Mithali 20

Proverbs Chapter 20

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima.
Wine is a mocker, and beer is a brawler; Whoever is led astray by them is not wise.
2
Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba; Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake.
The terror of a king is like the roaring of a lion: He who provokes him to anger forfeits his own life.
3
Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana.
It is an honor for a man to keep aloof from strife; But every fool will be quarreling.
4
Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu.
The sluggard will not plow by reason of the winter; Therefore he shall beg in harvest, and have nothing.
5
Mashauri ya moyoni ni kama kilindi; Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.
Counsel in the heart of man is like deep water; But a man of understanding will draw it out.
6
Wanadamu hutangaza kila mtu hisani yake mwenyewe; Bali mtu aliye mwaminifu, ni nani awezaye kumpata?
Many men claim to be men of unfailing love, But who can find a faithful man?
7
Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.
A righteous man walks in integrity. Blessed are his children after him.
8
Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu, Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.
A king who sits on the throne of judgment Scatters away all evil with his eyes.
9
Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu; Nimetakasika dhambi yangu?
Who can say, "I have made my heart pure. I am clean and without sin?"
10
Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali, Vyote viwili ni chukizo kwa Bwana.
Differing weights and differing measures, Both of them alike are an abomination to Yahweh.
11
Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.
Even a child makes himself known by his doings, Whether his work is pure, and whether it is right.
12
Sikio lisikialo, na jicho lionalo, Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili.
The hearing ear, and the seeing eye, Yahweh has made even both of them.
13
Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.
Don't love sleep, lest you come to poverty; Open your eyes, and you shall be satisfied with bread.
14
Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi; Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.
"It's no good, it's no good," says the buyer; But when he is gone his way, then he boasts.
15
Dhahabu iko, na marijani tele; Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.
There is gold and abundance of rubies; But the lips of knowledge are a rare jewel.
16
Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni; Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.
Take the garment of one who puts up collateral for a stranger; And hold him in pledge for a wayward woman.
17
Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu; Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.
Fraudulent food is sweet to a man, But afterwards his mouth is filled with gravel.
18
Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita.
Plans are established by advice; By wise guidance you wage war!
19
Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.
He who goes about as a tale-bearer reveals secrets; Therefore don't keep company with him who opens wide his lips.
20
Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu.
Whoever curses his father or his mother, His lamp shall be put out in blackness of darkness.
21
Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka, Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.
An inheritance quickly gained at the beginning, Won't be blessed in the end.
22
Usiseme, Mimi nitalipa mabaya; Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
Don't say, "I will pay back evil." Wait for Yahweh, and he will save you.
23
Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa Bwana; Tena mizani ya hila si njema.
Yahweh detests differing weights, And dishonest scales are not pleasing.
24
Mwenendo wa mtu watoka kwa Bwana; Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake?
A man's steps are from Yahweh; How then can man understand his way?
25
Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu; Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari.
It is a snare to a man to make a rash dedication, Then later to consider his vows.
26
Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki; Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao.
A wise king winnows out the wicked, And drives the threshing wheel over them.
27
Pumzi ya mwanadamu ni taa ya Bwana; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.
The spirit of man is Yahweh's lamp, Searching all his innermost parts.
28
Fadhili na uaminifu humhifadhi mfalme, Na kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa fadhili.
Love and faithfulness keep the king safe. His throne is sustained by love.
29
Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.
The glory of young men is their strength. The splendor of old men is their gray hair.
30
Machubuko ya fimbo husafisha uovu, Na mapigo hufikilia ndani ya mtima.
Wounding blows cleanse away evil, And beatings purge the innermost parts.
« 19 21 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)