Zabron Singers - Nimerudishiwa Lyrics
Lyrics
Yupo mungu wa upendo Pamoja twamuita Baba Mwenye familia na upendo Asiye na mwanzo wala mwisho Mungu mwenye haki Muumba wa mbingu Huwapa haki watu wote Tumaini la mwisho kwa watu Watu wa dunia hii
Tangu mi nikujue sio Yule Umerudisha mengi kwangu, ndio Bwana ninakusifu Naimba halleluya Utukuzwa milele yote
Nimerudishiwa na bwana Thamani ya uzima yangu Siwezi hesabu Siwezi kuhesabu Matendo na wema ya mungu Nimerudishiwa na Yesu Zaidi ya jana na juzi Sasa ninakiri Ninashuhudia kuna mungu Mungu wa watu
Utumwa wa yusufu Bwana uliondoa Kamvika na heshima, kapanda kapanda Kawa mheshimiwa Bwana uliondoa shida za yusufu tukuzwe
Nilipolemewa na mizigo Moyo ukajawa na simanzi, hee Ukanirudishia furaha yangu Ukanijaza Baraka na uzima
Nimerudishiwa na bwana Thamani ya uzima yangu Siwezi hesabu Siwezi kuhesabu Matendo na wema ya mungu Nimerudishiwa na Yesu Zaidi ya jana na juzi Sasa ninakiri Ninashuhudia kuna mungu Mungu wa watu
Najua najua kwamba wewe Ni mungu uliye mwaminifu Kwamba, mambo yote warudisha Nilivyopoteza Bado mi huomba huomba Sijawahi kuchoka Nakuamini pekee, pekee Yesu Wanipenda ndio maana Warudisha vingi vilivyo vyangu
Nimerudishiwa na bwana Thamani ya uzima yangu Siwezi hesabu Siwezi kuhesabu Matendo na wema ya mungu Nimerudishiwa na Yesu Zaidi ya jana na juzi Sasa ninakiri Ninashuhudia kuna mungu Mungu wa watu
Video
Nimerudishiwa by Zabron Singers