Paul Clement - Mwaminifu Lyrics

Mwaminifu Lyrics

Una wasi wasi
Hofu na mashaka
Unahisi moyoni kama Mungu kakuacha
Maana unaona hausogei wala huendelei
Uko palepale kila siku
Uko vilevile (rudia 2)

Mungu aliianzisha safari tena ataimaliza
Maana alikujua kabla hujajijua kabla hujazaliwa  
Mungu hawezi kukuacha njiani
Safari yako aliianzisha mwenyewe
Asingetaka angekuacha mwanzoni
Unakokwenda yeye anajua 
(rudia 4)

Atainyosha njia yako 
Atainyosha njia yako 
Ina mabonde kweli
Ina vikwazo vingi
Atainyoosha njia yako


Mwaminifu Video

Mwaminifu Lyrics -  Paul Clement

Paul Clement Songs

Related Songs