Mithali 24 Swahili & English
Listen/Download AudioMithali 24 (Swahili) | Proverbs 24 (English) |
---|---|
Usiwahusudu watu waovu, Wala usitamani kuwa pamoja nao; Mithali 24:1 |
Don't be envious of evil men; Neither desire to be with them: |
Kwa maana moyo wao hufikiri dhuluma, Na midomo yao huongea madhara. Mithali 24:2 |
For their hearts plot violence, And their lips talk about mischief. |
Nyumba hujengwa kwa hekima, Na kwa ufahamu huthibitika, Mithali 24:3 |
Through wisdom a house is built; By understanding it is established; |
Na kwa maarifa vyumba vyake hujazwa Vitu vyote vya thamani na vya kupendeza. Mithali 24:4 |
By knowledge the rooms are filled With all rare and beautiful treasure. |
Mtu mwenye hekima ana nguvu; Naam, mtu wa maarifa huongeza uwezo; Mithali 24:5 |
A wise man has great power; And a knowledgeable man increases strength; |
Maana kwa mashauri ya akili utafanya vita; Na kwa wingi wa washauri huja wokovu. Mithali 24:6 |
For by wise guidance you wage your war; And victory is in many advisors. |
Kwa mpumbavu hekima haipatikani; Hafumbui kinywa chake langoni. Mithali 24:7 |
Wisdom is too high for a fool: He doesn't open his mouth in the gate. |
Mtu afikiriye kutenda maovu, Watu watamwita mtundu; Mithali 24:8 |
One who plots to do evil Will be called a schemer. |
Fikira za mpumbavu ni dhambi, Na mwenye mzaha huwachukiza watu. Mithali 24:9 |
The schemes of folly are sin. The mocker is detested by men. |
Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache. Mithali 24:10 |
If you falter in the time of trouble, Your strength is small. |
Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe; Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe. Mithali 24:11 |
Rescue those who are being led away to death! Indeed, hold back those who are staggering to the slaughter! |
Ukisema, Sisi hatukujua hayo; Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye? Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye? Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake? Mithali 24:12 |
If you say, "Behold, we didn't know this;" Doesn't he who weighs the hearts consider it? He who keeps your soul, doesn't he know it? Shall he not render to every man according to his work? |
Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema, Na sega la asali lililo tamu ulionjapo. Mithali 24:13 |
My son, eat honey, for it is good; The droppings of the honeycomb, which are sweet to your taste: |
Basi utaijua hekima kuwa tamu kwa nafsi yako; Ikiwa umekwisha kuiona; Ndipo itakapofuata thawabu; Wala tumaini lako halitabatilika. Mithali 24:14 |
So you shall know wisdom to be to your soul; If you have found it, then there will be a reward, Your hope will not be cut off. |
Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki; Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika; Mithali 24:15 |
Don't lay in wait, wicked man, against the habitation of the righteous. Don't destroy his resting-place: |
Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya. Mithali 24:16 |
For a righteous man falls seven times, and rises up again; But the wicked are overthrown by calamity. |
Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo; Mithali 24:17 |
Don't rejoice when your enemy falls. Don't let your heart be glad when he is overthrown; |
Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake. Mithali 24:18 |
Lest Yahweh see it, and it displease him, And he turn away his wrath from him. |
Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya; Wala usiwahusudu wabaya; Mithali 24:19 |
Don't fret yourself because of evildoers; Neither be envious of the wicked: |
Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu; Taa ya mtu mbaya itazimika. Mithali 24:20 |
For there will be no reward to the evil man; And the lamp of the wicked shall be snuffed out. |
Mwanangu, mche Bwana, na mfalme; Wala usishirikiane na wenye kigeugeu; Mithali 24:21 |
My son, fear Yahweh and the king. Don't join those who are rebellious: |
Maana msiba wao utatokea kwa ghafula; Tena ni nani aujuaye uharibifu wa miaka yao. Mithali 24:22 |
For their calamity will rise suddenly; The destruction from them both--who knows? |
Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili. Kupendelea watu katika hukumu si kwema. Mithali 24:23 |
These also are sayings of the wise. To show partiality in judgment is not good. |
Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki; Kabila za watu watamlaani, taifa watamchukia. Mithali 24:24 |
He who says to the wicked, "You are righteous;" Peoples shall curse him, and nations shall abhor him-- |
Bali kwao wakemeao furaha itakuwako; Na baraka ya kufanikiwa itawajilia. Mithali 24:25 |
But it will go well with those who convict the guilty, And a rich blessing will come on them. |
Aibusu midomo atoaye jawabu la haki. Mithali 24:26 |
An honest answer Is like a kiss on the lips. |
Tengeneza kazi yako huko nje, Jifanyizie kazi yako tayari shambani, Ukiisha, jenga nyumba yako. Mithali 24:27 |
Prepare your work outside, And get your fields ready. Afterwards, build your house. |
Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu, Wala usidanganye kwa midomo yako. Mithali 24:28 |
Don't be a witness against your neighbor without cause. Don't deceive with your lips. |
Usiseme, Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; Nitamlipa mtu huyo sawasawa na tendo lake. Mithali 24:29 |
Don't say, "I will do to him as he has done to me; I will render to the man according to his work." |
Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili. Mithali 24:30 |
I went by the field of the sluggard, By the vineyard of the man void of understanding; |
Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka. Mithali 24:31 |
Behold, it was all grown over with thorns. Its surface was covered with nettles, And its stone wall was broken down. |
Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; Naliona, nikapata mafundisho. Mithali 24:32 |
Then I saw, and considered well. I saw, and received instruction: |
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi! Mithali 24:33 |
A little sleep, a little slumber, A little folding of the hands to sleep; |
Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang'anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha. Mithali 24:34 |
So shall your poverty come as a robber, And your want as an armed man. |