Mambo ya Walawi 10 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mambo ya Walawi 10 (Swahili) Leviticus 10 (English)

Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mtu chetezo chake, wakatia moto ndani yake, wakatia na uvumba, nao wakatoa moto wa kigeni mbele ya Bwana, ambao yeye hakuwaagiza. Mambo ya Walawi 10:1

Nadab and Abihu, the sons of Aaron, each took his censer, and put fire in it, and laid incense on it, and offered strange fire before Yahweh, which he had not commanded them.

Kisha moto ukatoka hapo mbele za Bwana, nao ukawala, nao wakafa mbele za Bwana. Mambo ya Walawi 10:2

And fire came forth from before Yahweh, and devoured them, and they died before Yahweh.

Ndipo Musa akamwambia Haruni, Jambo hili ni hilo Bwana alilolinena, akisema, Nitatakaswa mimi katika hao wanikaribiao, nami nitatukuzwa mbele ya watu hao wote. Haruni akanyamaza kimya. Mambo ya Walawi 10:3

Then Moses said to Aaron, "This is what Yahweh spoke of, saying, "'I will show myself holy to those who come near me, And before all the people I will be glorified.'" Aaron held his peace.

Musa akawaita Mishaeli na Elisafani, wana wa Uzieli mjombaye Haruni, na kuwaambia, Njoni karibu, mwachukue hawa ndugu zenu, mkawaondoe hapa mbele ya maskani, mwende nao nje ya marago. Mambo ya Walawi 10:4

Moses called Mishael and Elzaphan, the sons of Uzziel the uncle of Aaron, and said to them, "Draw near, carry your brothers from before the sanctuary out of the camp."

Basi wakaja karibu, na kuwachukua, hali wamevaa nguo zao, wakawachukua nje ya marago; kama Musa alivyosema. Mambo ya Walawi 10:5

So they drew near, and carried them in their coats out of the camp, as Moses had said.

Kisha Musa akamwambia Haruni na wanawe Eleazari na Ithamari, Msiache wazi nywele za vichwani mwenu, wala msiyararue mavao yenu; ili kwamba msife, tena asiukasirikie mkutano wote; lakini ndugu zenu, nyumba yote ya Israeli, na waomboleze kwa ajili ya hicho kichomo alichowasha Bwana. Mambo ya Walawi 10:6

Moses said to Aaron, and to Eleazar and to Ithamar, his sons, "Don't let the hair of your heads go loose, neither tear your clothes; that you don't die, and that he not be angry with all the congregation: but let your brothers, the whole house of Israel, bewail the burning which Yahweh has kindled.

Wala hamtatoka nje mlangoni mwa hema ya kukutania, msije mkafa; kwa sababu mafuta ya kutiwa ya Bwana ya juu yenu. Nao wakafanya kama hilo neno la Musa. Mambo ya Walawi 10:7

You shall not go out from the door of the Tent of Meeting, lest you die; for the anointing oil of Yahweh is on you." They did according to the word of Moses.

Kisha Bwana akanena na Haruni, na kumwambia, Mambo ya Walawi 10:8

Yahweh spoke to Aaron, saying,

Usinywe divai wala kileo cho chote, wewe, wala wanao pamoja nawe, hapo mwingiapo ndani ya hema ya kukutania, ili kwamba msife; amri hii itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyenu; Mambo ya Walawi 10:9

"Drink no wine nor strong drink, you, nor your sons with you, when you go into the Tent of Meeting, that you don't die: it shall be a statute forever throughout your generations:

kisha, mpate kupambanua kati ya yaliyo matakatifu na hayo yaliyo ya siku zote, na kati ya yaliyo najisi na hayo yaliyo safi; Mambo ya Walawi 10:10

and that you are to make a distinction between the holy and the common, and between the unclean and the clean;

tena mpate kuwafundisha wana wa Israeli amri hizi zote ambazo Bwana amewaambia kwa mkono wa Musa. Mambo ya Walawi 10:11

and that you are to teach the children of Israel all the statutes which Yahweh has spoken to them by Moses."

Kisha Musa akanena na Haruni, na Eleazari, na Ithamari, hao wanawe waliobaki, Twaeni hiyo sadaka ya unga iliyosalia katika kafara za Bwana zilizotolewa kwa moto, mkaile pasipo kutiwa chachu, pale karibu na madhabahu; kwa kuwa ni takatifu sana; Mambo ya Walawi 10:12

Moses spoke to Aaron, and to Eleazar and to Ithamar, his sons who were left, "Take the meal offering that remains of the offerings of Yahweh made by fire, and eat it without yeast beside the altar; for it is most holy;

nanyi mtaila katika mahali patakatifu, kwa sababu ni haki yako, na haki ya wanao, katika hizo kafara zisongezwazo kwa Bwana kwa moto; kwani ni hivyo nilivyoagizwa. Mambo ya Walawi 10:13

and you shall eat it in a holy place, because it is your portion, and your sons' portion, of the offerings of Yahweh made by fire: for so I am commanded.

Na kidari cha kutikiswa, na mguu wa kuinuliwa, mtavila katika mahali palipo safi; wewe, na wanao, na binti zako pamoja nawe; kwa maana vimetolewa kuwa ni haki yako, na haki ya wanao, katika zile kafara za sadaka za amani za wana wa Israeli. Mambo ya Walawi 10:14

The waved breast and the heaved thigh you shall eat in a clean place, you, and your sons, and your daughters with you: for they are given as your portion, and your sons' portion, out of the sacrifices of the peace offerings of the children of Israel.

Mguu wa kuinuliwa, na kidari cha kutikiswa, Watavileta pamoja na dhabihu zisongezwazo kwa njia ya moto, za hayo mafuta ili kuvitikisa viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana; kisha vitakuwa ni vyako wewe, na vya wanao pamoja nawe, ni haki yenu milele, kama Bwana alivyoagiza. Mambo ya Walawi 10:15

The heaved thigh and the waved breast they shall bring with the offerings made by fire of the fat, to wave it for a wave offering before Yahweh: and it shall be yours, and your sons' with you, as a portion forever; as Yahweh has commanded."

Kisha Musa akamtafuta sana huyo mbuzi wa sadaka ya dhambi, naye, tazama, alikuwa amekwisha kuchomwa moto; naye akawakasirikia hao Eleazari na Ithamari, wana wa Haruni, hao waliobaki, akawaambia, Mambo ya Walawi 10:16

Moses diligently inquired about the goat of the sin offering, and, behold, it was burned: and he was angry with Eleazar and with Ithamar, the sons of Aaron who were left, saying,

Kwa nini hamkula hiyo sadaka ya dhambi katika mahali patakatifu, kwa kuwa ni takatifu sana, naye amewapa ninyi ili kuuchukua uovu wa mkutano, na kuwafanyia upatanisho mbele za Bwana? Mambo ya Walawi 10:17

"Why haven't you eaten the sin offering in the place of the sanctuary, seeing it is most holy, and he has given it you to bear the iniquity of the congregation, to make atonement for them before Yahweh?

Angalieni, hiyo damu yake haikuletwa ndani ya mahali patakatifu; iliwapasa kuila ndani ya mahali patakatifu, kama nilivyowaagiza. Mambo ya Walawi 10:18

Behold, its blood was not brought into the inner part of the sanctuary: you certainly should have eaten it in the sanctuary, as I commanded."

Haruni akamwambia Musa, Angalia, hivi leo wamesongeza sadaka yao ya dhambi, na sadaka yao ya kuteketezwa, mbele za Bwana; kisha mambo kama haya yamenipata; tena kama ningalikula hiyo sadaka ya dhambi hivi leo, je! Lingekuwa ni jambo la kupendeza mbele za macho ya Bwana? Mambo ya Walawi 10:19

Aaron spoke to Moses, "Behold, this day they have offered their sin offering and their burnt offering before Yahweh; and such things as these have happend to me: and if I had eaten the sin offering today, would it have been pleasing in the sight of Yahweh?"

Naye Musa aliposikia hayo, yakampendeza. Mambo ya Walawi 10:20

When Moses heard that, it was pleasing in his sight.