1
Makuhani Walawi, kabila yote ya Lawi, wasiwe na fungu wala urithi pamoja na Israeli; watakula sadaka za Bwana zifanywazo kwa moto, na urithi wake.
The Levitical priests—indeed the whole tribe of Levi—shall have no portion or inheritance with Israel. They are to eat the food offerings to the LORD; that is their inheritance.
2
Wala wasiwe na urithi kati ya ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaambia.
Although they have no inheritance among their brothers, the LORD is their inheritance, as He promised them.
3
Na hii itakuwa haki ya makuhani kwa watu hao wasongezao sadaka, ikiwa ni ng'ombe au kondoo wampe kuhani mkono, na mashavu mawili, na tumbo.
This shall be the priests’ share from the people who offer a sacrifice, whether a bull or a sheep: the priests are to be given the shoulder, the jowls, and the stomach.
4
Malimbuko ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na manyoya ya kwanza ya kondoo zako, umpe.
You are to give them the firstfruits of your grain, new wine, and oil, and the first wool sheared from your flock.
5
Kwani Bwana, Mungu wako, amemchagua katika kabila zako zote, asimame atumike kwa jina la Bwana, yeye na wanawe milele.
For the LORD your God has chosen Levi and his sons out of all your tribes to stand and minister in His name for all time.
6
Na akija Mlawi atokaye katika malango yako mojawapo, katika Israeli yote alipokuwa akikaa, akaja kwa mapenzi yote ya nafsi yake mahali atakapochagua Bwana;
Now if a Levite moves from any town of residence throughout Israel and comes in all earnestness to the place the LORD will choose,
7
na atumike kwa jina la Bwana, Mungu wake, kama wafanyavyo ndugu zake wote, Walawi wasimamao huko mbele za Bwana.
then he shall serve in the name of the LORD his God like all his fellow Levites who stand there before the LORD.
8
Wawe na fungu sawasawa la kula, pamoja na haya yaliyomfikilia kwa kuuzwa urithi wa baba zake.
They shall eat equal portions, even though he has received money from the sale of his father’s estate.
9
Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.
When you enter the land that the LORD your God is giving you, do not imitate the detestable ways of the nations there.
10
Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,
Let no one be found among you who sacrifices his son or daughter in the fire, practices divination or conjury, interprets omens, practices sorcery,
11
wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.
casts spells, consults a medium or spiritist, or inquires of the dead.
12
Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.
For whoever does these things is detestable to the LORD. And because of these detestable things, the LORD your God is driving out the nations before you.
13
Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako.
You must be blameless before the LORD your God.
14
Maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanaoshika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe, Bwana, Mungu wako, hakukupa ruhusa kutenda hayo.
Though these nations, which you will dispossess, listen to conjurers and diviners, the LORD your God has not permitted you to do so.
15
Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye.
The LORD your God will raise up for you a prophet like me from among your brothers. You must listen to him.
16
Kama vile ulivyotaka kwa Bwana, Mungu wako, huko Horebu, siku ya kusanyiko, ukisema, Nisisikie tena sauti ya Bwana, Mungu wangu, wala nisiuone tena moto huu mkubwa, nisije nikafa.
This is what you asked of the LORD your God at Horeb on the day of the assembly, when you said, “Let us not hear the voice of the LORD our God or see this great fire anymore, so that we will not die!”
17
Bwana akaniambia, Wametenda vema kusema walivyosema.
Then the LORD said to me, “They have spoken well.
18
Mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.
I will raise up for them a prophet like you from among their brothers. I will put My words in his mouth, and he will tell them everything I command him.
19
Hata itakuwa, mtu asiyesikiliza maneno yangu atakayosema yule kwa jina langu, nitalitaka kwake.
And I will hold accountable anyone who does not listen to My words that the prophet speaks in My name.
20
Lakini nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu, ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena katika jina la miungu mingine, nabii yule atakufa.
But if any prophet dares to speak a message in My name that I have not commanded him to speak, or to speak in the name of other gods, that prophet must be put to death.”
21
Nawe ukisema moyoni mwako, Tutajuaje neno asilolinena Bwana?
You may ask in your heart, “How can we recognize a message that the LORD has not spoken?”
22
Atakaponena nabii kwa jina la Bwana, lisifuate jambo lile wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena Bwana; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimwogope
When a prophet speaks in the name of the LORD and the message does not come to pass or come true, that is a message the LORD has not spoken. The prophet has spoken presumptuously. Do not be afraid of him.