Warumi 13 Swahili & English

Listen/Download Audio
Warumi 13 (Swahili) Romans 13 (English)

Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. Warumi 13:1

Let every soul be in subjection to the higher authorities, for there is no authority except from God, and those who exist are ordained by God.

Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu. Warumi 13:2

Therefore he who resists the authority, withstands the ordinance of God; and those who withstand will receive to themselves judgment.

Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake; Warumi 13:3

For rulers are not a terror to the good work, but to the evil. Do you desire to have no fear of the authority? Do that which is good, and you will have praise from the same,

kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu. Warumi 13:4

for he is a servant of God to you for good. But if you do that which is evil, be afraid, for he doesn't bear the sword in vain; for he is a minister of God, an avenger for wrath to him who does evil.

Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri. Warumi 13:5

Therefore you need to be in subjection, not only because of the wrath, but also for conscience' sake.

Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi; kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo. Warumi 13:6

For this reason you also pay taxes, for they are ministers of God's service, attending continually on this very thing.

Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima. Warumi 13:7

Give therefore to everyone what you owe: taxes to whom taxes are due; customs to whom customs; respect to whom respect; honor to whom honor.

Msiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria. Warumi 13:8

Owe no one anything, except to love one another; for he who loves his neighbor has fulfilled the law.

Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Warumi 13:9

For the commandments, "You shall not commit adultery," "You shall not murder," "You shall not steal," "You shall not give false testimony," "You shall not covet,"{TR adds "You shall not give false testimony,"} and whatever other commandments there are, are all summed up in this saying, namely, "You shall love your neighbor as yourself."

Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria. Warumi 13:10

Love doesn't harm a neighbor. Love therefore is the fulfillment of the law.

Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini Warumi 13:11

Do this, knowing the time, that it is already time for you to awaken out of sleep, for salvation is now nearer to us than when we first believed.

Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru. Warumi 13:12

The night is far gone, and the day is near. Let's therefore throw off the works of darkness, and let's put on the armor of light.

Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu. Warumi 13:13

Let us walk properly, as in the day; not in reveling and drunkenness, not in sexual promiscuity and lustful acts, and not in strife and jealousy.

Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake. Warumi 13:14

But put on the Lord Jesus Christ, and make no provision for the flesh, for its lusts.