Sifa Lyrics

Nikumbushe Cover by Glory Shavu cover art

Glory Shavu - Nikumbushe Cover Lyrics

Artist:
Glory Shavu

Lyrics

Nirahisi kinywa kujawa na lawama tele


Pale mambo yanapoonekana hayaendi


ni ajabu sana namna moyo unahangaika


Ajabu sana moyo unavyoonyesha mashaka yakwamba


japokuwa Mungu anaishi ndani yangu kuna muda nahofu,


Japokuwa Mungu anaketi kati yetu kuna muda nahofu, ahh


nakumbuka wana wa Israel katika bahari yashamu


Japo walikatiza katikati ya bahari kwa ushindi,


Kwa nyimbo nyingi waliimba na kumsifu Bwanaa.


Lakini baada ya kuvuka na kuliona jagwa


yalibadilika mambo, manung'unikoo yalisimama


Na kusahau muujiza alotenda Bwana Mwanzo aah.


Eee MUNGU Nisaidie ee eeh


Nikumbushe wema wako nisije laumu


Nikumbushe ukuu wako wakati wa Magumu


Nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu


Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi,


Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi,


Eeh ee MUNGU Nisaidie


Nisaidie kukumbuka baba yakwamba umenichora


Kiganjani mwako kati ya wengi walioko duniani eenh


na mimi umenionaa oooh ooo


Nikumbushe baba yakwamba ni wewe umeniponya nilipoumwa


Yakwamba ni wewe mlipaji wa ada yangu shuleni.


ouoh ooh Yakwamba kama ungeniacha hatua moja


nisingelifika nilipo ooh eee Babaa


umenikung'uta mavumbi, kung'uta


mavumbi mimi na kuniheshimisha.


Nikumbushe wema wako nisije laumu


Nikumbushe ukuu wako wakati wa Magumu


Nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu


Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi


Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi,


Nikumbushe wema wako nisije laumu


Nikumbushe ukuu wako wakati wa Magumu


Nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu


Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi


Niimbe wimbo wa sifa katikati ya machozi,


Yesu nakutazama ninakuamini wewe


Fungua maisha yangu, nisaidie nisilalamike


Mbele zako, katika hali zote nijue upo


Umesema hutaniacha eeh Yahweh


Original Song: Nikumbushe Wema Wako by Angel B


Video