Mwaminifu Lyrics - Paul Clement
Paul Clement swahili
Buy/Download AudioMwaminifu Lyrics
Una wasi wasi
Hofu na mashaka
Unahisi moyoni kama Mungu kakuacha
Maana unaona hausogei wala huendelei
Uko palepale kila siku
Uko vilevile (rudia 2)
Mungu aliianzisha safari tena ataimaliza
Maana alikujua kabla hujajijua kabla hujazaliwa
Mungu hawezi kukuacha njiani
Safari yako aliianzisha mwenyewe
Asingetaka angekuacha mwanzoni
Unakokwenda yeye anajua
(rudia 4)
Atainyosha njia yako
Atainyosha njia yako
Ina mabonde kweli
Ina vikwazo vingi
Atainyoosha njia yako