2 Samweli 1 Swahili & English
Listen/Download Audio2 Samweli 1 (Swahili) | 2nd Samuel 1 (English) |
---|---|
Ikawa baada ya kufa kwake Sauli, hapo Daudi aliporudi katika kuwaua Waamaleki, naye Daudi amekaa siku mbili katika Siklagi; 2 Samweli 1:1 |
It happened after the death of Saul, when David was returned from the slaughter of the Amalekites, and David had abode two days in Ziklag; |
hata siku ya tatu ikawa, tazama! Akaja mtu kutoka kambi ya Sauli, nguo zake zimeraruliwa, tena ana mavumbi kichwani mwake; basi, ikawa alipomfikia Daudi, akaanguka chini, akamsujudia. 2 Samweli 1:2 |
it happened on the third day, that behold, a man came out of the camp from Saul, with his clothes torn, and earth on his head: and so it was, when he came to David, that he fell to the earth, and did obeisance. |
Daudi akamwambia, Umetoka wapi? Akamwambia, Nimeokoka katika kambi ya Israeli. 2 Samweli 1:3 |
David said to him, From whence come you? He said to him, Out of the camp of Israel am I escaped. |
Daudi akamwambia, Yalikwendaje? Tafadhali uniambie. Akajibu, Watu wamekimbia vitani, tena watu wengi wameanguka wamekufa; hata Sauli naye na Yonathani, mwanawe, wamekufa. 2 Samweli 1:4 |
David said to him, How went the matter? Please tell me. He answered, The people are fled from the battle, and many of the people also are fallen and dead; and Saul and Jonathan his son are dead also. |
Daudi akamwambia yule kijana aliyempa habari, Umejuaje ya kuwa Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa? 2 Samweli 1:5 |
David said to the young man who told him, How know you that Saul and Jonathan his son are dead? |
Yule kijana aliyempa habari akasema, Nalikuwapo kwa nasibu juu ya kilima cha Gilboa, na tazama, Sauli alikuwa ameegemea fumo lake; na tazama, magari na wapanda farasi wanamfuatia kwa kasi. 2 Samweli 1:6 |
The young man who told him said, As I happened by chance on Mount Gilboa, behold, Saul was leaning on his spear; and, behold, the chariots and the horsemen followed hard after him. |
Naye alipotazama nyuma, akaniona, akaniita. Nikajibu, Mimi hapa. 2 Samweli 1:7 |
When he looked behind him, he saw me, and called to me. I answered, Here am I. |
Akaniambia, U nani wewe? Nikamjibu, Mimi ni Mwamaleki. 2 Samweli 1:8 |
He said to me, Who are you? I answered him, I am an Amalekite. |
Akaniambia, Tafadhali simama karibu nami, ukaniue, maana shida imenipata; kwa sababu roho yangu ingali hai ndani yangu. 2 Samweli 1:9 |
He said to me, Stand, I pray you, beside me, and kill me; for anguish has taken hold of me, because my life is yet whole in me. |
Basi, nikasimama karibu naye, nikamwua, kwa sababu nalijua hakika ya kuwa hawezi kupona baada ya kuanguka; kisha nikaitwaa ile taji iliyokuwa kichwani mwake, na kikuku kilichokuwa mkononi mwake, nami nimevileta hapa kwa bwana wangu. 2 Samweli 1:10 |
So I stood beside him, and killed him, because I was sure that he could not live after that he was fallen: and I took the crown that was on his head, and the bracelet that was on his arm, and have brought them here to my lord. |
Ndipo Daudi akashika nguo zake akazirarua na kadhalika watu wote waliokuwa pamoja naye; 2 Samweli 1:11 |
Then David took hold on his clothes, and tore them; and likewise all the men who were with him: |
wakaomboleza, wakalia, wakafunga hata jioni, kwa ajili ya Sauli, na kwa ajili ya Yonathani mwanawe, na kwa ajili ya watu wa Bwana na kwa ajili ya nyumba ya Israeli; kwa sababu wameanguka kwa upanga. 2 Samweli 1:12 |
and they mourned, and wept, and fasted until even, for Saul, and for Jonathan his son, and for the people of Yahweh, and for the house of Israel; because they were fallen by the sword. |
Naye Daudi akamwambia yule kijana aliyempa habari, Watoka wapi wewe? Akajibu, Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki. 2 Samweli 1:13 |
David said to the young man who told him, Whence are you? He answered, I am the son of a foreigner, an Amalekite. |
Daudi akamwambia, Jinsi gani hukuogopa kuunyosha mkono wako umwangamize masihi wa BWANA? 2 Samweli 1:14 |
David said to him, How were you not afraid to put forth your hand to destroy Yahweh's anointed? |
Ndipo Daudi akamwita mmoja wa vijana, akamwambia, Mwendee, ukamwangukie. Basi akampiga hata akafa. 2 Samweli 1:15 |
David called one of the young men, and said, Go near, and fall on him. He struck him, so that he died. |
Daudi akamwambia, Damu yako na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe; maana umejishuhudia nafsi yako ukisema, Nimemwua masihi wa Bwana. 2 Samweli 1:16 |
David said to him, Your blood be on your head; for your mouth has testified against you, saying, I have slain Yahweh's anointed. |
Basi Daudi akamwomboleza Sauli, na Yonathani, mwanawe, maombolezo haya; 2 Samweli 1:17 |
David lamented with this lamentation over Saul and over Jonathan his son |
(kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Yashari), akasema, Wana wa Yuda na wafundishwe haya, 2 Samweli 1:18 |
(and he bade them teach the children of Judah [the song of] the bow: behold, it is written in the book of Jashar): |
Walio fahari yako, Ee Israeli Juu ya mahali pako palipoinuka wameuawa; Jinsi mashujaa walivyoanguka! 2 Samweli 1:19 |
Your glory, Israel, is slain on your high places! How are the mighty fallen! |
Msiyahubiri mambo haya katika Gathi, Msiyatangaze katika njia za Ashkeloni; Wasije wakashangilia binti za Wafilisti, Binti za wasiotahiriwa wakasimanga. 2 Samweli 1:20 |
Don't tell it in Gath, Don't publish it in the streets of Ashkelon; Lest the daughters of the Philistines rejoice, Lest the daughters of the uncircumcised triumph. |
Enyi milima ya Gilboa, visiwepo juu yenu Umande wala mvua, wala mashamba ya matoleo; Maana ndipo ilipotupwa kwa aibu ngao ya shujaa, Ngao yake Sauli, pasipo kutiwa mafuta. 2 Samweli 1:21 |
You mountains of Gilboa, Let there be no dew nor rain on you, neither fields of offerings: For there the shield of the mighty was vilely cast away, The shield of Saul, not anointed with oil. |
Kutoka kwa damu yao waliouawa, Kutoka kwa shahamu yao mashujaa, Upinde wa Yonathani haukurudi nyuma, Wala upanga wa Sauli haukurudi bure. 2 Samweli 1:22 |
From the blood of the slain, from the fat of the mighty, The bow of Jonathan didn't turn back, The sword of Saul didn't return empty. |
Sauli na Yonathani walipendwa na kupendeza Maishani wala mautini hawakutengwa; Walikuwa wepesi kuliko tai, Walikuwa hodari kuliko simba. 2 Samweli 1:23 |
Saul and Jonathan were lovely and pleasant in their lives, In their death they were not divided: They were swifter than eagles, They were stronger than lions. |
Enyi binti za Israeli, mlilieni Huyo Sauli, ambaye aliwavika Mavazi mekundu kwa anasa, Akazipamba nguo zenu dhahabu. 2 Samweli 1:24 |
You daughters of Israel, weep over Saul, Who clothed you in scarlet delicately, Who put ornaments of gold on your clothing. |
Jinsi mashujaa walivyoanguka Katikati ya vita! Ee Yonathani, wewe umeuawa Juu ya mahali pako palipoinuka 2 Samweli 1:25 |
How are the mighty fallen in the midst of the battle! Jonathan is slain on your high places. |
Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani, ndugu yangu, Ulikuwa ukinipendeza sana; Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, Kupita upendo wa wanawake. 2 Samweli 1:26 |
I am distressed for you, my brother Jonathan: Very pleasant have you been to me: Your love to me was wonderful, Passing the love of women. |
Jinsi mashujaa walivyoanguka, Na silaha za vita zilivyoangamia! 2 Samweli 1:27 |
How are the mighty fallen, The weapons of war perished! |