Mambo ya Walawi 3 Swahili & English
Listen/Download AudioMambo ya Walawi 3 (Swahili) | Leviticus 3 (English) |
---|---|
Na matoleo yake kwamba ni sadaka za amani; kwamba asongeza katika ng'ombe, mume au mke, atamtoa huyo aliye mkamilifu mbele ya Bwana. Mambo ya Walawi 3:1 |
"'If his offering is a sacrifice of peace offerings; if he offers it from the herd, whether male or female, he shall offer it without blemish before Yahweh. |
Naye ataweka mkono wake kichwani mwake huyo aliyemtoa, na kumchinja mlangoni pa hema ya kukutania; na wana wa Haruni, hao makuhani, watainyunyiza damu yake katika madhabahu pande zote. Mambo ya Walawi 3:2 |
He shall lay his hand on the head of his offering, and kill it at the door of the tent of meeting: and Aaron's sons the priests shall sprinkle the blood on the altar round about. |
Naye atasongeza katika sadaka hiyo ya amani, dhabihu kwa Bwana itakayofanywa kwa njia ya moto; yaani, mafuta yafunikayo matumbo, na mafuta yote yaliyo juu ya matumbo, Mambo ya Walawi 3:3 |
He shall offer of the sacrifice of peace offerings an offering made by fire to Yahweh; the fat that covers the innards, and all the fat that is on the innards, |
na figo zake mbili, na mafuta yaliyoshikamana nazo, yaliyo karibu na kiuno, na hicho kitambi kilicho katika ini, pamoja na hizo figo; hayo yote atayaondoa. Mambo ya Walawi 3:4 |
and the two kidneys, and the fat that is on them, which is by the loins, and the cover on the liver, with the kidneys, he shall take away. |
Na wana wa Haruni watayateketeza kwa moto juu ya madhabahu, juu ya sadaka ya kuteketezwa, iliyo katika kuni zilizo juu ya moto; ni dhabihu ya kusongezwa kwa njia ya moto, harufu ya kupendeza kwa Bwana. Mambo ya Walawi 3:5 |
Aaron's sons shall burn it on the altar on the burnt offering, which is on the wood that is on the fire: it is an offering made by fire, of a sweet savor to Yahweh. |
Na matoleo yake kwa sadaka za amani atakayomchinjia Bwana, kwamba ni katika kundi la kondoo; mume au mke, atamtoa huyo aliye mkamilifu. Mambo ya Walawi 3:6 |
"'If his offering for a sacrifice of peace offerings to Yahweh is from the flock; male or female, he shall offer it without blemish. |
Kama akimtoa mwana-kondoo kuwa matoleo yake, ndipo atakapomtolea Bwana; Mambo ya Walawi 3:7 |
If he offers a lamb for his offering, then he shall offer it before Yahweh; |
naye ataweka mkono wake kichwani mwake huyo aliyemsongeza, na kumchinja mlangoni pa hema ya kukutania; na wana wa Haruni watainyunyiza damu yake katika madhabahu pande zote. Mambo ya Walawi 3:8 |
and he shall lay his hand on the head of his offering, and kill it before the tent of meeting: and Aaron's sons shall sprinkle its blood on the altar round about. |
Naye atasongeza katika sadaka hiyo ya amani dhabihu kwa Bwana, itakayofanywa kwa njia ya moto; yaani, mafuta yake, na mkia wenye mafuta mzima, atauondoa kwa kuukata hapo karibu na mfupa wa maungoni; na mafuta yafunikayo matumbo, na mafuta yote yaliyo katika matumbo, Mambo ya Walawi 3:9 |
He shall offer from the sacrifice of peace offerings an offering made by fire to Yahweh; its fat, the entire tail fat, he shall take away close to the backbone; and the fat that covers the inwards, and all the fat that is on the inwards, |
na figo zake mbili, na mafuta yaliyoshikamana nazo, yaliyo karibu na kiuno chake, na kitambi kilicho katika ini, pamoja na hizo figo; hayo yote atayaondoa. Mambo ya Walawi 3:10 |
and the two kidneys, and the fat that is on them, which is by the loins, and the cover on the liver, with the kidneys, he shall take away. |
Naye kuhani atayateketeza kwa moto juu ya madhabahu; ni chakula cha dhabihu ya kusongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto. Mambo ya Walawi 3:11 |
The priest shall burn it on the altar: it is the food of the offering made by fire to Yahweh. |
Na matoleo yake, kwamba ni mbuzi, ndipo atakapomtoa mbele za Bwana; Mambo ya Walawi 3:12 |
"'If his offering is a goat, then he shall offer it before Yahweh: |
naye ataweka mkono wake kichwani mwake, na kumchinja hapo mbele ya hema ya kukutania; na wana wa Haruni watainyunyiza damu yake katika madhabahu pande zote. Mambo ya Walawi 3:13 |
and he shall lay his hand on its head, and kill it before the tent of meeting; and the sons of Aaron shall sprinkle its blood on the altar round about. |
Naye atasongeza katika sadaka hiyo matoleo yake, dhabihu kwa Bwana kwa njia ya moto; yaani, mafuta yafunikayo matumbo, na mafuta yote yaliyo katika matumbo, Mambo ya Walawi 3:14 |
He shall offer from it as his offering, an offering made by fire to Yahweh; the fat that covers the innards, and all the fat that is on the innards, |
na figo zake mbili, na mafuta yaliyoshikamana nazo, yaliyo karibu na kiuno chake, na kitambi kilicho katika ini pamoja na hizo figo mbili; hayo yote atayaondoa. Mambo ya Walawi 3:15 |
and the two kidneys, and the fat that is on them, which is by the loins, and the cover on the liver, with the kidneys, he shall take away. |
Naye kuhani atayateketeza kwa moto juu ya madhabahu; ni chakula cha dhabihu ya kusongezwa kwa njia ya moto, iwe harufu ya kupendeza; mafuta yote ni ya Bwana. Mambo ya Walawi 3:16 |
The priest shall burn them on the altar: it is the food of the offering made by fire, for a sweet savor; all the fat is Yahweh's. |
Neno hili litakuwa amri ya daima, katika vizazi vyenu vyote, ndani ya nyumba zenu zote, ya kwamba hamtakula mafuta wala damu kabisa. Mambo ya Walawi 3:17 |
"'It shall be a perpetual statute throughout your generations in all your dwellings, that you shall eat neither fat nor blood.'" |