Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo.
Now concerning the collection for the saints, as I commanded the assemblies of Galatia, you do likewise.
Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;
On the first day of the week, let each one of you save, as he may prosper, that no collections be made when I come.
nami nitakapofika nitawatuma kwa nyaraka wale mtakaowachagua, wachukue hisani yenu mpaka Yerusalemu.
When I arrive, I will send whoever you approve with letters to carry your gracious gift to Jerusalem.
Na kama ikifaa niende na mimi, watasafiri pamoja nami.
If it is appropriate for me to go also, they will go with me.
Lakini nitakuja kwenu, nikiisha kupita kati ya Makedonia; maana napita kati ya Makedonia.
But I will come to you when I have passed through Macedonia, for I am passing through Macedonia.
Labda nitakaa kwenu; naam, labda wakati wote wa baridi, mpate kunisafirisha ko kote nitakakokwenda.
But with you it may be that I will stay, or even winter, that you may send me on my journey wherever I go.
Maana sipendi kuonana nanyi sasa, katika kupita tu, kwa sababu nataraji kukaa kwenu muda kidogo, Bwana akinijalia.
For I do not wish to see you now in passing, but I hope to stay a while with you, if the Lord permits.
Lakini nitakaa Efeso hata Pentekoste;
But I will stay at Ephesus until Pentecost,
kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa wa kufaa sana, na wako wengi wanipingao.
for a great and effective door has opened to me, and there are many adversaries.
Lakini, Timotheo akija, angalieni akae kwenu pasipo hofu; maana anaifanya kazi ya Bwana vile vile kama mimi mwenyewe;
Now if Timothy comes, see that he is with you without fear, for he does the work of the Lord, as I also do.
basi mtu ye yote asimdharau, lakini msafirisheni kwa amani, ili aje kwangu; maana ninamtazamia pamoja na ndugu zetu.
Therefore let no one despise him. But set him forward on his journey in peace, that he may come to me; for I expect him with the brothers.
Lakini kwa habari za Apolo, ndugu yetu, nalimsihi sana aende kwenu pamoja na hao ndugu; ambaye si mapenzi yake kwenda sasa; lakini atakuja atakapopata nafasi.
Now concerning Apollos, the brother, I strongly urged him to come to you with the brothers; and it was not at all his desire to come now; but he will come when he has an opportunity.
Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari.
Watch! Stand firm in the faith! Be courageous! Be strong!
Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.
Let all that you do be done in love.
Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa Stefana kwamba ni malimbuko ya Akaya, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumu watakatifu);
Now I beg you, brothers (you know the house of Stephanas, that it is the first fruits of Achaia, and that they have set themselves to minister to the saints),
watiini watu kama hawa, na kila mtu afanyaye kazi pamoja nao, na kujitaabisha.
that you also be in subjection to such, and to everyone who helps in the work and labors.
Nami nafurahi kwa sababu ya kuja kwao Stefana na Fortunato na Akaiko; maana hawa wamenikirimia kwa wingi yale niliyopungukiwa kwenu.
I rejoice at the coming of Stephanas, Fortunatus, and Achaicus; for that which was lacking on your part, they supplied.
Maana wameniburudisha roho yangu, na roho zenu pia; basi wajueni sana watu kama hao.
For they refreshed my spirit and yours. Therefore acknowledge those who are like that.
Makanisa ya Asia wawasalimu. Akila na Priska wawasalimu sana katika Bwana, pamoja na kanisa lililoko ndani ya nyumba yao.
The assemblies of Asia greet you. Aquila and Priscilla greet you much in the Lord, together with the assembly that is in their house.
Ndugu wote wawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
All the brothers greet you. Greet one another with a holy kiss.
Hii ni salamu yangu Paulo kwa mkono wangu mwenyewe.
This greeting is by me, Paul, with my own hand.
Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha.
If any man doesn't love the Lord Jesus Christ, let him be accursed{Greek: anathema.}. Come, Lord!{Aramaic: Maranatha!}
Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi.
The grace of the Lord Jesus Christ be with you.
Pendo langu na liwe pamoja nanyi nyote katika Kristo Yesu.
My love to all of you in Christ Jesus. Amen.