1 Wakorintho 14

1st Corinthians Chapter 14

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Ufuateni upendo, na kutaka sana karama za rohoni, lakini zaidi kwamba mpate kuhutubu.
Follow after love, and earnestly desire spiritual gifts, but especially that you may prophesy.
2
Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake.
For he who speaks in another language speaks not to men, but to God; for no one understands; but in the Spirit he speaks mysteries.
3
Bali yeye ahutubuye, asema na watu maneno ya kuwajenga, na kuwafariji, na kuwatia moyo.
But he who prophesies speaks to men for their edification, exhortation, and consolation.
4
Yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijenga kanisa.
He who speaks in another language edifies himself, but he who prophesies edifies the assembly.
5
Nami nataka ninyi nyote mnene kwa lugha, lakini zaidi sana mpate kuhutubu, maana yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha, isipokuwa afasiri, ili kusudi kanisa lipate kujengwa.
Now I desire to have you all speak with other languages, but rather that you would prophesy. For he is greater who prophesies than he who speaks with other languages, unless he interprets, that the assembly may be built up.
6
Ila sasa, ndugu, nikija kwenu na kunena kwa lugha, nitawafaidia nini, isipokuwa nasema nanyi kwa njia ya ufunuo, au kwa njia ya elimu, au kwa njia ya hotuba, au kwa njia ya fundisho?
But now, brothers,{The word for "brothers" here and where context allows may also be correctly translated "brothers and sisters" or "siblings."} if I come to you speaking with other languages, what would I profit you, unless I speak to you either by way of revelation, or of knowledge, or of prophesying, or of teaching?
7
Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, ikiwa ni filimbi, ikiwa ni kinubi, visipotoa sauti zilizo na tofauti, itatambulikanaje ni wimbo gani unaopigwa kwa filimbi au kwa kinubi?
Even things without life, giving a voice, whether pipe or harp, if they didn't give a distinction in the sounds, how would it be known what is piped or harped?
8
Kwa maana baragumu ikitoa sauti isiyojulikana, ni nani atakayejifanya tayari kwa vita?
For if the trumpet gave an uncertain sound, who would prepare himself for war?
9
Vivyo hivyo na ninyi, msipotoa kwa ulimi neno lililo dhahiri, neno lile linenwalo litajulikanaje? Maana mtakuwa mkinena hewani tu.
So also you, unless you uttered by the tongue words easy to understand, how would it be known what is spoken? For you would be speaking into the air.
10
Yamkini ziko sauti za namna nyingi duniani, wala hakuna moja isiyo na maana.
There are, it may be, so many kinds of sounds in the world, and none of them is without meaning.
11
Basi nisipoijua maana ya ile sauti nitakuwa kama mjinga kwake yeye anenaye; naye anenaye atakuwa mjinga kwangu.
If then I don't know the meaning of the sound, I would be to him who speaks a foreigner, and he who speaks would be a foreigner to me.
12
Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa.
So also you, since you are zealous for spiritual gifts, seek that you may abound to the building up of the assembly.
13
Kwa sababu hiyo yeye anenaye kwa lugha na aombe apewe kufasiri.
Therefore let him who speaks in another language pray that he may interpret.
14
Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
For if I pray in another language, my spirit prays, but my understanding is unfruitful.
15
Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia.
What is it then? I will pray with the spirit, and I will pray with the understanding also. I will sing with the spirit, and I will sing with the understanding also.
16
Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui usemayo?
Otherwise if you bless with the spirit, how will he who fills the place of the unlearned say the "Amen" at your giving of thanks, seeing he doesn't know what you say?
17
Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali yule mwingine hajengwi.
For you most assuredly give thanks well, but the other person is not built up.
18
Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote;
I thank my God, I speak with other languages more than you all.
19
lakini katika kanisa napenda kunena maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.
However in the assembly I would rather speak five words with my understanding, that I might instruct others also, than ten thousand words in another language.
20
Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima.
Brothers, don't be children in thoughts, yet in malice be babies, but in thoughts be mature.
21
Imeandikwa katika torati, Nitasema na watu hawa kwa watu wa lugha nyingine, na kwa midomo ya wageni, wala hata hivyo hawatanisikia, asema Bwana.
In the law it is written, "By men of strange languages and by the lips of strangers I will speak to this people. Not even thus will they hear me, says the Lord."
22
Basi, hizi lugha ni ishara, si kwao waaminio, bali kwao wasioamini lakini kuhutubu si kwa ajili yao wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio.
Therefore other languages are for a sign, not to those who believe, but to the unbelieving; but prophesying is for a sign, not to the unbelieving, but to those who believe.
23
Haya! Ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja, na wote wanene kwa lugha, kisha ikawa wameingia watu wajinga au wasioamini, je! Hawatasema ya kwamba mna wazimu?
If therefore the whole assembly is assembled together and all speak with other languages, and unlearned or unbelieving people come in, won't they say that you are crazy?
24
Lakini wote wakihutubu, kisha akaingia mtu asiyeamini, au mjinga, abainishwa na wote, ahukumiwa na wote;
But if all prophesy, and someone unbelieving or unlearned comes in, he is reproved by all, and he is judged by all.
25
siri za moyo wake huwa wazi; na hivyo atamwabudu Mungu, akianguka kifudifudi, na kukiri ya kuwa Mungu yu kati yenu bila shaka.
And thus the secrets of his heart are revealed. So he will fall down on his face and worship God, declaring that God is among you indeed.
26
Basi, ndugu, imekuwaje? Mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi, ana fundisho, ana ufunuo, ana lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kwa kusudi la kujenga.
What is it then, brothers? When you come together, each one of you has a psalm, has a teaching, has a revelation, has another language, has an interpretation. Let all things be done to build each other up.
27
Kama mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri.
If any man speaks in another language, let it be two, or at the most three, and in turn; and let one interpret.
28
Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu.
But if there is no interpreter, let him keep silent in the assembly, and let him speak to himself, and to God.
29
Na manabii wanene wawili, au watatu, na wengine wapambanue.
Let the prophets speak, two or three, and let the others discern.
30
Lakini mwingine aliyeketi akifunuliwa neno, yule wa kwanza na anyamaze.
But if a revelation is made to another sitting by, let the first keep silent.
31
Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.
For you all can prophesy one by one, that all may learn, and all may be exhorted.
32
Na roho za manabii huwatii manabii.
The spirits of the prophets are subject to the prophets,
33
Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu.
for God is not a God of confusion, but of peace. As in all the assemblies of the saints,
34
Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.
let your wives keep silent in the assemblies, for it has not been permitted for them to speak; but let them be in subjection, as the law also says.
35
Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.
If they desire to learn anything, let them ask their own husbands at home, for it is shameful for a woman to chatter in the assembly.
36
Au je! Neno la Mungu lilitoka kwenu? Au kuwafikia ninyi peke yenu?
What? Was it from you that the word of God went out? Or did it come to you alone?
37
Mtu akijiona kuwa ni nabii au mtu wa rohoni, na ayatambue hayo ninayowaandikia, ya kwamba ni maagizo ya Bwana.
If any man thinks himself to be a prophet, or spiritual, let him recognize the things which I write to you, that they are the commandment of the Lord.
38
Lakini mtu akiwa mjinga, na awe mjinga.
But if anyone is ignorant, let him be ignorant.
39
Kwa ajili ya hayo, ndugu, takeni sana kuhutubu, wala msizuie kunena kwa lugha.
Therefore, brothers, desire earnestly to prophesy, and don't forbid speaking with other languages.
40
Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.
Let all things be done decently and in order.
« 13 15 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)