1 Wakorintho 5 Swahili & English
Listen/Download Audio1 Wakorintho 5 (Swahili) | 1st Corinthians 5 (English) |
---|---|
Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye. 1 Wakorintho 5:1 |
It is actually reported that there is sexual immorality among you, and such sexual immorality as is not even named among the Gentiles, that one has his father's wife. |
Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo. 1 Wakorintho 5:2 |
You are puffed up, and didn't rather mourn, that he who had done this deed might be removed from among you. |
Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo. 1 Wakorintho 5:3 |
For I most assuredly, as being absent in body but present in spirit, have already, as though I were present, judged him who has done this thing. |
Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu; 1 Wakorintho 5:4 |
In the name of our Lord Jesus Christ, you being gathered together, and my spirit, with the power of our Lord Jesus Christ, |
kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu. 1 Wakorintho 5:5 |
are to deliver such a one to Satan for the destruction of the flesh, that the spirit may be saved in the day of the Lord Jesus. |
Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima? 1 Wakorintho 5:6 |
Your boasting is not good. Don't you know that a little yeast leavens the whole lump? |
Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo; 1 Wakorintho 5:7 |
Purge out the old yeast, that you may be a new lump, even as you are unleavened. For indeed Christ, our Passover, has been sacrificed in our place. |
basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli. 1 Wakorintho 5:8 |
Therefore let us keep the feast, not with old yeast, neither with the yeast of malice and wickedness, but with the unleavened bread of sincerity and truth. |
Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi. 1 Wakorintho 5:9 |
I wrote to you in my letter to have no company with sexual sinners; |
Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang'anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia. 1 Wakorintho 5:10 |
yet not at all meaning with the sexual sinners of this world, or with the covetous and extortioners, or with idolaters; for then you would have to leave the world. |
Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang'anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye. 1 Wakorintho 5:11 |
But as it is, I wrote to you not to associate with anyone who is called a brother who is a sexual sinner, or covetous, or an idolater, or a slanderer, or a drunkard, or an extortioner. Don't even eat with such a person. |
Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani? 1 Wakorintho 5:12 |
For what have I to do with also judging those who are outside? Don't you judge those who are within? |
Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu. 1 Wakorintho 5:13 |
But those who are outside, God judges. "Put away the wicked man from among yourselves." |