Warumi 6 Swahili & English

Listen/Download Audio
Warumi 6 (Swahili) Romans 6 (English)

Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Warumi 6:1

What shall we say then? Shall we continue in sin, that grace may abound?

Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Warumi 6:2

May it never be! We who died to sin, how could we live in it any longer?

Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Warumi 6:3

Or don't you know that all we who were baptized into Christ Jesus were baptized into his death?

Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. Warumi 6:4

We were buried therefore with him through baptism to death, that just like Christ was raised from the dead through the glory of the Father, so we also might walk in newness of life.

Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake; Warumi 6:5

For if we have become united with him in the likeness of his death, we will also be part of his resurrection;

mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena; Warumi 6:6

knowing this, that our old man was crucified with him, that the body of sin might be done away with, so that we would no longer be in bondage to sin.

kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi. Warumi 6:7

For he who has died has been freed from sin.

Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; Warumi 6:8

But if we died with Christ, we believe that we will also live with him;

tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Warumi 6:9

knowing that Christ, being raised from the dead, dies no more. Death no more has dominion over him!

Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. Warumi 6:10

For the death that he died, he died to sin one time; but the life that he lives, he lives to God.

Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu. Warumi 6:11

Thus also consider yourselves also to be dead to sin, but alive to God in Christ Jesus our Lord.

Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa zake; Warumi 6:12

Therefore don't let sin reign in your mortal body, that you should obey it in its lusts.

wala msiendelee kuvitoa viungo vyenu kuwa silaha za dhuluma kwa dhambi; bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama walio hai baada ya kufa, na viungo vyenu kwa Mungu kuwa silaha za haki. Warumi 6:13

Neither present your members to sin as instruments of unrighteousness, but present yourselves to God, as alive from the dead, and your members as instruments of righteousness to God.

Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema. Warumi 6:14

For sin will not have dominion over you. For you are not under law, but under grace.

Ni nini basi? Tufanye dhambi kwa sababu hatuwi chini ya sheria bali chini ya neema? Hasha! Warumi 6:15

What then? Shall we sin, because we are not under law, but under grace? May it never be!

Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki. Warumi 6:16

Don't you know that to whom you present yourselves as servants to obedience, his servants you are whom you obey; whether of sin to death, or of obedience to righteousness?

Lakini Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa mioyo yenu ile namna ya elimu ambayo mliwekwa chini yake; Warumi 6:17

But thanks be to God, that, whereas you were bondservants of sin, you became obedient from the heart to that form of teaching whereunto you were delivered.

na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki. Warumi 6:18

Being made free from sin, you became bondservants of righteousness.

Nasema kwa jinsi ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa miili yenu. Kwa kuwa kama mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa. Warumi 6:19

I speak in human terms because of the weakness of your flesh, for as you presented your members as servants to uncleanness and to wickedness upon wickedness, even so now present your members as servants to righteousness for sanctification.

Kwa maana mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki. Warumi 6:20

For when you were servants of sin, you were free in regard to righteousness.

Ni faida gani basi mliyopata siku zile kwa mambo hayo mnayoyatahayarikia sasa? Kwa maana mwisho wa mambo hayo ni mauti. Warumi 6:21

What fruit then did you have at that time in the things of which you are now ashamed? For the end of those things is death.

Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele. Warumi 6:22

But now, being made free from sin, and having become servants of God, you have your fruit of sanctification, and the result of eternal life.

Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. Warumi 6:23

For the wages of sin is death, but the free gift of God is eternal life in Christ Jesus our Lord.