Kumbukumbu la Torati BSB

Kumbukumbu la Torati 14

Deuteronomy Chapter 14

1
Ninyi mmekuwa wana wa Bwana, Mungu wenu; msijitoje miili yenu, wala msifanye upaa katikati ya macho yenu kwa ajili ya aliyekufa.
You are sons of the LORD your God; do not cut yourselves or shave your foreheads on behalf of the dead,
2
Kwa kuwa u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako, na Bwana amekuchagua kuwa watu wake hasa, kuliko mataifa yote yaliyo juu ya uso wa nchi.
for you are a people holy to the LORD your God. The LORD has chosen you to be a people for His prized possession out of all the peoples on the face of the earth.
3
Usile kitu cho chote kichukizacho.
You must not eat any detestable thing.
4
Wanyama mtakaokula ni hawa ng'ombe, na kondoo, na mbuzi,
These are the animals that you may eat: The ox, the sheep, the goat,
5
kulungu, na paa, na kongoni, na mbuzi wa mwitu, na paa mweupe, na pofu, na mbuzi wa mlima;
the deer, the gazelle, the roe deer, the wild goat, the ibex, the antelope, and the mountain sheep.
6
na kila mnyama aliyepasuliwa ukwato, ukapasuka ukwato wake zikawa mbili, naye ni mnyama mwenye kucheua akatafuna tena, katika wanyama wote, ndiye mnyama mtakayemla.
You may eat any animal that has a split hoof divided in two and that chews the cud.
7
Lakini, hawa msile katika wale wenye kucheua, na hao waliopasuliwa ukwato; ngamia, na sungura, na kwang'a, kwa kuwa hucheua, lakini hawakupasuliwa kwato, ni najisi kwenu;
But of those that chew the cud or have a completely divided hoof, you are not to eat the following: the camel, the rabbit, or the rock badger. Although they chew the cud, they do not have a divided hoof. They are unclean for you,
8
na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.
as well as the pig; though it has a divided hoof, it does not chew the cud. It is unclean for you. You must not eat its meat or touch its carcass.
9
Mtakula hawa katika wote walio majini; kila kilicho na mapezi na magamba mtakula;
Of all the creatures that live in the water, you may eat anything with fins and scales,
10
na kila kisichokuwa na mapezi na magamba msile; ni najisi kwenu.
but you may not eat anything that does not have fins and scales; it is unclean for you.
11
Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.
You may eat any clean bird,
12
Lakini hawa msiwale; tai, na furukombe, na kipungu;
but these you may not eat: the eagle, the bearded vulture, the black vulture,
13
na kengewa, na kozi, na mwewe kwa aina zake;
the red kite, the falcon, any kind of kite,
14
na kila kunguru kwa aina zake;
any kind of raven,
15
na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;
the ostrich, the screech owl, the gull, any kind of hawk,
16
na bundi, na mumbi, na bundi mkubwa;
the little owl, the great owl, the white owl,
17
na mwari, na nderi, na mnandi;
the desert owl, the osprey, the cormorant,
18
na membe, na koikoi, kwa aina zake; na hudihudi, na popo.
the stork, any kind of heron, the hoopoe, or the bat.
19
Na wadudu wote watambaao wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.
All flying insects are unclean for you; they may not be eaten.
20
Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.
But you may eat any clean bird.
21
Msile nyamafu yo yote; waweza kumpa mgeni aliye ndani ya malango yako, ili apate kula; au kumliza mtu wa mataifa; kwa kuwa wewe u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mamaye.
You are not to eat any carcass; you may give it to the foreigner residing within your gates, and he may eat it, or you may sell it to a foreigner. For you are a holy people belonging to the LORD your God. You must not cook a young goat in its mother’s milk.
22
Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka.
You must be sure to set aside a tenth of all the produce brought forth each year from your fields.
23
Nawe utakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake, zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yako ya ng'ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wako, daima.
And you are to eat a tenth of your grain, new wine, and oil, and the firstborn of your herds and flocks, in the presence of the LORD your God at the place He will choose as a dwelling for His Name, so that you may learn to fear the LORD your God always.
24
Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia Bwana, Mungu wako;
But if the distance is too great for you to carry that with which the LORD your God has blessed you, because the place where the LORD your God will choose to put His Name is too far away,
25
ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako;
then exchange it for money, take the money in your hand, and go to the place the LORD your God will choose.
26
na zile fedha zitumie kwa cho chote itakachotamani roho yako, ng'ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako cho chote; nawe utakula huko mbele za Bwana, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako;
Then you may spend the money on anything you desire: cattle, sheep, wine, strong drink, or anything you wish. You are to feast there in the presence of the LORD your God and rejoice with your household.
27
na Mlawi aliye ndani ya malango yako usimwache, kwani hana fungu wala urithi pamoja nawe.
And do not neglect the Levite within your gates, since he has no portion or inheritance among you.
28
Kila mwaka wa tatu, mwisho wake, toa fungu la kumi lote la maongeo yako ya mwaka huo, uliweke ndani ya malango yako;
At the end of every three years, bring a tenth of all your produce for that year and lay it up within your gates.
29
na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako, na waje wale na kushiba; ili kwamba Bwana, Mungu wako, akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.
Then the Levite (because he has no portion or inheritance among you), the foreigner, the fatherless, and the widow within your gates may come and eat and be satisfied. And the LORD your God will bless you in all the work of your hands.

Chagua Sura