepers met him, who stood at a distance.
13
wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
They lifted up their voices, saying, "Jesus, Master, have mercy on us!"
14
Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
When he saw them, he said to them, "Go and show yourselves to the priests." It happened that as they went, they were cleansed.
15
Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;
One of them, when he saw that he was healed, turned back, glorifying God with a loud voice.
16
akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
He fell on his face at Jesus' feet, giving him thanks; and he was a Samaritan.
17
Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?
Jesus answered, "Weren't the ten cleansed? But where are the nine?
18
Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?
Were there none found who returned to give glory to God, except this stranger?"
19
Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.
Then he said to him, "Get up, and go your way. Your faith has healed you."
20
Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza;
Being asked by the Pharisees when the Kingdom of God would come, he answered them, "The Kingdom of God doesn't come with observation;
21
wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu.
neither will they say, 'Look, here!' or, 'Look, there!' for behold, the Kingdom of God is within you."
22
Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.
He said to the disciples, "The days will come, when you will desire to see one of the days of the Son of Man, and you will not see it.
23
Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate;
They will tell you, 'Look, here!' or 'Look, there!' Don't go away, nor follow after them,
24
kwa kuwa, kama vile umeme umulikavyo toka upande huu chini ya mbingu hata upande huu chini ya mbingu, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
for as the lightning, when it flashes out of the one part under the sky, shines to the other part under the sky; so will the Son of Man be in his day.
25
Lakini kwanza, hana budi kupata mateso mengi, na kukataliwa na kizazi hiki.
But first, he must suffer many things and be rejected by this generation.
26
Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.
As it happened in the days of Noah, even so will it be also in the days of the Son of Man.
27
Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.
They ate, they drank, they married, they were given in marriage, until the day that Noah entered into the ark, and the flood came, and destroyed them all.
28
Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;
Likewise, even as it happened in the days of Lot: they ate, they drank, they bought, they sold, they planted, they built;
29
lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.
but in the day that Lot went out from Sodom, it rained fire and sulfur from the sky, and destroyed them all.
30
Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu.
It will be the same way in the day that the Son of Man is revealed.
31
Katika siku ile, aliye juu ya dari, na vyombo vyake vimo ndani ya nyumba, asishuke ili kuvitwaa; na kadhalika, aliye shambani asirejee nyuma.
In that day, he who will be on the housetop, and his goods in the house, let him not go down to take them away. Let him who is in the field likewise not turn back.
32
Mkumbukeni mkewe Lutu.
Remember Lot's wife!
33
Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya.
Whoever seeks to save his life loses it, but whoever loses his life preserves it.
34
Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
I tell you, in that night there will be two people in one bed. The one will be taken, and the other will be left.
35
Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
There will be two grinding grain together. One will be taken, and the other will be left."
36
Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.]
{Some Greek manuscripts add: "Two will be in the field, the one taken, and the other left."}
37
Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai.
They answering, asked him, "Where, Lord?" He said to them, "Where the body is, there will the vultures also be gathered together."
« 16 18 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)