Mithali 29

Proverbs Chapter 29

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa.
He who is often rebuked and stiffens his neck Will be destroyed suddenly, with no remedy.
2
Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua.
When the righteous thrive, the people rejoice; But when the wicked rule, the people groan.
3
Apendaye hekima humfurahisha babaye; Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali.
Whoever loves wisdom brings joy to his father; But a companion of prostitutes squanders his wealth.
4
Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.
The king by justice makes the land stable, But he who takes bribes tears it down.
5
Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.
A man who flatters his neighbor, Spreads a net for his feet.
6
Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya; Bali mwenye haki huimba na kufurahi.
An evil man is snared by his sin, But the righteous can sing and be glad.
7
Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini; Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.
The righteous care about justice for the poor. The wicked aren't concerned about knowledge.
8
Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.
Mockers stir up a city, But wise men turn away anger.
9
Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
If a wise man goes to court with a foolish man, The fool rages or scoffs, and there is no peace.
10
Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu; Bali wenye haki humtunza nafsi yake.
The bloodthirsty hate a man of integrity; And they seek the life of the upright.
11
Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.
A fool vents all of his anger, But a wise man brings himself under control.
12
Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.
If a ruler listens to lies, All of his officials are wicked.
13
Maskini na mdhalimu hukutana pamoja; Bwana huwatia nuru macho yao wote wawili.
The poor man and the oppressor have this in common: Yahweh gives sight to the eyes of both.
14
Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu; Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.
The king who fairly judges the poor, His throne shall be established forever.
15
Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
The rod of correction gives wisdom, But a child left to himself causes shame to his mother.
16
Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka; Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.
When the wicked increase, sin increases; But the righteous will see their downfall.
17
Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako.
Correct your son, and he will give you peace; Yes, he will bring delight to your soul.
18
Pasipo maono, watu huacha kujizuia; Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Where there is no revelation, the people cast off restraint; But one who keeps the law is blessed.
19
Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno; Maana ajapoyafahamu hataitika.
A servant can't be corrected by words. Though he understands, yet he will not respond.
20
Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
Do you see a man who is hasty in his words? There is more hope for a fool than for him.
21
Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.
He who pampers his servant from youth Will have him become a son in the end.
22
Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.
An angry man stirs up strife, And a wrathful man abounds in sin.
23
Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.
A man's pride brings him low, But one of lowly spirit gains honor.
24
Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe; Asikia maapizo, wala hana neno.
Whoever is an accomplice of a thief is an enemy of his own soul. He takes an oath, but dares not testify.
25
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama.
The fear of man proves to be a snare, But whoever puts his trust in Yahweh is kept safe.
26
Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu; Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa Bwana
Many seek the ruler's favor, But a man's justice comes from Yahweh.
27
Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki; Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.
A dishonest man detests the righteous, And the upright in their ways detest the wicked.
« 28 30 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)