Mambo ya Walawi 24 Swahili & English
Listen/Download AudioMambo ya Walawi 24 (Swahili) | Leviticus 24 (English) |
---|---|
Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Mambo ya Walawi 24:1 |
Yahweh spoke to Moses, saying, |
Waagize wana wa Israeli kwamba wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya ile nuru, ili hiyo taa iwake daima. Mambo ya Walawi 24:2 |
"Command the children of Israel, that they bring to you pure olive oil beaten for the light, to cause a lamp to burn continually. |
Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza tangu jioni hata asubuhi mbele za Bwana daima; ni amri ya milele katika vizazi vyenu. Mambo ya Walawi 24:3 |
Outside of the veil of the Testimony, in the Tent of Meeting, shall Aaron keep it in order from evening to morning before Yahweh continually: it shall be a statute forever throughout your generations. |
Atazitengeza hizo taa katika kile kinara kilicho safi mbele za Bwana daima. Mambo ya Walawi 24:4 |
He shall keep in order the lamps on the pure gold lampstand before Yahweh continually. |
Nawe utatwaa unga mwembamba, na kuoka mikate kumi na miwili ya huo unga; sehemu za kumi mbili za efa, zitakuwa katika mkate mmoja. Mambo ya Walawi 24:5 |
"You shall take fine flour, and bake twelve cakes of it: two tenth parts of an ephah shall be in one cake. |
Nawe iweke mistari miwili, mikate sita kwa kila mstari, juu ya hiyo meza safi, mbele za Bwana. Mambo ya Walawi 24:6 |
You shall set them in two rows, six on a row, on the pure gold table before Yahweh. |
Nawe utatia ubani safi juu ya kila mstari, ili uwe ukumbusho kwa hiyo mikate, sadaka ya kusongezwa kwa Bwana kwa moto. Mambo ya Walawi 24:7 |
You shall put pure frankincense on each row, that it may be to the bread for a memorial, even an offering made by fire to Yahweh. |
Kila siku ya Sabato ataipanga mbele za Bwana daima; ni kwa ajili ya wana wa Israeli, agano la milele. Mambo ya Walawi 24:8 |
Every Sabbath day he shall set it in order before Yahweh continually. It is on the behalf of the children of Israel an everlasting covenant. |
Nayo itakuwa ya Haruni na wanawe; nao wataila katika mahali patakatifu; kwa sababu kwake ni takatifu sana katika sadaka zisongezwazo kwa Bwana kwa moto, kwa amri ya milele. Mambo ya Walawi 24:9 |
It shall be for Aaron and his sons; and they shall eat it in a holy place: for it is most holy to him of the offerings of Yahweh made by fire by a perpetual statute." |
Ikawa mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, ambaye babaye alikuwa Mmisri, akatokea kati ya wana wa Israeli; na huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, na Mwisraeli mmoja, wakapigana pamoja ndani ya marago; Mambo ya Walawi 24:10 |
The son of an Israelite woman, whose father was an Egyptian, went out among the children of Israel; and the son of the Israelite woman and a man of Israel strove together in the camp. |
kisha huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli akalikufuru hilo Jina, na kuapiza; nao wakamleta kwa Musa. Na jina la mamaye alikuwa akiitwa Shelomithi, binti ya Dibri, wa kabila ya Dani. Mambo ya Walawi 24:11 |
The son of the Israelite woman blasphemed the Name, and cursed; and they brought him to Moses. His mother's name was Shelomith, the daughter of Dibri, of the tribe of Dan. |
Nao wakamtia kifungoni, ili wapate kuambiwa neno litakalotoka kinywani pa Bwana. Mambo ya Walawi 24:12 |
They put him in custody, until the will of Yahweh should be declared to them. |
Na Bwana akasema na Musa, na kumwambia, Mambo ya Walawi 24:13 |
Yahweh spoke to Moses, saying, |
Mtoe huyo aliyeapiza nje ya marago; na wale wote waliomsikia na waweke mikono yao kichwani mwake, kisha mkutano wote na wamwue kwa kumpiga kwa mawe. Mambo ya Walawi 24:14 |
"Bring out of the camp him who cursed; and let all who heard him lay their hands on his head, and let all the congregation stone him. |
Nawe nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake atachukua dhambi yake. Mambo ya Walawi 24:15 |
You shall speak to the children of Israel, saying, 'Whoever curses his God shall bear his sin. |
Na yeye atakayelikufuru jina la Bwana hakika atauawa; mkutano wote watamwua kwa kumpiga kwa mawe; kama ni mgeni, kama ni mzalia, hapo atakapolikufuru jina la Bwana atauawa. Mambo ya Walawi 24:16 |
He who blasphemes the name of Yahweh, he shall surely be put to death; all the congregation shall certainly stone him: the foreigner as well as the native-born, when he blasphemes the Name, shall be put to death. |
Na mtu ampigaye mtu hata akafa, lazima atauawa; Mambo ya Walawi 24:17 |
"'He who strikes any man mortally shall surely be put to death. |
na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai. Mambo ya Walawi 24:18 |
He who strikes a animal mortally shall make it good, life for life. |
Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo; Mambo ya Walawi 24:19 |
If anyone injures his neighbor; as he has done, so shall it be done to him: |
jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo. Mambo ya Walawi 24:20 |
fracture for fracture, eye for eye, tooth for tooth; as he has injured someone, so shall it be done to him. |
Na mtu amwuaye mnyama atalipa; na yeye atakayemwua binadamu atauawa. Mambo ya Walawi 24:21 |
He who kills an animal shall make it good; and he who kills a man shall be put to death. |
Mtakuwa na sheria moja tu, kwa huyo aliye mgeni, na kwa mzalia; kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. Mambo ya Walawi 24:22 |
You shall have one kind of law, for the foreigner as well as the native-born: for I am Yahweh your God.'" |
Musa akanena na wana wa Israeli, nao wakamtoa huyo aliyeapiza nje ya marago, wakamwua kwa kumpiga kwa mawe. Wana wa Israeli wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Musa. Mambo ya Walawi 24:23 |
Moses spoke to the children of Israel; and they brought forth him who had cursed out of the camp, and stoned him with stones. The children of Israel did as Yahweh commanded Moses. |