2 Samweli 18 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Samweli 18 (Swahili) 2nd Samuel 18 (English)

Kisha Daudi akawahesabu watu waliokuwa pamoja naye, akaweka maakida wa elfu elfu, na maakida wa mia mia juu yao. 2 Samweli 18:1

David numbered the people who were with him, and set captains of thousands and captains of hundreds over them.

Daudi akawapeleka hao watu vitani, theluthi moja chini ya mkono wa Yoabu, na theluthi ya pili chini ya mkono wa Abishai, mwana wa Seruya nduguye Yoabu, na theluthi ya tatu chini ya mkono wa Itai, Mgiti. Mfalme akawaambia watu, Bila shaka mimi mwenyewe nami nitatoka pamoja nanyi. 2 Samweli 18:2

David sent forth the people, a third part under the hand of Joab, and a third part under the hand of Abishai the son of Zeruiah, Joab's brother, and a third part under the hand of Ittai the Gittite. The king said to the people, I will surely go forth with you myself also.

Lakini watu wakasema, Wewe usitoke nje; kwa maana tukikimbia, hawatatuona sisi kuwa kitu; au tukifa nusu yetu, hawatatuona kuwa kitu; lakini wewe u wa thamani kuliko watu elfu kumi katika sisi; kwa hivyo sasa ni afadhali ukae tayari kutusaidia toka mjini. 2 Samweli 18:3

But the people said, You shall not go forth: for if we flee away, they will not care for us; neither if half of us die, will they care for us: but you are worth ten thousand of us; therefore now it is better that you are ready to help us out of the city.

Mfalme akawaambia, Yaliyo mema machoni penu ndiyo nitakayofanya. Basi mfalme akasimama kando ya lango, na hao watu wakatoka kwa elfu zao na mia zao. 2 Samweli 18:4

The king said to them, What seems you best I will do. The king stood by the gate-side, and all the people went out by hundreds and by thousands.

Mfalme akawaamuru Yoabu na Abishai na Itai, akasema, Mtendeeni yule kijana, Absalomu, kwa upole kwa ajili yangu. Nao watu wote wakasikia, mfalme alipowaagiza maakida wote katika habari za Absalomu. 2 Samweli 18:5

The king commanded Joab and Abishai and Ittai, saying, Deal gently for my sake with the young man, even with Absalom. All the people heard when the king gave all the captains charge concerning Absalom.

Hivyo watu wakatoka waende nyikani ili kupigana na Israeli; na vita vikatokea ndani ya msitu wa Efraimu. 2 Samweli 18:6

So the people went out into the field against Israel: and the battle was in the forest of Ephraim.

Watu wa Israeli wakapigwa huko mbele ya watumishi wa Daudi, kukawa na maangamizo makuu huko siku ile, ya watu ishirini elfu. 2 Samweli 18:7

The people of Israel were struck there before the servants of David, and there was a great slaughter there that day of twenty thousand men.

Kwa maana vita vilienea huko juu ya uso wote wa nchi; na siku ile huo msitu ukala watu wengi kuliko wale walioliwa na upanga. 2 Samweli 18:8

For the battle was there spread over the surface of all the country; and the forest devoured more people that day than the sword devoured.

Na kwa bahati Absalomu akakutana na watumishi wa Daudi. Naye Absalomu alikuwa amepanda nyumbu wake, na yule nyumbu akapita chini ya matawi manene ya mwaloni mkubwa, hata kichwa chake kikakwama katika mwaloni huo, akanyakuliwa juu kati ya mbingu na nchi; na yule nyumbu aliyekuwa chini yake akaenda mbele. 2 Samweli 18:9

Absalom happened to meet the servants of David. Absalom was riding on his mule, and the mule went under the thick boughs of a great oak, and his head caught hold of the oak, and he was taken up between the sky and earth; and the mule that was under him went on.

Basi mtu mmoja akaona hayo, akaenda akamwambia Yoabu, akasema, Tazama, mimi nalimwona Absalomu ametundikwa katika mwaloni. 2 Samweli 18:10

A certain man saw it, and told Joab, and said, Behold, I saw Absalom hanging in an oak.

Naye Yoabu akamwambia mtu yule aliyempasha habari, Je! Wewe umeona haya; Mbona, basi, hukumpiga hata nchi papo hapo? Nami ningalikupa fedha kumi na mshipi. 2 Samweli 18:11

Joab said to the man who told him, Behold, you saw it, and why didn't you strike him there to the ground? and I would have given you ten [pieces of] silver, and a sash.

Yule mtu akamwambia Yoabu, Kama ningalipata fedha elfu mkononi mwangu, hata hivyo singalinyosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme masikioni mwetu alikuagiza wewe, na Abishai na Itai, akisema, Angalieni sana mtu awaye yote asimguse yule kijana, Absalomu. 2 Samweli 18:12

The man said to Joab, Though I should receive a thousand [pieces of] silver in my hand, I still wouldn't put forth my hand against the king's son; for in our hearing the king charged you and Abishai and Ittai, saying, Beware that none touch the young man Absalom.

Na tena, kama ningaliitendea roho yake kwa hila; (wala hapana neno lo lote liwezalo kufichwa mbele ya mfalme); ndipo wewe mwenyewe ungalijitenga. 2 Samweli 18:13

Otherwise if I had dealt falsely against his life (and there is no matter hid from the king), then you yourself would have set yourself against [me].

Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua vyemba vitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa akali hai katikati ya ule mwaloni. 2 Samweli 18:14

Then said Joab, I may not wait thus with you. He took three darts in his hand, and thrust them through the heart of Absalom, while he was yet alive in the midst of the oak.

Kisha vijana kumi, waliomchukulia Yoabu silaha zake wakamzunguka, wakampiga Absalomu, na kumwua. 2 Samweli 18:15

Ten young men who bore Joab's armor compassed about and struck Absalom, and killed him.

Kisha Yoabu akapiga tarumbeta, wakarudi watu toka kuwafuatia Israeli; kwani Yoabu akawazuia watu. 2 Samweli 18:16

Joab blew the trumpet, and the people returned from pursuing after Israel; for Joab held back the people.

Nao wakamtwaa Absalomu wakamtupa katika shimo kubwa mle msituni, wakaweka juu yake chungu kubwa sana la mawe; kisha Israeli wote wakakimbia kila mtu hemani mwake. 2 Samweli 18:17

They took Absalom, and cast him into the great pit in the forest, and raised over him a very great heap of stones: and all Israel fled everyone to his tent.

Huyo Absalomu alipokuwa yu hai alikuwa ameitwaa na kujiinulia ile nguzo iliyoko bondeni mwa mfalme; kwa maana alisema, Mimi sina mtoto wa kulikumbusha jina langu; akaiita hiyo nguzo kwa jina lake mwenyewe nayo inaitwa ziara la Absalomu hata hivi leo. 2 Samweli 18:18

Now Absalom in his lifetime had taken and reared up for himself the pillar, which is in the king's dale; for he said, I have no son to keep my name in memory: and he called the pillar after his own name; and it is called Absalom's monument, to this day.

Basi Ahimaasi, mwana wa Sadoki, akasema, Niende mbio sasa, nikampelekee mfalme habari, jinsi Bwana alivyomlipiza kisasi juu ya adui zake. 2 Samweli 18:19

Then said Ahimaaz the son of Zadok, Let me now run, and bear the king news, how that Yahweh has avenged him of his enemies.

Yoabu akamwambia, Wewe hutakuwa mchukua habari leo, siku nyingine utachukua habari; lakini leo hutachukua habari, kwa sababu mwana wa mfalme amekufa. 2 Samweli 18:20

Joab said to him, You shall not be the bearer of news this day, but you shall bear news another day; but this day you shall bear no news, because the king's son is dead.

Ndipo Yoabu akamwambia Mkushi mmoja, Nenda ukamwambie mfalme hayo uliyoyaona. Na huyo Mkushi akajiinamisha mbele ya Yoabu, akaenda zake mbio. 2 Samweli 18:21

Then said Joab to the Cushite, Go, tell the king what you have seen. The Cushite bowed himself to Joab, and ran.

Ndipo Ahimaasi, mwana wa Sadoki, akamwambia Yoabu mara ya pili, Haidhuru, tafadhali nipe ruhusa, nipige mbio na mimi nyuma ya huyo Mkushi. Naye Yoabu akasema, Mbona wewe unataka kupiga mbio, mwanangu, kwa maana hutapata kitu kwa habari hizo unazopeleka? 2 Samweli 18:22

Then said Ahimaaz the son of Zadok yet again to Joab, But come what may, Please let me also run after the Cushite. Joab said, Why will you run, my son, seeing that you will have no reward for the news?

Akasema, Haidhuru, nitapiga mbio. Akamwambia, Haya, piga mbio. Ndipo Ahimaasi akapiga mbio, akishika njia ya uwandani, akampita yule Mkushi. 2 Samweli 18:23

But come what may, [said he], I will run. He said to him, Run. Then Ahimaaz ran by the way of the Plain, and outran the Cushite.

Basi Daudi alikuwa ameketi kati ya malango mawili; mlinzi akapanda juu hata dari ya lile lango hata ukutani, akainua macho yake, akaangalia, na tazama, mtu anakuja mbio peke yake. 2 Samweli 18:24

Now David was sitting between the two gates: and the watchman went up to the roof of the gate to the wall, and lifted up his eyes, and looked, and, behold, a man running alone.

Mlinzi akalia, akamwambia mfalme. Naye mfalme akasema, Kama yu peke yake, ana habari kinywani mwake. Akaja mbio, akakaribia. 2 Samweli 18:25

The watchman cried, and told the king. The king said, If he be alone, there is news in his mouth. He came apace, and drew near.

Kisha huyo mlinzi akaona mtu mwingine anapiga mbio; mlinzi akamwita bawabu, akasema, Angalia, mtu mwingine anakuja mbio peke yake. Mfalme akasema, Huyu naye analeta habari. 2 Samweli 18:26

The watchman saw another man running; and the watchman called to the porter, and said, Behold, [another] man running alone. The king said, He also brings news.

Na huyo mlinzi akasema, Nionavyo mimi, kupiga mbio kwake yule wa kwanza ni kama kupiga mbio kwake Ahimaasi, mwana wa Sadoki. Naye mfalme akasema, Yeye ni mtu mwema, anakuja na habari njema. 2 Samweli 18:27

The watchman said, I think the running of the foremost is like the running of Ahimaaz the son of Zadok. The king said, He is a good man, and comes with good news.

Ahimaasi akainua sauti yake, akamwambia mfalme, Amani. Akainama mbele ya mfalme kifudifudi, akasema, Ahimidiwe Bwana, Mungu wako, aliyewatoa watu hao walioiinua mikono yao juu ya bwana wangu, mfalme. 2 Samweli 18:28

Ahimaaz called, and said to the king, All is well. He bowed himself before the king with his face to the earth, and said, Blessed be Yahweh your God, who has delivered up the men who lifted up their hand against my lord the king.

Mfalme akauliza, Je! Yule kijana, Absalomu, yu salama? Ahimaasi akajibu, Yoabu aliponituma mimi mtumishi wa mfalme, mimi mtumishi wako, naliona kishindo kikubwa, lakini sikujua sababu yake. 2 Samweli 18:29

The king said, Is it well with the young man Absalom? Ahimaaz answered, When Joab sent the king's servant, even me your servant, I saw a great tumult, but I don't know what it was.

Naye mfalme akasema, Geuka, usimame hapa. Akageuka, akasimama. 2 Samweli 18:30

The king said, Turn aside, and stand here. He turned aside, and stood still.

Na tazama, yule Mkushi akafika; Mkushi akasema, Nina habari kwa bwana wangu mfalme; kwa maana Bwana amekulipizia kisasi leo juu ya hao wote walioinuka kupigana nawe. 2 Samweli 18:31

Behold, the Cushite came; and the Cushite said, News for my lord the king; for Yahweh has avenged you this day of all those who rose up against you.

Naye mfalme akamwambia yule Mkushi, Yule kijana, Absalomu, je! Yu salama? Yule Mkushi akajibu, Adui za bwana wangu mfalme, na wote wainukao ili kukudhuru, na wawe kama alivyo yule kijana. 2 Samweli 18:32

The king said to the Cushite, Is it well with the young man Absalom? The Cushite answered, The enemies of my lord the king, and all who rise up against you to do you hurt, be as that young man is.

Naye mfalme akataabika sana, akapanda juu, akaingia kile chumba kilichokuwa juu ya lango, akalia; na katika kwenda kwake alisema hivi, Mwanangu Absalomu! Ee mwanangu! Mwanangu Absalomu! Laiti ningalikufa badala yako, Absalomu, mwanangu, mwanangu!

2 Samweli 18:33

The king was much moved, and went up to the chamber over the gate, and wept: and as he went, thus he said, my son Absalom, my son, my son Absalom! would I had died for you, Absalom, my son, my son!