1 Wakorintho 12 Swahili & English
Listen/Download Audio1 Wakorintho 12 (Swahili) | 1st Corinthians 12 (English) |
---|---|
Basi, ndugu zangu, kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose kufahamu. 1 Wakorintho 12:1 |
Now concerning spiritual things, brothers, I don't want you to be ignorant. |
Mwajua ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa, mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama mlivyoongozwa. 1 Wakorintho 12:2 |
You know that when you were heathen{or Gentiles}, you were led away to those mute idols, however you might be led. |
Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. 1 Wakorintho 12:3 |
Therefore I make known to you that no man speaking by God's Spirit says, "Jesus is accursed." No one can say, "Jesus is Lord," but by the Holy Spirit. |
Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. 1 Wakorintho 12:4 |
Now there are various kinds of gifts, but the same Spirit. |
Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. 1 Wakorintho 12:5 |
There are various kinds of service, and the same Lord. |
Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. 1 Wakorintho 12:6 |
There are various kinds of workings, but the same God, who works all things in all. |
Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. 1 Wakorintho 12:7 |
But to each one is given the manifestation of the Spirit for the profit of all. |
Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; 1 Wakorintho 12:8 |
For to one is given through the Spirit the word of wisdom, and to another the word of knowledge, according to the same Spirit; |
mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja; 1 Wakorintho 12:9 |
to another faith, by the same Spirit; and to another gifts of healings, by the same Spirit; |
na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha; 1 Wakorintho 12:10 |
and to another workings of miracles; and to another prophecy; and to another discerning of spirits; to another different kinds of languages; and to another the interpretation of languages. |
lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye. 1 Wakorintho 12:11 |
But the one and the same Spirit works all of these, distributing to each one separately as he desires. |
Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. 1 Wakorintho 12:12 |
For as the body is one, and has many members, and all the members of the body, being many, are one body; so also is Christ. |
Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. 1 Wakorintho 12:13 |
For in one Spirit we were all baptized into one body, whether Jews or Greeks, whether bond or free; and were all given to drink into one Spirit. |
Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi. 1 Wakorintho 12:14 |
For the body is not one member, but many. |
Mguu ukisema, Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si wa mwili; je! Si wa mwili kwa sababu hiyo? 1 Wakorintho 12:15 |
If the foot would say, "Because I'm not the hand, I'm not part of the body," it is not therefore not part of the body. |
Na sikio likisema, Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si la mwili; je! Si la mwili kwa sababu hiyo? 1 Wakorintho 12:16 |
If the ear would say, "Because I'm not the eye, I'm not part of the body," it's not therefore not part of the body. |
Kama mwili wote ukiwa jicho, ku wapi kusikia? Kama wote ni sikio ku wapi kunusa? 1 Wakorintho 12:17 |
If the whole body were an eye, where would the hearing be? If the whole were hearing, where would the smelling be? |
Bali Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka. 1 Wakorintho 12:18 |
But now God has set the members, each one of them, in the body, just as he desired. |
Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? 1 Wakorintho 12:19 |
If they were all one member, where would the body be? |
Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. 1 Wakorintho 12:20 |
But now they are many members, but one body. |
Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi. 1 Wakorintho 12:21 |
The eye can't tell the hand, "I have no need for you," or again the head to the feet, "I have no need for you." |
Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi. 1 Wakorintho 12:22 |
No, much rather, those members of the body which seem to be weaker are necessary. |
Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana. 1 Wakorintho 12:23 |
Those parts of the body which we think to be less honorable, on those we bestow more abundant honor; and our unpresentable parts have more abundant propriety; |
Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa; 1 Wakorintho 12:24 |
whereas our presentable parts have no such need. But God composed the body together, giving more abundant honor to the inferior part, |
ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe. 1 Wakorintho 12:25 |
that there should be no division in the body, but that the members should have the same care for one another. |
Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho. 1 Wakorintho 12:26 |
When one member suffers, all the members suffer with it. Or when one member is honored, all the members rejoice with it. |
Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake. 1 Wakorintho 12:27 |
Now you are the body of Christ, and members individually. |
Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha. 1 Wakorintho 12:28 |
God has set some in the assembly: first apostles, second prophets, third teachers, then miracle workers, then gifts of healings, helps, governments, and various kinds of languages. |
Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza? 1 Wakorintho 12:29 |
Are all apostles? Are all prophets? Are all teachers? Are all miracle workers? |
Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri? 1 Wakorintho 12:30 |
Do all have gifts of healings? Do all speak with various languages? Do all interpret? |
Takeni sana karama zilizo kuu. Hata hivyo nawaonyesha njia iliyo bora. 1 Wakorintho 12:31 |
But earnestly desire the best gifts. Moreover, I show a most excellent way to you. |