Wakati huo hao vichwa vya nyumba za mababa ya Walawi wakamwendea Eleazari, kuhani, na Yoshua, mwana wa Nuni, na hao waliokuwa vichwa vya nyumba za mababa ya kabila za wana wa Israeli;
Then came near the heads of fathers' [houses] of the Levites to Eleazar the priest, and to Joshua the son of Nun, and to the heads of fathers' [houses] of the tribes of the children of Israel;
wakanena nao hapo Shilo katika nchi ya Kanaani, wakisema, Yeye Bwana aliamuru kwa mkono wa Musa kwamba sisi tupewe miji tupate kukaa humo, pamoja na malisho yake kwa ajili ya wanyama wetu wa mifugo.
and they spoke to them at Shiloh in the land of Canaan, saying, Yahweh commanded Moses to give us cities to dwell in, with the suburbs of it for our cattle.
Basi wana wa Israeli wakawapa Walawi miji hii, pamoja na malisho yake, katika urithi wao, sawasawa na hiyo amri ya Bwana.
The children of Israel gave to the Levites out of their inheritance, according to the commandment of Yahweh, these cities with their suburbs.
Kura ikatokea kwa ajili ya jamaa za Wakohathi; na wana wa Haruni kuhani, waliokuwa katika Walawi, walipata miji kumi na mitatu kwa kura katika kabila ya Yuda, na katika kabila ya Simeoni, na katika kabila ya Benyamini.
The lot came out for the families of the Kohathites: and the children of Aaron the priest, who were of the Levites, had by lot out of the tribe of Judah, and out of the tribe of the Simeonites, and out of the tribe of Benjamin, thirteen cities.
Kisha Wakohathi wengine waliosalia walipata kwa kura katika jamaa za kabila ya Efraimu, na katika kabila ya Dani, na katika hiyo nusu ya kabila ya Manase, miji kumi.
The rest of the children of Kohath had by lot out of the families of the tribe of Ephraim, and out of the tribe of Dan, and out of the half-tribe of Manasseh, ten cities.
Tena wana wa Gershoni walipata kwa kura katika jamaa za kabila ya Isakari, na katika kabila ya Asheri, na katika kabila ya Naftali, na katika hiyo nusu ya kabila ya Manase huko Bashani, miji kumi na mitatu.
The children of Gershon had by lot out of the families of the tribe of Issachar, and out of the tribe of Asher, and out of the tribe of Naphtali, and out of the half-tribe of Manasseh in Bashan, thirteen cities.
Na wana wa Merari kwa kuandama jamaa zao walipata katika kabila ya Reubeni, na katika kabila ya Gadi, na katika kabila ya Zabuloni, miji kumi na miwili.
The children of Merari according to their families had out of the tribe of Reuben, and out of the tribe of Gad, and out of the tribe of Zebulun, twelve cities.
Kisha wana wa Israeli waliwapa Walawi kwa kura miji hiyo pamoja na malisho yake, kama Bwana alivyoamuru kwa mkono wa Musa.
The children of Israel gave by lot to the Levites these cities with their suburbs, as Yahweh commanded by Moses.
Kisha wakawapa katika kabila ya wana wa Yuda, na katika kabila ya wana wa Simeoni, miji hii iliyotajwa hapa kwa majina;
They gave out of the tribe of the children of Judah, and out of the tribe of the children of Simeon, these cities which are [here] mentioned by name:
nayo ilikuwa kwa ajili ya wana wa Haruni, wa jamaa ya Wakohathi, waliokuwa wa wana wa Lawi; kwa kuwa kura ya kwanza ilikuwa ni yao.
and they were for the children of Aaron, of the families of the Kohathites, who were of the children of Levi; for theirs was the first lot.
Nao wakawapa Kiriath-arba, huyo Arba alikuwa baba yake Anaki, (ndio Hebroni), katika nchi ya vilima ya Yuda, pamoja na malisho yake yaliyouzunguka pande zote.
They gave them Kiriath Arba, [which Arba was] the father of Anak (the same is Hebron), in the hill-country of Judah, with the suburbs of it round about it.
Lakini mashamba ya mji, na vile vijiji vyake, wakampa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
But the fields of the city, and the villages of it, gave they to Caleb the son of Jephunneh for his possession.
Kisha wakawapa wana wa Haruni kuhani Hebroni pamoja na malisho yake, huo mji wa kukimbilia kwa ajili ya mwuaji, na Libna pamoja na malisho yake;
To the children of Aaron the priest they gave Hebron with its suburbs, the city of refuge for the manslayer, and Libnah with its suburbs,
na Yatiri pamoja na malisho yake, na Eshtemoa pamoja na malisho yake;
and Jattir with its suburbs, and Eshtemoa with its suburbs,
na Holoni pamoja na malisho yake, na Debiri pamoja na malisho yake;
and Holon with its suburbs, and Debir with its suburbs,
na Aini pamoja na malisho yake, na Yuta pamoja na malisho yake, na Bethshemeshi pamoja na malisho yake; miji kenda katika kabila hizo mbili.
and Ain with its suburbs, and Juttah with its suburbs, [and] Beth-shemesh with its suburbs; nine cities out of those two tribes.
Tena katika kabila ya Benyamini, Gibeoni pamoja na malisho yake, na Geba pamoja na malisho yake;
Out of the tribe of Benjamin, Gibeon with its suburbs, Geba with its suburbs,
na Anathothi pamoja na malisho yake, na Almoni pamoja na malisho yake; miji minne.
Anathoth with its suburbs, and Almon with its suburbs; four cities.
Miji yote ya wana wa Haruni, makuhani, ilikuwa ni miji kumi na mitatu, pamoja na malisho yake.
All the cities of the children of Aaron, the priests, were thirteen cities with their suburbs.
Na jamaa za wana wa Kohathi, Walawi, hao wana wengine wa Kohathi waliosalia, wao walikuwa na miji ya kura yao katika kabila ya Efraimu.
The families of the children of Kohath, the Levites, even the rest of the children of Kohath, they had the cities of their lot out of the tribe of Ephraim.
Nao wakawapa Shekemu pamoja na malisho yake, katika nchi ya vilima ya Efraimu, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji; na Gezeri pamoja na malisho yake;
They gave them Shechem with its suburbs in the hill-country of Ephraim, the city of refuge for the manslayer, and Gezer with its suburbs,
na Kibisaumu pamoja na malisho yake, na Beth-horoni pamoja na malisho yake, miji minne.
and Kibzaim with its suburbs, and Beth Horon with its suburbs; four cities.
Tena katika kabila ya Dani Elteke pamoja na malisho yake, na Gibethoni pamoja na malisho yake;
Out of the tribe of Dan, Elteke with its suburbs, Gibbethon with its suburbs,
na Aiyaloni pamoja na malisho yake, na Gath-rimoni pamoja na malisho yake; miji minne.
Aijalon with its suburbs, Gath-rimmon with its suburbs; four cities.
Tena katika hiyo nusu ya kabila ya Manase, Taanaki pamoja na malisho yake, na Gath-rimoni pamoja na malisho yake; miji miwili.
Out of the half-tribe of Manasseh, Taanach with its suburbs, and Gath-rimmon with its suburbs; two cities.
Miji yote ya jamaa za wana wa Kohathi waliosalia ilikuwa ni miji kumi, pamoja na malisho yake.
All the cities of the families of the rest of the children of Kohath were ten with their suburbs.
Tena wana wa Gershoni, katika jamaa za Walawi, waliwapa, katika hiyo nusu ya kabila ya Manase, Golani katika Bashani pamoja na malisho yake, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji; na Beeshtera pamoja na malisho yake; miji miwili.
To the children of Gershon, of the families of the Levites, out of the half-tribe of Manasseh [they gave] Golan in Bashan with its suburbs, the city of refuge for the manslayer, and Be-eshterah with its suburbs; two cities.
Tena katika kabila ya Isakari, Kishioni pamoja na malisho yake, na Daberathi pamoja na malisho yake;
Out of the tribe of Issachar, Kishion with its suburbs, Daberath with its suburbs,
na Yarmuthi pamoja na malisho yake, na Enganimu pamoja na malisho yake; miji minne.
Jarmuth with its suburbs, En Gannim with its suburbs; four cities.
Tena katika kabila ya Asheri, Mishali pamoja na malisho yake, na Abdoni pamoja na malisho yake;
Out of the tribe of Asher, Mishal with its suburbs, Abdon with its suburbs,
na Helkathi pamoja na malisho yake, na Rehobu pamoja na malisho yake; miji minne.
Helkath with its suburbs, and Rehob with its suburbs; four cities.
Tena katika kabila ya Naftali, Kedeshi katika Galilaya pamoja na malisho yake, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji, na Hamoth-dori pamoja na malisho yake, na Kartani pamoja na malisho yake; miji mitatu.
Out of the tribe of Naphtali, Kedesh in Galilee with its suburbs, the city of refuge for the manslayer, and Hammothdor with its suburbs, and Kartan with its suburbs; three cities.
Miji yote ya Wagershoni kwa kuandama jamaa zao ilikuwa ni miji kumi na mitatu, pamoja na malisho yake.
All the cities of the Gershonites according to their families were thirteen cities with their suburbs.
Tena jamaa za wana wa Merari, hao Walawi waliosalia, katika kabila ya Zabuloni, Yokneamu pamoja na malisho yake, na Karta pamoja na malisho yake,
To the families of the children of Merari, the rest of the Levites, out of the tribe of Zebulun, Jokneam with its suburbs, and Kartah with its suburbs,
na Dimna pamoja na malisho yake, na Nahalali pamoja na malisho yake; miji minne.
Dimnah with its suburbs, Nahalal with its suburbs; four cities.
Tena katika kabila ya Reubeni, Bezeri pamoja na malisho yake, na Yahasa pamoja na malisho yake,
Out of the tribe of Reuben, Bezer with its suburbs, and Jahaz with its suburbs,
na Kedemothi pamoja na malisho yake, na Mefaathi pamoja na malisho yake; miji minne.
Kedemoth with its suburbs, and Mephaath with its suburbs; four cities.
Tena katika kabila ya Gadi Ramothi katika Gileadi pamoja na malisho yake, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji, na Mahanaimu pamoja na malisho yake;
Out of the tribe of Gad, Ramoth in Gilead with its suburbs, the city of refuge for the manslayer, and Mahanaim with its suburbs,
na Heshboni pamoja na malisho yake, na Yazeri pamoja na malisho yake; jumla yake miji minne.
Heshbon with its suburbs, Jazer with its suburbs; four cities in all.
Miji hiyo yote ilikuwa ni miji ya wana wa Merari kwa kuandama jamaa zao, ni hizo jamaa za Walawi zilizosalia; na kura yao ilikuwa ni miji kumi na miwili.
All [these were] the cities of the children of Merari according to their families, even the rest of the families of the Levites; and their lot was twelve cities.
Miji yote ya Walawi iliyokuwa kati ya milki ya wana wa Israeli ilikuwa ni miji arobaini na minane, pamoja na malisho yake.
All the cities of the Levites in the midst of the possession of the children of Israel were forty-eight cities with their suburbs.
Miji hiyo kila mmoja ulikuwa pamoja na malisho yake, yaliyouzunguka pande zote; ndivyo ilivyokuwa katika miji hiyo yote.
These cities were every one with their suburbs round about them: thus it was with all these cities.
Basi Bwana aliwapa Israeli nchi hiyo yote, ambayo aliapa kwamba atawapa baba zao; nao wakaimiliki, na kukaa mumo.
So Yahweh gave to Israel all the land which he swore to give to their fathers; and they possessed it, and lived therein.
Kisha Bwana akawapa raha pande zote, sawasawa na hayo yote aliyokuwa amewaapia baba zao; wala katika adui zao wote hakusimama hata mtu mmoja miongoni mwao mbele zao; yeye Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Yahweh gave them rest round about, according to all that he swore to their fathers: and there stood not a man of all their enemies before them; Yahweh delivered all their enemies into their hand.
Halikuanguka neno lo lote katika jambo lo lote lililokuwa ni jema ambalo Bwana alikuwa amelinena katika habari ya nyumba ya Israeli; yalitimia mambo yote.
There failed not anything of any good thing which Yahweh had spoken to the house of Israel; all came to pass.