Neema Gospel Choir - UNIREHEMU Lyrics

Album: The Sound of Ahsante
Released: 11 Oct 2021
iTunes Amazon Music

Lyrics

Unirehemu Mungu unirehemu,

Mimi Bwana MUNGU wangu naja,

Maana nafsi yangu imekukimbilia wewe Bwana,


Nafsi yangu ikatikati ya Simba

Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale. .

Na ndimi zao ni upanga mkali peke yangu mimi siwezi.

wameweka wavu iii kuninasa. .

Nafsi yangu imeinama

Wamechimba shimo mbele yangu, wametumbukia ndani yake.

(Bwana uniumbie moyo safi

iii ni-kutumikie )


Bwana uniumbie moyo safi

Ili ni-kutumikie


Nimekukimbilia wewe Bwana wangu,


Ili nisiahibike milele, kwa haki yako uniponye uniokoe.

Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu,

Uwe kwangu baba yangu, niumbie moyo safi

Nakuhitaji 


Bwana Yesu maishani mwangu.


Niumbie moyo safi, Ili nitembee katika kweli yako


Hii ndo haja ya moyo wangu Bwana unisikie,

Niumbie moyo safi, niko mbele zako Bwana ninakuomba

Bwana uniumbie Moyo safi

Bwana uniumbie moyo safi,

Ili nikutumikie

Walinizunguka, naam walinizunguka, watesi wangu.

Lakini kwa jina la Yesu, naliwakatilia mbali.

Yesu wewe unaweza

Yesu wewe unatosha,

Watumishi wako wote.

Utawalinda na kuwatunza.


Video

UNIREHEMU - Neema Gospel Choir (Official Audio) The Sound of Ahsante

Thumbnail for UNIREHEMU video
Loading...
In Queue
View Lyrics