Luka 17 Swahili & English

Listen/Download Audio
Luka 17 (Swahili) Luke 17 (English)

Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake! Luka 17:1

He said to the disciples, "It is impossible that no occasions of stumbling should come, but woe to him through whom they come!

Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa. Luka 17:2

It would be better for him if a millstone were hung around his neck, and he were thrown into the sea, rather than that he should cause one of these little ones to stumble.

Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe. Luka 17:3

Be careful. If your brother sins against you, rebuke him. If he repents, forgive him.

Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe. Luka 17:4

If he sins against you seven times in the day, and seven times returns, saying, 'I repent,' you shall forgive him."

Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani. Luka 17:5

The apostles said to the Lord, "Increase our faith."

Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng'oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii. Luka 17:6

The Lord said, "If you had faith like a grain of mustard seed, you would tell this sycamore tree, 'Be uprooted, and be planted in the sea,' and it would obey you.

Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng'ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula? Luka 17:7

But who is there among you, having a servant plowing or keeping sheep, that will say, when he comes in from the field, 'Come immediately and sit down at the table,'

Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa? Luka 17:8

and will not rather tell him, 'Prepare my supper, clothe yourself properly, and serve me, while I eat and drink. Afterward you shall eat and drink'?

Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa? Luka 17:9

Does he thank that servant because he did the things that were commanded? I think not.

Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya. Luka 17:10

Even so you also, when you have done all the things that are commanded you, say, 'We are unworthy servants. We have done our duty.'"

Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya. Luka 17:11

It happened as he was on his way to Jerusalem, that he was passing along the borders of Samaria and Galilee.

Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali, Luka 17:12

As he entered into a certain village, ten men who were lepers met him, who stood at a distance.

wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu! Luka 17:13

They lifted up their voices, saying, "Jesus, Master, have mercy on us!"

Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika. Luka 17:14

When he saw them, he said to them, "Go and show yourselves to the priests." It happened that as they went, they were cleansed.

Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu; Luka 17:15

One of them, when he saw that he was healed, turned back, glorifying God with a loud voice.

akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria. Luka 17:16

He fell on his face at Jesus' feet, giving him thanks; and he was a Samaritan.

Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi? Luka 17:17

Jesus answered, "Weren't the ten cleansed? But where are the nine?

Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu? Luka 17:18

Were there none found who returned to give glory to God, except this stranger?"

Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa. Luka 17:19

Then he said to him, "Get up, and go your way. Your faith has healed you."

Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza; Luka 17:20

Being asked by the Pharisees when the Kingdom of God would come, he answered them, "The Kingdom of God doesn't come with observation;

wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu. Luka 17:21

neither will they say, 'Look, here!' or, 'Look, there!' for behold, the Kingdom of God is within you."

Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione. Luka 17:22

He said to the disciples, "The days will come, when you will desire to see one of the days of the Son of Man, and you will not see it.

Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate; Luka 17:23

They will tell you, 'Look, here!' or 'Look, there!' Don't go away, nor follow after them,

kwa kuwa, kama vile umeme umulikavyo toka upande huu chini ya mbingu hata upande huu chini ya mbingu, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake. Luka 17:24

for as the lightning, when it flashes out of the one part under the sky, shines to the other part under the sky; so will the Son of Man be in his day.

Lakini kwanza, hana budi kupata mateso mengi, na kukataliwa na kizazi hiki. Luka 17:25

But first, he must suffer many things and be rejected by this generation.

Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu. Luka 17:26

As it happened in the days of Noah, even so will it be also in the days of the Son of Man.

Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote. Luka 17:27

They ate, they drank, they married, they were given in marriage, until the day that Noah entered into the ark, and the flood came, and destroyed them all.

Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga; Luka 17:28

Likewise, even as it happened in the days of Lot: they ate, they drank, they bought, they sold, they planted, they built;

lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote. Luka 17:29

but in the day that Lot went out from Sodom, it rained fire and sulfur from the sky, and destroyed them all.

Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu. Luka 17:30

It will be the same way in the day that the Son of Man is revealed.

Katika siku ile, aliye juu ya dari, na vyombo vyake vimo ndani ya nyumba, asishuke ili kuvitwaa; na kadhalika, aliye shambani asirejee nyuma. Luka 17:31

In that day, he who will be on the housetop, and his goods in the house, let him not go down to take them away. Let him who is in the field likewise not turn back.

Mkumbukeni mkewe Lutu. Luka 17:32

Remember Lot's wife!

Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya. Luka 17:33

Whoever seeks to save his life loses it, but whoever loses his life preserves it.

Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa. Luka 17:34

I tell you, in that night there will be two people in one bed. The one will be taken, and the other will be left.

Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa. Luka 17:35

There will be two grinding grain together. One will be taken, and the other will be left."

Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.] Luka 17:36

{Some Greek manuscripts add: "Two will be in the field, the one taken, and the other left."}

Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai. Luka 17:37

They answering, asked him, "Where, Lord?" He said to them, "Where the body is, there will the vultures also be gathered together."