Kumbukumbu la Torati 33 Swahili & English
Listen/Download AudioKumbukumbu la Torati 33 (Swahili) | Deuteronomy 33 (English) |
---|---|
Hii ndiyo baraka ya Musa, huyo mtu wa Mungu, aliyowabarikia wana wa Israeli kabla ya kufa kwake. Kumbukumbu la Torati 33:1 |
This is the blessing, with which Moses the man of God blessed the children of Israel before his death. |
Akasema,Bwana alitoka Sinai,Akawaondokea kutoka Seiri;Aliangaza katika kilima cha Parani,Akaja Meribath-Kadeshi.Upande wake wa kuume Palikuwa na sheria ya moto-moto kwao. Kumbukumbu la Torati 33:2 |
He said, Yahweh came from Sinai, Rose from Seir to them; He shined forth from Mount Paran, He came from the ten thousands of holy ones: At his right hand was a fiery law for them. |
Hakika awapenda hayo makabila ya watu; Watakatifu wake wote wamo mkononi mwako; Nao waliketi miguuni pako; Watapokea kila mmoja katika maneno yako. Kumbukumbu la Torati 33:3 |
Yes, he loves the people; All his saints are in your hand: They sat down at your feet; [Everyone] shall receive of your words. |
Musa alituagiza torati, Ni urithi kwa mkutano wa Yakobo. Kumbukumbu la Torati 33:4 |
Moses commanded us a law, An inheritance for the assembly of Jacob. |
Akawa mfalme katika Yeshuruni, Walipokutanika wakuu wa watu, Makabila yote ya Israeli pamoja. Kumbukumbu la Torati 33:5 |
He was king in Jeshurun, When the heads of the people were gathered, All the tribes of Israel together. |
Reubeni na aishi, asife; Lakini watu wake na wawe wachache. Kumbukumbu la Torati 33:6 |
Let Reuben live, and not die; Nor let his men be few. |
Na baraka ya Yuda ni hii; akasema, Isikize, Ee Bwana, sauti ya Yuda, Umlete ndani kwa watu wake; Alijitetea kwa mikono yake; Nawe utakuwa msaada juu ya adui zake. Kumbukumbu la Torati 33:7 |
This is [the blessing] of Judah: and he said, Hear, Yahweh, the voice of Judah, Bring him in to his people. With his hands he contended for himself; You shall be a help against his adversaries. |
Akamnena Lawi, Thumimu yako na Urimu yako vina mtakatifu wako, Uliyemjaribu huko Masa; Ukateta naye kwenye maji ya Meriba. Kumbukumbu la Torati 33:8 |
Of Levi he said, Your Thummim and your Urim are with your godly one, Whom you did prove at Massah, With whom you did strive at the waters of Meribah; |
Aliyemtaja baba yake na mama yake, Mimi sikumwona; Wala nduguze hakuwakubali; Wala hakuwajua watoto wake mwenyewe; Maana wameliangalia neno lako, Wamelishika agano lako. Kumbukumbu la Torati 33:9 |
Who said of his father, and of his mother, I have not seen him; Neither did he acknowledge his brothers, Nor knew he his own children: For they have observed your word, Keep your covenant. |
Watamfundisha Yakobo hukumu zako, Na Israeli torati yako, Wataweka uvumba mbele zako, Na sadaka nzima za kuteketezwa madhabahuni mwako. Kumbukumbu la Torati 33:10 |
They shall teach Jacob your ordinances, Israel your law: They shall put incense before you, Whole burnt offering on your altar. |
Ee Bwana, ubariki mali zake, Utakabali kazi ya mikono yake; Uwapige viuno vyao waondokao juu yake, Na wenye kumchukia, wasiinuke tena. Kumbukumbu la Torati 33:11 |
Bless, Yahweh, his substance, Accept the work of his hands: Smite through the loins of those who rise up against him, Of those who hate him, that they not rise again. |
Akamnena Benyamini, Mpenzi wa Bwana atakaa salama kwake; Yuamfunika mchana kutwa, Naye hukaa kati ya mabega yake. Kumbukumbu la Torati 33:12 |
Of Benjamin he said, The beloved of Yahweh shall dwell in safety by him; He covers him all the day long, He dwells between his shoulders. |
Na Yusufu akamnena, Nchi yake na ibarikiwe na Bwana; Kwa vitu vya thamani vya mbinguni, kwa huo umande, Na kwa kilindi kilalacho chini, Kumbukumbu la Torati 33:13 |
Of Joseph he said, Blessed of Yahweh be his land, For the precious things of the heavens, for the dew, For the deep that couches beneath, |
Na kwa vitu vilivyo bora vya matunda ya jua, Na kwa vitu vilivyo bora vya maongeo ya miezi, Kumbukumbu la Torati 33:14 |
For the precious things of the fruits of the sun, For the precious things of the growth of the moons, |
Na kwa vitu viteule vya milima ya kale, Na kwa vitu vilivyo bora vya vilima vya milele, Kumbukumbu la Torati 33:15 |
For the chief things of the ancient mountains, For the precious things of the everlasting hills, |
Na kwa vitu vilivyo bora vya nchi, na kujaa kwake, Na uradhi wake aliyekaa ndani ya kile kijiti; Na ije baraka juu ya kichwa chake Yusufu, Juu ya utosi wa kichwa chake aliyetengwa na nduguze. Kumbukumbu la Torati 33:16 |
For the precious things of the earth and the fullness of it, The good will of him who lived in the bush. Let [the blessing] come on the head of Joseph, On the crown of the head of him who was separate from his brothers. |
Mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe wake mume, enzi ni yake; Na pembe zake ni pembe za nyati; Kwa hizo atayasukuma mataifa yote, hata ncha za nchi; Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu, Nao ni maelfu ya Manase. Kumbukumbu la Torati 33:17 |
The firstborn of his herd, majesty is his; His horns are the horns of the wild-ox: With them he shall push the peoples all of them, [even] the ends of the earth: They are the ten thousands of Ephraim, They are the thousands of Manasseh. |
Na Zabuloni akamnena, Furahi Zabuloni, katika kutoka kwako; Kumbukumbu la Torati 33:18 |
Of Zebulun he said, Rejoice, Zebulun, in your going out; Issachar, in your tents. |
Watayaita mataifa waje mlimani; Wakasongeze huko sadaka za haki; Kwa kuwa watanyonya wingi wa bahari, Na akiba zilizofichamana za mchangani. Kumbukumbu la Torati 33:19 |
They shall call the peoples to the mountain; There shall they offer sacrifices of righteousness: For they shall suck the abundance of the seas, The hidden treasures of the sand. |
Na Gadi akamnena, Na abarikiwe amwongezaye Gadi; Yeye hukaa kama simba mke, Hurarua mkono, naam, na utosi wa kichwa. Kumbukumbu la Torati 33:20 |
Of Gad he said, Blessed be he who enlarges Gad: He dwells as a lioness, Tears the arm, yes, the crown of the head. |
Akajichagulia sehemu ya kwanza, Kwani ndiko lilikowekwa fungu la mtoa-sheria; Akaja pamoja na wakuu wa watu, Akaitekeleza haki ya Bwana, Na hukumu zake kwa Israeli. Kumbukumbu la Torati 33:21 |
He provided the first part for himself, For there was the lawgiver's portion reserved; He came [with] the heads of the people; He executed the righteousness of Yahweh, His ordinances with Israel. |
Na Dani akamnena, Dani ni mwana-simba, Arukaye kutoka Bashani. Kumbukumbu la Torati 33:22 |
Of Dan he said, Dan is a lion's cub, That leaps forth from Bashan. |
Na Naftali akamnena, Ee Naftali, uliyeshiba fadhili, Uliyejawa na baraka ya Bwana; Umiliki magharibi na kusini. Kumbukumbu la Torati 33:23 |
Of Naphtali he said, Naphtali, satisfied with favor, Full with the blessing of Yahweh, Possess you the west and the south. |
Na Asheri akamnena, Na abarikiwe Asheri kwa watoto; Na akubaliwe katika nduguze, Na achovye mguu wake katika mafuta. Kumbukumbu la Torati 33:24 |
Of Asher he said, Blessed be Asher with children; Let him be acceptable to his brothers, Let him dip his foot in oil. |
Makomeo yako yatakuwa ya chuma na shaba; Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako. Kumbukumbu la Torati 33:25 |
Your bars shall be iron and brass; As your days, so shall your strength be. |
Hapana aliyefanana na Mungu, Ee Yeshuruni, Ajaye amepanda juu ya mbingu ili akusaidie. Na juu ya mawingu katika utukufu wake. Kumbukumbu la Torati 33:26 |
There is none like God, Jeshurun, Who rides on the heavens for your help, In his excellency on the skies. |
Mungu wa milele ndiye makazi yako, Na mikono ya milele i chini yako. Na mbele yako amemsukumia mbali adui; Akasema, Angamiza. Kumbukumbu la Torati 33:27 |
The eternal God is [your] dwelling-place, Underneath are the everlasting arms. He thrust out the enemy from before you, Said, Destroy. |
Na Israeli anakaa salama, Chemchemi ya Yakobo peke yake, Katika nchi ya ngano na divai; Naam, mbingu zake zadondoza umande. Kumbukumbu la Torati 33:28 |
Israel dwells in safety, The fountain of Jacob alone, In a land of grain and new wine; Yes, his heavens drop down dew. |
U heri, Israeli. Ni nani aliye kama wewe, taifa lililookolewa na Bwana! Ndiye ngao ya msaada wako, Na upanga wa utukufu wako; Na adui zako watajitiisha chini yako, Nawe utapakanyaga mahali pao pa juu. Kumbukumbu la Torati 33:29 |
Happy are you, Israel: Who is like you, a people saved by Yahweh, The shield of your help, The sword of your excellency! Your enemies shall submit themselves to you; You shall tread on their high places. |