Zabron Singers - Sweetie Sweetie Lyrics

Sweetie Sweetie Lyrics

Hatimaye ni leo ni siku yetu 
Siku yetu muhimu harusi yetu 
Kuwepo kwenyu kwetu muhimu 
Kwetu nyinyi ni ndugu leo na kesho 

Harusi maua ng'ari ng'ari wanapendeza 
Leo ni furaha shangwe na furaha 
Harusi maua tabasamu, suti na shela 
Wacha tufurahi sote tufurahi 

Sweetie sweetie sweetie 
Haikuwa rahisi tufike leo hii 
Na hapa tulipo ndio siku yetu 
Ipo ukivu ya harusi 

Sasa nyumba moja mwili mmoja 
Kila kitu ni moja tuwe pamoja 
Upendo naongeza nawe ongeza 
Heshima napandisha tuwe pamoja 

Sweetie sweetie sweetie 
Haikuwa rahisi tufike leo hii 
Na hapa tulipo ndio siku yetu 
Ipo ukivu ya harusi 

Sasa wewe ni mimi, mimi ni wewe 
Wewe ndio wendani wangu rafiki yangu 

Na wazazi wameona wakaturusu 
Kwa furaha wakasema tumewabariki 
Na mwenyezi maulana atatubariki 
Tukazae na tulee watoto wazuri 

Sweetie sweetie sweetie 
Haikuwa rahisi tufike leo hii 
Na hapa tulipo ndio siku yetu 
Ipo ukivu ya harusi 

Sasa nyumba moja mwili mmoja 
Kila kitu ni moja tuwe pamoja 
Upendo naongeza nawe ongeza 
Heshima napandisha tuwe pamoja 

Sweetie sweetie sweetie 
Haikuwa rahisi tufike leo hii (my love)
Na hapa tulipo ndio siku yetu 
Ipo ukivu ya harusi 

Ya ndoa mengi mengi tupande nayo 
Sweetie nikuheshimu uniheshimu 
Mahaba moto moto yawe ni wimbo 
KWetu yakawe waridi yakanukie 

Walikuweko nao walitamani 
Wakaparangana haikuwezekana 
Nasi Mungu tusingefika hapa na kufurahi hivi 
Leo ni leo mambo sasa ni mambo

Sweetie sweetie sweetie 
Haikuwa rahisi tufike leo hii (my baby)
Na hapa tulipo ndio siku yetu 
Ipo ukivu ya harusi 

Sasa nyumba moja mwili mmoja 
Kila kitu ni moja tuwe pamoja 
Upendo naongeza nawe ongeza 
Heshima napandisha tuwe pamoja 

Na tutakumbushana kukaa na Mungu 
Familia ya Mungu hujaa upendo 
Wema kwa ndugu zote wa pande zote 
Tutapendwa na wote hata na Mungu 


Sweetie Sweetie Video

Sweetie Sweetie Lyrics -  Zabron Singers

Zabron Singers Songs

Related Songs