Sifa Lyrics

Wageni by Paul Clement cover art

Paul Clement - Wageni Lyrics

Artist:
Paul Clement
Album:
SERMON
Official Release:
03 Aug 2022

Lyrics

Katika maisha yangu nilipokea wageni,


Nikawakaribisha kwangu, wakafanya vitu vingi


Hawakuwa wa kudumu, walikuwa wapitaji


Ila moyo wa ukarimu, ukanisababishia machozi


Mgeni wa kwanza alikuwa ni uchungu, 


Akaniumiza, akanipa maumivu


Alipomaliza akaenda zake,


Mgeni wa pili alikuwa ni huzuni,


Huyu naye


Akanikosesha furaha,


Mgeni wa tatu alikuwa ni magonjwa,


Akanidhoofisha, akataka kuniua


Hakufanikiwa akaenda zake


Aliyefuata alininyima watoto


Jina lake tasa, naye alipita


Mgeni mmoja jina lake ni mauti


Akamchukua Ntimi, akaniachia jeraha


Mgeni mwingine jina lake hofu


Hakutaka nifanikiwe, akanipa fikra potofu


Nikajiona siwezi, tena nitafeli


Huyo naye alipita


Hawa ni wageni, tena wapitaji


Hawatadumu, watapita


Hawa ni wageni, tena wapitaji


Hawatadumu, watapita


Hakuna jambo lolote gumu


Litakalodumu kwenye maisha yako


Ila yote yatapita


Na yakishapita, 


Hayatarudi tena


Tough times never last,


But tough people do


Mapito siyo mambo magumu unayoyapitia kwenye maisha yako, 


Ila mapito ni mambo magumu yanayopita kwenye maisha yako, 


Ndiyo maana ninaita mapito, kwa kuwa yanapita tu, na yanapita kwenye maisha yako, 


Na yakishapita hayawezi kurudi tena, Hah


Magonjwa,


Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita


Uchungu, (Huzuni)


Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita


Mateso, (Changamoto)


Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita


(Hata dhiki)


Hao ni wageni, tena wapitaji, Hawatadumu, watapita


Video