Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa.
He who is often rebuked and stiffens his neck Will be destroyed suddenly, with no remedy.
Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua.
When the righteous thrive, the people rejoice; But when the wicked rule, the people groan.
Apendaye hekima humfurahisha babaye; Bali ashikamanaye na makahaba hutapanya mali.
Whoever loves wisdom brings joy to his father; But a companion of prostitutes squanders his wealth.
Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.
The king by justice makes the land stable, But he who takes bribes tears it down.
Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake.
A man who flatters his neighbor, Spreads a net for his feet.
Kuna mtego katika kosa la mtu mbaya; Bali mwenye haki huimba na kufurahi.
An evil man is snared by his sin, But the righteous can sing and be glad.
Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini; Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue.
The righteous care about justice for the poor. The wicked aren't concerned about knowledge.
Watu wenye dharau huwasha mji moto; Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu.
Mockers stir up a city, But wise men turn away anger.
Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
If a wise man goes to court with a foolish man, The fool rages or scoffs, and there is no peace.
Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu; Bali wenye haki humtunza nafsi yake.
The bloodthirsty hate a man of integrity; And they seek the life of the upright.
Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.
A fool vents all of his anger, But a wise man brings himself under control.
Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.
If a ruler listens to lies, All of his officials are wicked.
Maskini na mdhalimu hukutana pamoja; Bwana huwatia nuru macho yao wote wawili.
The poor man and the oppressor have this in common: Yahweh gives sight to the eyes of both.
Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu; Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.
The king who fairly judges the poor, His throne shall be established forever.
Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
The rod of correction gives wisdom, But a child left to himself causes shame to his mother.
Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka; Bali wenye haki watayatazama maanguko yao.
When the wicked increase, sin increases; But the righteous will see their downfall.
Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako.
Correct your son, and he will give you peace; Yes, he will bring delight to your soul.
Pasipo maono, watu huacha kujizuia; Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Where there is no revelation, the people cast off restraint; But one who keeps the law is blessed.
Haitoshi mtumwa kuonywa kwa maneno; Maana ajapoyafahamu hataitika.
A servant can't be corrected by words. Though he understands, yet he will not respond.
Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
Do you see a man who is hasty in his words? There is more hope for a fool than for him.
Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.
He who pampers his servant from youth Will have him become a son in the end.
Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.
An angry man stirs up strife, And a wrathful man abounds in sin.
Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa.
A man's pride brings him low, But one of lowly spirit gains honor.
Mshiriki wa mwivi huichukia nafsi yake mwenyewe; Asikia maapizo, wala hana neno.
Whoever is an accomplice of a thief is an enemy of his own soul. He takes an oath, but dares not testify.
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama.
The fear of man proves to be a snare, But whoever puts his trust in Yahweh is kept safe.
Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu; Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa Bwana
Many seek the ruler's favor, But a man's justice comes from Yahweh.
Mtu aliye dhalimu ni chukizo kwa wenye haki; Na mnyofu wa mwenendo ni chukizo kwa waovu.
A dishonest man detests the righteous, And the upright in their ways detest the wicked.