Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.
Now after these things, the Lord also appointed seventy others, and sent them two by two ahead of him{literally, "before his face"} into every city and place, where he was about to come.
Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.
Then he said to them, "The harvest is indeed plentiful, but the laborers are few. Pray therefore to the Lord of the harvest, that he may send out laborers into his harvest.
Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.
Go your ways. Behold, I send you out as lambs among wolves.
Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njiani.
Carry no purse, nor wallet, nor sandals. Greet no one on the way.
Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu;
Into whatever house you enter, first say, 'Peace be to this house.'
na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu.
If a son of peace is there, your peace will rest on him; but if not, it will return to you.
Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.
Remain in that same house, eating and drinking the things they give, for the laborer is worthy of his wages. Don't go from house to house.
Na mji wo wote mtakaouingia, wakiwakaribisha, vileni vyakula viwekwavyo mbele yenu;
Into whatever city you enter, and they receive you, eat the things that are set before you.
waponyeni wagonjwa waliomo, waambieni, Ufalme wa Mungu umewakaribia.
Heal the sick who are therein, and tell them, 'The Kingdom of God has come near to you.'
Na mji wo wote mtakaouingia, nao hawawakaribishi, tokeni humo, nanyi mkipita katika njia zake semeni,
But into whatever city you enter, and they don't receive you, go out into the streets of it and say,
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyogandamana na miguu yetu tunayakung'uta juu yenu. Lakini jueni hili, ya kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia.
'Even the dust from your city that clings to us, we wipe off against you. Nevertheless know this, that the Kingdom of God has come near to you.'
Nawaambia ya kwamba siku ile itakuwa rahisi zaidi Sodoma kuistahimili adhabu yake kuliko mji huo.
I tell you, it will be more tolerable in that day for Sodom than for that city.
Ole wako Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza hiyo iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu tangu hapo, huku wakiketi katika nguo za kigunia na majivu.
"Woe to you, Chorazin! Woe to you, Bethsaida! For if the mighty works had been done in Tyre and Sidon which were done in you, they would have repented long ago, sitting in sackcloth and ashes.
Lakini, siku ya hukumu itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zake kuliko ninyi.
But it will be more tolerable for Tyre and Sidon in the judgment than for you.
Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa hata mbinguni? Utashushwa hata kuzimu.
You, Capernaum, who are exalted to heaven, will be brought down to Hades.{Hades is the lower realm of the dead, or Hell.}
Awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.
Whoever listens to you listens to me, and whoever rejects you rejects me. Whoever rejects me rejects him who sent me."
Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.
The seventy returned with joy, saying, "Lord, even the demons are subject to us in your name!"
Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
He said to them, "I saw Satan having fallen like lightning from heaven.
Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.
Behold, I give you authority to tread on serpents and scorpions, and over all the power of the enemy. Nothing will in any way hurt you.
Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.
Nevertheless, don't rejoice in this, that the spirits are subject to you, but rejoice that your names are written in heaven."
Saa ile ile alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza.
In that same hour Jesus rejoiced in the Holy Spirit, and said, "I thank you, O Father, Lord of heaven and earth, that you have hidden these things from the wise and understanding, and revealed them to little children. Yes, Father, for so it was well-pleasing in your sight."
Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu, wala hakuna amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia.
Turning to the disciples, he said, "All things have been delivered to me by my Father. No one knows who the Son is, except the Father, and who the Father is, except the Son, and he to whomever the Son desires to reveal him."
Akawageukia wanafunzi wake, akasema nao kwa faragha, Heri macho yaonayo mnayoyaona ninyi.
Turning to the disciples, he said privately, "Blessed are the eyes which see the things that you see,
Kwa kuwa nawaambia ya kwamba manabii wengi na wafalme walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi wasiyaone; na kuyasikia mnayoyasikia ninyi wasiyasikie.
for I tell you that many prophets and kings desired to see the things which you see, and didn't see them, and to hear the things which you hear, and didn't hear them."
Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?
Behold, a certain lawyer stood up and tested him, saying, "Teacher, what shall I do to inherit eternal life?"
Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?
He said to him, "What is written in the law? How do you read it?"
Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.
He answered, "You shall love the Lord your God with all your heart, with all your soul, with all your strength, and with all your mind; and your neighbor as yourself."
Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.
He said to him, "You have answered correctly. Do this, and you will live."
Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?
But he, desiring to justify himself, asked Jesus, "Who is my neighbor?"
Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang'anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
Jesus answered, "A certain man was going down from Jerusalem to Jericho, and he fell among robbers, who both stripped him and beat him, and departed, leaving him half dead.
Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
By chance a certain priest was going down that way. When he saw him, he passed by on the other side.
Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
In the same way a Levite also, when he came to the place, and saw him, passed by on the other side.
Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,
But a certain Samaritan, as he traveled, came where he was. When he saw him, he was moved with compassion,
akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.
came to him, and bound up his wounds, pouring on oil and wine. He set him on his own animal, and brought him to an inn, and took care of him.
Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.
On the next day, when he departed, he took out two denarii, and gave them to the host, and said to him, 'Take care of him. Whatever you spend beyond that, I will repay you when I return.'
Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang'anyi?
Now which of these three do you think seemed to be a neighbor to him who fell among the robbers?"
Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo.
He said, "He who showed mercy on him." Then Jesus said to him, "Go and do likewise."
Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake.
It happened as they went on their way, he entered into a certain village, and a certain woman named Martha received him into her house.
Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake.
She had a sister called Mary, who also sat at Jesus' feet, and heard his word.
Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie.
But Martha was distracted with much serving, and she came up to him, and said, "Lord, don't you care that my sister left me to serve alone? Ask her therefore to help me."
Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi;
Jesus answered her, "Martha, Martha, you are anxious and troubled about many things,
lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa.
but one thing is needed. Mary has chosen the good part, which will not be taken away from her."