Mithali 15

Proverbs Chapter 15

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
A gentle answer turns away wrath, But a harsh word stirs up anger.
2
Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri; Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.
The tongue of the wise commends knowledge, But the mouth of fools gush out folly.
3
Macho ya Bwana yako kila mahali; Yakimchunguza mbaya na mwema.
Yahweh's eyes are everywhere, Keeping watch on the evil and the good.
4
Ulimi safi ni mti wa uzima; Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
A gentle tongue is a tree of life, But deceit in it crushes the spirit.
5
Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye; Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.
A fool despises his father's correction, But he who heeds reproof shows prudence.
6
Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
In the house of the righteous is much treasure, But the income of the wicked brings trouble.
7
Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa; Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.
The lips of the wise spread knowledge; Not so with the heart of fools.
8
Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.
The sacrifice made by the wicked is an abomination to Yahweh, But the prayer of the upright is his delight.
9
Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali humpenda mtu afuatiaye wema.
The way of the wicked is an abomination to Yahweh, But he loves him who follows after righteousness.
10
Adhabu kali ina yeye aiachaye njia; Naye achukiaye kukemewa atakufa.
There is stern discipline for one who forsakes the way: Whoever hates reproof shall die.
11
Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za Bwana; Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
Sheol and Abaddon are before Yahweh-- How much more then the hearts of the children of men!
12
Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa; Wala yeye hawaendei wenye hekima.
A scoffer doesn't love to be reproved; He will not go to the wise.
13
Moyo wa furaha huchangamsha uso; Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
A glad heart makes a cheerful face; But an aching heart breaks the spirit.
14
Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa; Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
The heart of one who has understanding seeks knowledge, But the mouths of fools feed on folly.
15
Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya; Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
All the days of the afflicted are wretched, But one who has a cheerful heart enjoys a continual feast.
16
Kuwa na mali chache pamoja na kumcha Bwana; Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
Better is little, with the fear of Yahweh, Than great treasure with trouble.
17
Chakula cha mboga penye mapendano; Ni bora kuliko ng'ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
Better is a dinner of herbs, where love is, Than a fattened calf with hatred.
18
Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
A wrathful man stirs up contention, But one who is slow to anger appeases strife.
19
Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba; Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
The way of the sluggard is like a thorn patch, But the path of the upright is a highway.
20
Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mpumbavu humdharau mamaye.
A wise son makes a father glad, But a foolish man despises his mother.
21
Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili; Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
Folly is joy to one who is void of wisdom, But a man of understanding keeps his way straight.
22
Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
Where there is no counsel, plans fail; But in a multitude of counselors they are established.
23
Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
Joy comes to a man with the reply of his mouth. How good is a word at the right time!
24
Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.
The path of life leads upward for the wise, To keep him from going downward to Sheol.
25
Bwana ataing'oa nyumba ya mwenye kiburi; Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
Yahweh will uproot the house of the proud, But he will keep the widow's borders intact.
26
Mashauri mabaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maneno yapendezayo ni safi.
Yahweh detests the thoughts of the wicked, But the thoughts of the pure are pleasing.
27
Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.
He who is greedy for gain troubles his own house, But he who hates bribes will live.
28
Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu; Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.
The heart of the righteous weighs answers, But the mouth of the wicked gushes out evil.
29
Bwana yu mbali na wasio haki; Bali huisikia sala ya mwenye haki.
Yahweh is far from the wicked, But he hears the prayer of the righteous.
30
Mng'ao wa macho huufurahisha moyo; Habari njema huinenepesha mifupa.
The light of the eyes rejoices the heart. Good news gives health to the bones.
31
Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai Litakaa kati yao wenye hekima.
The ear that listens to reproof lives, And will be at home among the wise.
32
Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe; Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.
He who refuses correction despises his own soul, But he who listens to reproof gets understanding.
33
Kumcha Bwana ni maonyo ya hekima; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
The fear of Yahweh teaches wisdom. Before honor is humility.
« 14 16 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)