Mithali 22 Swahili & English
Listen/Download AudioMithali 22 (Swahili) | Proverbs 22 (English) |
---|---|
Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu. Mithali 22:1 |
A good name is more desirable than great riches, And loving favor is better than silver and gold. |
Tajiri na maskini hukutana pamoja; Bwana ndiye aliyewaumba wote wawili. Mithali 22:2 |
The rich and the poor have this in common: Yahweh is the maker of them all. |
Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha; Bali wajinga huendelea mbele wakaumia. Mithali 22:3 |
A prudent man sees danger, and hides himself; But the simple pass on, and suffer for it. |
Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha Bwana Ni utajiri, na heshima, nayo ni uzima. Mithali 22:4 |
The result of humility and the fear of Yahweh Is wealth, honor, and life. |
Miiba na mitego huwa katika njia ya mshupavu; Yeye aitunzaye nafsi yake atakuwa mbali nayo. Mithali 22:5 |
Thorns and snares are in the path of the wicked: Whoever guards his soul stays from them. |
Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee. Mithali 22:6 |
Train up a child in the way he should go, And when he is old he will not depart from it. |
Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye. Mithali 22:7 |
The rich rule over the poor. The borrower is servant to the lender. |
Yeye apandaye uovu atavuna msiba, Na fimbo ya ghadhabu yake itakoma. Mithali 22:8 |
He who sows wickedness reaps trouble, And the rod of his fury will be destroyed. |
Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa maskini chakula chake. Mithali 22:9 |
He who has a generous eye will be blessed; For he shares his food with the poor. |
Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka; Naam, fitina na fedheha zitakoma. Mithali 22:10 |
Drive out the mocker, and strife will go out; Yes, quarrels and insults will stop. |
Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo; Mfalme atakuwa rafiki yake. Mithali 22:11 |
He who loves purity of heart and speaks gracefully Is the king's friend. |
Macho ya Bwana humhifadhi mwenye maarifa; Bali huyapindua maneno ya mtu haini. Mithali 22:12 |
The eyes of Yahweh watch over knowledge; But he frustrates the words of the unfaithful. |
Mtu mvivu husema, Simba yuko nje; Nitauawa katika njia kuu. Mithali 22:13 |
The sluggard says, "There is a lion outside! I will be killed in the streets!" |
Kinywa cha malaya ni shimo refu; Anayechukiwa na Bwana atatumbukia ndani yake. Mithali 22:14 |
The mouth of an adulteress is a deep pit: He who is under Yahweh's wrath will fall into it. |
Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali. Mithali 22:15 |
Folly is bound up in the heart of a child: The rod of discipline drives it far from him. |
Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato, Naye ampaye tajiri, hupata hasara. Mithali 22:16 |
Whoever oppresses the poor for his own increase and whoever gives to the rich, Both come to poverty. |
Tega sikio lako uyasikie maneno ya wenye hekima, na kuuelekeza moyo wako kwa maarifa yangu; Mithali 22:17 |
Turn your ear, and listen to the words of the wise. Apply your heart to my teaching. |
maana ni vizuri kuyahifadhi ndani yako, hali yakithibitika pamoja midomoni mwako. Mithali 22:18 |
For it is a pleasant thing if you keep them within you, If all of them are ready on your lips. |
Ili matumaini yako uyaweke kwa Bwana, leo nimekujulisha wewe haya, naam, wewe. Mithali 22:19 |
That your trust may be in Yahweh, I teach you today, even you. |
Je! Sikukuandikia mambo makuu juu ya mashauri na juu ya maarifa; Mithali 22:20 |
Haven't I written to you thirty excellent things Of counsel and knowledge, |
ili kukujulisha hakika ya maneno ya kweli, uwarudishie wakutumao maneno ya kweli? Mithali 22:21 |
To teach you truth, reliable words, To give sound answers to the ones who sent you? |
Usimnyang'anye maskini, kwa kuwa ni maskini; Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni; Mithali 22:22 |
Don't exploit the poor, because he is poor; And don't crush the needy in court; |
Kwa sababu Bwana atawatetea; Naye atawateka uhai wao waliowateka. Mithali 22:23 |
For Yahweh will plead their case, And plunder the life of those who plunder them. |
Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi; Mithali 22:24 |
Don't befriend a hot-tempered man, And don't associate with one who harbors anger: |
Usije ukajifunza njia zake; Na kujipatia nafsi yako mtego. Mithali 22:25 |
Lest you learn his ways, And ensnare your soul. |
Usiwe mmoja wao wawekao rehani; Au walio wadhamini kwa deni za watu; Mithali 22:26 |
Don't you be one of those who strike hands, Of those who are collateral for debts. |
Kama huna kitu cha kulipa; Kwani ukaondolee kitanda chako chini yako? Mithali 22:27 |
If you don't have means to pay, Why should he take away your bed from under you? |
Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani, Uliowekwa na baba zako. Mithali 22:28 |
Don't move the ancient boundary stone, Which your fathers have set up. |
Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake? Huyo atasimama mbele ya wafalme; Hatasimama mbele ya watu wasio na cheo. Mithali 22:29 |
Do you see a man skilled in his work? He will serve kings; He won't serve obscure men. |