Mambo ya Walawi 22 Swahili & English

Listen/Download Audio
Mambo ya Walawi 22 (Swahili) Leviticus 22 (English)

Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Mambo ya Walawi 22:1

Yahweh spoke to Moses, saying,

Nena na Haruni na wanawe, ili wajitenge wenyewe na vitu vitakatifu vya wana wa Israeli ambavyo wanitakasia mimi, tena kwamba wasilinajisi jina langu takatifu; mimi ndimi Bwana. Mambo ya Walawi 22:2

"Tell Aaron and his sons to separate themselves from the holy things of the children of Israel, which they make holy to me, and that they not profane my holy name. I am Yahweh.

Waambie, Mtu ye yote wa kizazi chenu chote katika vizazi vyenu, atakayevikaribia vile vitu vitakatifu, ambavyo wana wa Israeli wamtakasia Bwana, naye ana unajisi, mtu huyo atakatiliwa mbali asiwe mbele zangu; mimi ndimi Bwana. Mambo ya Walawi 22:3

Tell them, 'If anyone of all your seed throughout your generations approaches the holy things, which the children of Israel make holy to Yahweh, having his uncleanness on him, that soul shall be cut off from before me. I am Yahweh.

Mtu ye yote wa kizazi cha Haruni aliye mwenye ukoma, au mwenye kisonono; yeye asile katika vitu vitakatifu, hata atakapokuwa safi. Tena mtu awaye yote atakayekinusa kitu kilicho na unajisi kwa sababu ya wafu, au mtu ambaye shahawa humtoka; Mambo ya Walawi 22:4

"'Whoever of the seed of Aaron is a leper or has an issue; he shall not eat of the holy things, until he is clean. Whoever touches anything that is unclean by the dead, or a man whose seed goes from him;

au mtu amgusaye mnyama atambaaye, wa kumpatia unajisi, au kwamba amgusa mtu wa kumpatia unajisi, kwa unajisi wo wote alio nao; Mambo ya Walawi 22:5

or whoever touches any creeping thing, whereby he may be made unclean, or a man of whom he may take uncleanness, whatever uncleanness he has;

huyo mtu atakayegusa kitu cho chote namna hiyo atakuwa najisi hata jioni, naye hatakula katika vitu vitakatifu, asipooga mwili wake majini. Mambo ya Walawi 22:6

the person that touches any such shall be unclean until the evening, and shall not eat of the holy things, unless he bathe his body in water.

Jua likiisha kuchwa atakuwa safi; kisha baadaye atakula katika vitu vitakatifu, maana ni chakula chake. Mambo ya Walawi 22:7

When the sun is down, he shall be clean; and afterward he shall eat of the holy things, because it is his bread.

Nyamafu au mnyama aliyeraruliwa na wanyama asile, asijitie unajisi kwa hiyo nyama; mimi ndimi Bwana. Mambo ya Walawi 22:8

That which dies of itself, or is torn by animals, he shall not eat, defiling himself by it. I am Yahweh.

Basi kwa hiyo watayashika mausia yangu, wasije wakachukua dhambi kwa hayo, nao wakafa humo, wakiyanajisi; mimi ndimi Bwana niwatakasaye. Mambo ya Walawi 22:9

"'They shall therefore keep my charge, lest they bear sin for it, and die therein, if they profane it. I am Yahweh who sanctifies them.

Mgeni awaye yote asile katika kitu kitakatifu; mgeni wa kuhani akaaye kwake, au mtumishi aliyeajiriwa, asile katika kitu kitakatifu. Mambo ya Walawi 22:10

"'No stranger shall eat of the holy thing: a foreigner living with the priests, or a hired servant, shall not eat of the holy thing.

Lakini kwamba kuhani akinunua mtu ye yote, kwa kumnunua kwa fedha zake, yeye atakula katika hicho; na hao waliozaliwa nyumbani mwake watakula katika chakula chake. Mambo ya Walawi 22:11

But if a priest buys a slave, purchased by his money, he shall eat of it; and such as are born in his house, they shall eat of his bread.

Na binti ya kuhani kwamba ameolewa na mgeni, asile katika sadaka ya kuinuliwa katika vitu vile vitakatifu. Mambo ya Walawi 22:12

If a priest's daughter is married to an outsider, she shall not eat of the heave offering of the holy things.

Lakini kwamba binti ya kuhani ni mjane, au kwamba ameachwa na mumewe, wala hana mtoto, kisha amerudi na kuketi katika nyumba ya baba yake, kama vile katika ujana wake, yeye atakula katika chakula cha baba yake; lakini mgeni awaye yote asile katika chakula hicho. Mambo ya Walawi 22:13

But if a priest's daughter is a widow, or divorced, and has no child, and has returned to her father's house, as in her youth, she may eat of her father's bread: but no stranger shall eat any of it.

Tena kama mtu ye yote akila katika kitu kilicho kitakatifu pasipo kukijua, ndipo ataongeza sehemu ya tano juu ya kitu hicho, na kumpa kuhani kitu hicho kitakatifu. Mambo ya Walawi 22:14

"'If a man eats something holy unwittingly, then he shall add the fifth part of its value to it, and shall give the holy thing to the priest.

Wala wasivinajisi vitu vitakatifu vya wana wa Israeli, wavisongezavyo kwa Bwana; Mambo ya Walawi 22:15

The priests shall not profane the holy things of the children of Israel, which they offer to Yahweh,

hata wakawatwika ule uovu uletao hatia, hapo walapo vitu vyao vitakatifu; kwa kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye. Mambo ya Walawi 22:16

and so cause them to bear the iniquity that brings guilt, when they eat their holy things: for I am Yahweh who sanctifies them.'"

Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Mambo ya Walawi 22:17

Yahweh spoke to Moses, saying,

Nena na Haruni na wanawe, na wana wa israeli wote, uwaambie, Mtu ye yote wa nyumba ya Israeli, au wa wageni walio katika Israeli, atakayetoa matoleo yake, kama ni nadhiri zao mojawapo, au kama ni sadaka yo yote ya hiari, watakayomtolea Bwana kuwa sadaka ya kuteketezwa; Mambo ya Walawi 22:18

"Speak to Aaron, and to his sons, and to all the children of Israel, and say to them, 'Whoever is of the house of Israel, or of the foreigners in Israel, who offers his offering, whether it be any of their vows, or any of their freewill offerings, which they offer to Yahweh for a burnt offering;

ili mpate kukubaliwa, mtaleta mume mkamilifu, katika ng'ombe, au katika kondoo, au katika mbuzi. Mambo ya Walawi 22:19

that you may be accepted, you shall offer a male without blemish, of the bulls, of the sheep, or of the goats.

Lakini mnyama ye yote aliye na kilema msimtoe; kwa kuwa hatakubaliwa kwa ajili yenu. Mambo ya Walawi 22:20

But whatever has a blemish, that you shall not offer: for it shall not be acceptable for you.

Na mtu awaye yote atakayemtolea Bwana dhabihu katika sadaka za amani, ili kuondoa nadhiri, au sadaka ya moyo wa kupenda, katika ng'ombe, au katika kondoo, atakuwa mkamilifu, apate kukubaliwa; pasiwe na kilema ndani yake cho chote. Mambo ya Walawi 22:21

Whoever offers a sacrifice of peace offerings to Yahweh to accomplish a vow, or for a freewill offering, of the herd or of the flock, it shall be perfect to be accepted; there shall be no blemish therein.

Kipofu, au aliyevunjika mahali, au kiwete au aliye na vidonda, au aliye na upele, au aliye na kikoko, hamtamtolea Bwana wanyama hao, wala msiwasongeze kwa Bwana kwa njia ya moto juu ya madhabahu. Mambo ya Walawi 22:22

Blind, injured, maimed, having a wart, festering, or having a running sore, you shall not offer these to Yahweh, nor make an offering by fire of them on the altar to Yahweh.

Ng'ombe, au mwana-kondoo aliye na kitu kilichozidi, au aliyepungukiwa na kitu katika vitu vya mwilini mwake, mna ruhusa kutoa kuwa sadaka ya moyo wa kupenda; lakini kwa ajili ya nadhiri hatakubaliwa. Mambo ya Walawi 22:23

Either a bull or a lamb that has any deformity or lacking in his parts, that you may offer for a freewill offering; but for a vow it shall not be accepted.

Mnyama aliyeumia mapumbu yake, au kusetwa, au kuvunjwa, au kukatwa, msimtolee Bwana; wala msifanye hivi katika nchi yenu. Mambo ya Walawi 22:24

That which has its testicles bruised, crushed, broken, or cut, you shall not offer to Yahweh; neither shall you do thus in your land.

Wala msisongeze chakula cha Mungu wenu katika wanyama hao mmojawapo kitokacho mkononi mwa mgeni; kwa sababu uharibifu wao u ndani yao, wana kilema ndani yao; hawatakubaliwa kwa ajili yenu. Mambo ya Walawi 22:25

Neither from the hand of a foreigner shall you offer the bread of your God of any of these; because their corruption is in them. There is a blemish in them. They shall not be accepted for you.'"

Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Mambo ya Walawi 22:26

Yahweh spoke to Moses, saying,

Hapo ng'ombe, au kondoo, au mbuzi, akizaliwa, atakuwa pamoja na mamaye muda wa siku saba; na siku ya nane na baadaye atakubaliwa kuwa ni sadaka ya kutolewa kwa Bwana kwa njia ya moto. Mambo ya Walawi 22:27

"When a bull, or a sheep, or a goat, is born, then it shall remain seven days with its mother; and from the eighth day and thenceforth it shall be accepted for the offering of an offering made by fire to Yahweh.

Tena kama ni ng'ombe, au kama ni kondoo, msimchinje huyo na mwanawe wote wawili kwa siku moja. Mambo ya Walawi 22:28

Whether it is a cow or ewe, you shall not kill it and its young both in one day.

Tena mtakapomchinjia Bwana dhabihu ya shukrani, mtamchinja ili mpate kukubaliwa. Mambo ya Walawi 22:29

"When you sacrifice a sacrifice of thanksgiving to Yahweh, you shall sacrifice it so that you may be accepted.

Italiwa siku iyo hiyo; msisaze kitu chake hata asubuhi; mimi ndimi Bwana. Mambo ya Walawi 22:30

It shall be eaten on the same day; you shall leave none of it until the morning. I am Yahweh.

Kwa hiyo mtayashika maagizo yangu, na kuyafanya; mimi ndimi Bwana. Mambo ya Walawi 22:31

"Therefore you shall keep my commandments, and do them. I am Yahweh.

Wala msilinajisi jina langu takatifu; lakini nitatakaswa mimi katika wana wa Israeli; mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi, Mambo ya Walawi 22:32

You shall not profane my holy name, but I will be made holy among the children of Israel. I am Yahweh who makes you holy,

niliyewaleta mtoke nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu; mimi ndimi Bwana. Mambo ya Walawi 22:33

who brought you out of the land of Egypt, to be your God. I am Yahweh."