Mithali 20 Swahili & English
Listen/Download AudioMithali 20 (Swahili) | Proverbs 20 (English) |
---|---|
Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo hana hekima. Mithali 20:1 |
Wine is a mocker, and beer is a brawler; Whoever is led astray by them is not wise. |
Utisho wa mfalme ni kama ngurumo ya simba; Amkasirishaye huitendea dhambi nafsi yake. Mithali 20:2 |
The terror of a king is like the roaring of a lion: He who provokes him to anger forfeits his own life. |
Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake; Bali kila mpumbavu ataka kugombana. Mithali 20:3 |
It is an honor for a man to keep aloof from strife; But every fool will be quarreling. |
Mtu mvivu hataki kulima wakati wa baridi; Hivyo wakati wa mavuno ataomba, hana kitu. Mithali 20:4 |
The sluggard will not plow by reason of the winter; Therefore he shall beg in harvest, and have nothing. |
Mashauri ya moyoni ni kama kilindi; Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka. Mithali 20:5 |
Counsel in the heart of man is like deep water; But a man of understanding will draw it out. |
Wanadamu hutangaza kila mtu hisani yake mwenyewe; Bali mtu aliye mwaminifu, ni nani awezaye kumpata? Mithali 20:6 |
Many men claim to be men of unfailing love, But who can find a faithful man? |
Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake. Mithali 20:7 |
A righteous man walks in integrity. Blessed are his children after him. |
Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu, Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake. Mithali 20:8 |
A king who sits on the throne of judgment Scatters away all evil with his eyes. |
Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu; Nimetakasika dhambi yangu? Mithali 20:9 |
Who can say, "I have made my heart pure. I am clean and without sin?" |
Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali, Vyote viwili ni chukizo kwa Bwana. Mithali 20:10 |
Differing weights and differing measures, Both of them alike are an abomination to Yahweh. |
Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake; Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili. Mithali 20:11 |
Even a child makes himself known by his doings, Whether his work is pure, and whether it is right. |
Sikio lisikialo, na jicho lionalo, Bwana ndiye aliyeyafanya yote mawili. Mithali 20:12 |
The hearing ear, and the seeing eye, Yahweh has made even both of them. |
Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula. Mithali 20:13 |
Don't love sleep, lest you come to poverty; Open your eyes, and you shall be satisfied with bread. |
Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi; Lakini akiisha kwenda zake hujisifu. Mithali 20:14 |
"It's no good, it's no good," says the buyer; But when he is gone his way, then he boasts. |
Dhahabu iko, na marijani tele; Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani. Mithali 20:15 |
There is gold and abundance of rubies; But the lips of knowledge are a rare jewel. |
Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni; Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni. Mithali 20:16 |
Take the garment of one who puts up collateral for a stranger; And hold him in pledge for a wayward woman. |
Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu; Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe. Mithali 20:17 |
Fraudulent food is sweet to a man, But afterwards his mouth is filled with gravel. |
Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita. Mithali 20:18 |
Plans are established by advice; By wise guidance you wage war! |
Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana. Mithali 20:19 |
He who goes about as a tale-bearer reveals secrets; Therefore don't keep company with him who opens wide his lips. |
Amlaaniye babaye au mamaye, Taa yake itazimika katika giza kuu. Mithali 20:20 |
Whoever curses his father or his mother, His lamp shall be put out in blackness of darkness. |
Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka, Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa. Mithali 20:21 |
An inheritance quickly gained at the beginning, Won't be blessed in the end. |
Usiseme, Mimi nitalipa mabaya; Mngojee Bwana, naye atakuokoa. Mithali 20:22 |
Don't say, "I will pay back evil." Wait for Yahweh, and he will save you. |
Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa Bwana; Tena mizani ya hila si njema. Mithali 20:23 |
Yahweh detests differing weights, And dishonest scales are not pleasing. |
Mwenendo wa mtu watoka kwa Bwana; Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake? Mithali 20:24 |
A man's steps are from Yahweh; How then can man understand his way? |
Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu; Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari. Mithali 20:25 |
It is a snare to a man to make a rash dedication, Then later to consider his vows. |
Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki; Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao. Mithali 20:26 |
A wise king winnows out the wicked, And drives the threshing wheel over them. |
Pumzi ya mwanadamu ni taa ya Bwana; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake. Mithali 20:27 |
The spirit of man is Yahweh's lamp, Searching all his innermost parts. |
Fadhili na uaminifu humhifadhi mfalme, Na kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa fadhili. Mithali 20:28 |
Love and faithfulness keep the king safe. His throne is sustained by love. |
Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi. Mithali 20:29 |
The glory of young men is their strength. The splendor of old men is their gray hair. |
Machubuko ya fimbo husafisha uovu, Na mapigo hufikilia ndani ya mtima. Mithali 20:30 |
Wounding blows cleanse away evil, And beatings purge the innermost parts. |