Alice Kimanzi - Dua Lyrics

Lyrics

VERSE 1:

Hali hii yangu

Isiwe nafasi ya kuto msifu Mungu

Mahali nilofika pasi ninungúnishe moyo

Daima nimshukuru

Nafsi yangu ’sisahau

Yale yote ametenda

Kwa upendo wake mwema

Kanizingira kwa neema

Moyo wangu vuta heri kwa subira


CHORUS:

Atajibu dua langu

Kwa njia Yake na wakati Wake (x2)

Moyo tulia


VERSE 2:

Najua njia hii si rahisi

Natambua mlima huu umezidi

Uwezo wangu

Egemeo ni Yesu tu

Na hata giza likija na mashaka pia

Yazibe macho yangu

Bado nitazidi kwani Ye aliahidi

Nasadiki Neno Lake kweli


BRIDGE:

Kwani Yeye anakuona

Tena Yeye anakujali (moyo tulia)

Anahisi uchungu wako

Tulia, tulia

Video

Alice Kimanzi - Dua |Official Video|

Thumbnail for Dua video
Loading...
In Queue
View Lyrics