Warumi 9 Swahili & English

Listen/Download Audio
Warumi 9 (Swahili) Romans 9 (English)

Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu, Warumi 9:1

I tell the truth in Christ. I am not lying, my conscience testifying with me in the Holy Spirit,

ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu. Warumi 9:2

that I have great sorrow and unceasing pain in my heart.

Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili; Warumi 9:3

For I could wish that I myself were accursed from Christ for my brothers' sake, my relatives according to the flesh,

ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake; Warumi 9:4

who are Israelites; whose is the adoption, the glory, the covenants, the giving of the law, the service, and the promises;

ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina. Warumi 9:5

of whom are the fathers, and from whom is Christ as concerning the flesh, who is over all, God, blessed forever. Amen.

Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka. Maana hawawi wote Waisraeli walio wa uzao wa Israeli. Warumi 9:6

But it is not as though the word of God has come to nothing. For they are not all Israel, that are of Israel.

Wala hawawi wote wana kwa kuwa wazao wa Ibrahimu, bali, Katika Isaka wazao wako wataitwa; Warumi 9:7

Neither, because they are Abraham's seed, are they all children. But, "In Isaac will your seed be called."

yaani, si watoto wa mwili walio watoto wa Mungu, bali watoto wa ile ahadi wanahesabiwa kuwa wazao. Warumi 9:8

That is, it is not the children of the flesh who are children of God, but the children of the promise are counted as a seed.

Kwa maana neno la ahadi ni hili, Panapo wakati huu nitakuja, na Sara atakuwa na mwana. Warumi 9:9

For this is a word of promise, "At the appointed time I will come, and Sarah will have a son."

Wala si hivyo tu, lakini Rebeka naye, akiisha kuchukua mimba kwa mume mmoja, naye ni Isaka, baba yetu, Warumi 9:10

Not only so, but Rebecca also conceived by one, by our father Isaac.

(kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye), Warumi 9:11

For being not yet born, neither having done anything good or bad, that the purpose of God according to election might stand, not of works, but of him who calls,

aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo. Warumi 9:12

it was said to her, "The elder will serve the younger."

Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia. Warumi 9:13

Even as it is written, "Jacob I loved, but Esau I hated."

Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha! Warumi 9:14

What shall we say then? Is there unrighteousness with God? May it never be!

Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. Warumi 9:15

For he said to Moses, "I will have mercy on whom I have mercy, and I will have compassion on whom I have compassion."

Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu. Warumi 9:16

So then it is not of him who wills, nor of him who runs, but of God who has mercy.

Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote. Warumi 9:17

For the Scripture says to Pharaoh, "For this very purpose I caused you to be raised up, that I might show in you my power, and that my name might be published abroad in all the earth."

Basi, kama ni hivyo, atakaye kumrehemu humrehemu, na atakaye kumfanya mgumu humfanya mgumu. Warumi 9:18

So then, he has mercy on whom he desires, and he hardens whom he desires.

Basi, utaniambia, Mbona angali akilaumu? Kwa maana ni nani ashindanaye na kusudi lake? Warumi 9:19

You will say then to me, "Why does he still find fault? For who withstands his will?"

La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi? Warumi 9:20

But indeed, O man, who are you to reply against God? Will the thing formed ask him who formed it, "Why did you make me like this?"

Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima? Warumi 9:21

Or hasn't the potter a right over the clay, from the same lump to make one part a vessel for honor, and another for dishonor?

Ni nini basi, ikiwa Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake, na kuudhihirisha uweza wake, kwa uvumilivu mwingi, alichukuliana na vile vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa tayari kwa uharibifu; Warumi 9:22

What if God, willing to show his wrath, and to make his power known, endured with much patience vessels of wrath made for destruction,

tena, ili audhihirishe wingi wa utukufu wake katika vile vyombo vya rehema, alivyovitengeneza tangu zamani vipate utukufu; Warumi 9:23

and that he might make known the riches of his glory on vessels of mercy, which he prepared beforehand for glory,

ndio sisi aliotuita, si watu wa Wayahudi tu, ila na watu wa Mataifa pia? Warumi 9:24

us, whom he also called, not from the Jews only, but also from the Gentiles?

Ni kama vile alivyosema katika Hosea, Nitawaita watu wangu wale wasiokuwa watu wangu, Na mpenzi wangu yeye asiyekuwa mpenzi wangu. Warumi 9:25

As he says also in Hosea, "I will call them 'my people,' which were not my people; And her 'beloved,' who was not beloved."

Tena itakuwa mahali pale walipoambiwa, Ninyi si watu wangu, Hapo wataitwa wana wa Mungu aliye hai. Warumi 9:26

"It will be that in the place where it was said to them, 'You are not my people,' There they will be called 'children of the living God.'"

Isaya naye atoa sauti yake juu ya Israeli, kusema, Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa. Warumi 9:27

Isaiah cries concerning Israel, "If the number of the children of Israel are as the sand of the sea, It is the remnant who will be saved;

Kwa maana Bwana atalitekeleza neno lake juu ya nchi, akilimaliza na kulikata. Warumi 9:28

For He will finish the work and cut it short in righteousness, Because the LORD will make a short work upon the earth."

Tena kama Isaya alivyotangulia kunena, Kama Bwana wa majeshi asingalituachia uzao, Tungalikuwa kama Sodoma, tungalifananishwa na Gomora. Warumi 9:29

As Isaiah has said before, "Unless the Lord of Hosts{Greek: Sabaoth} had left us a seed, We would have become like Sodom, And would have been made like Gomorrah."

Tuseme nini, basi? Ya kwamba watu wa Mataifa, wasioifuata haki, walipata haki; lakini ni ile haki iliyo ya imani; Warumi 9:30

What shall we say then? That the Gentiles, who didn't follow after righteousness, attained to righteousness, even the righteousness which is of faith;

bali Israeli wakiifuata sheria ya haki hawakuifikilia ile sheria. Warumi 9:31

but Israel, following after a law of righteousness, didn't arrive at the law of righteousness.

Kwa sababu gani? Kwa sababu hawakuifuata kwa njia ya imani, bali kana kwamba kwa njia ya matendo. Wakajikwaa juu ya jiwe lile likwazalo, Warumi 9:32

Why? Because they didn't seek it by faith, but as it were by works of the law. They stumbled over the stumbling stone;

kama ilivyoandikwa, Tazama, naweka katika Sayuni jiwe likwazalo, na mwamba uangushao; Na kila amwaminiye hatatahayarika. Warumi 9:33

even as it is written, "Behold, I lay in Zion a stumbling stone and a rock of offense; And no one who believes in him will be disappointed."