Nehemia 11 Swahili & English

Listen/Download Audio
Nehemia 11 (Swahili) Nehemiah 11 (English)

Basi, wakuu wa watu walikuwa wakikaa Yerusalemu; nao watu waliosalia wakapiga kura, ili katika watu kumi kumleta mmoja akae ndani ya Yerusalemu mji mtakatifu, na wale kenda wakae mijini. Nehemia 11:1

The princes of the people lived in Jerusalem: the rest of the people also cast lots, to bring one of ten to dwell in Jerusalem the holy city, and nine parts in the [other] cities.

Na hao watu wakawabariki wote waliojitoa kwa hiari wakae Yerusalemu. Nehemia 11:2

The people blessed all the men who willingly offered themselves to dwell in Jerusalem.

Basi hawa ndio wakuu wa jimbo waliokaa Yerusalemu; ila mijini mwa Yuda wakakaa kila mtu katika milki yake mijini mwao, yaani, Israeli, makuhani, na Walawi, na Wanethini, na akina watumwa wa Sulemani. Nehemia 11:3

Now these are the chiefs of the province who lived in Jerusalem: but in the cities of Judah lived everyone in his possession in their cities, [to wit], Israel, the priests, and the Levites, and the Nethinim, and the children of Solomon's servants.

Tena wakakaa Yerusalemu wengine wa wana wa Yuda, na wengine wa wana wa Benyamini. Wa wana wa Yuda; Athaya, mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, wa wana wa Peresi; Nehemia 11:4

In Jerusalem lived certain of the children of Judah, and of the children of Benjamin. Of the children of Judah: Athaiah the son of Uzziah, the son of Zechariah, the son of Amariah, the son of Shephatiah, the son of Mahalalel, of the children of Perez;

na Maaseya, mwana wa Baruki, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, Mshelani. Nehemia 11:5

and Maaseiah the son of Baruch, the son of Colhozeh, the son of Hazaiah, the son of Adaiah, the son of Joiarib, the son of Zechariah, the son of the Shilonite.

Wana wa Peresi wote waliokaa Yerusalemu walikuwa watu mia nne sitini na wanane, mashujaa. Nehemia 11:6

All the sons of Perez who lived in Jerusalem were four hundred sixty-eight valiant men.

Na wana wa Benyamini ndio hawa; Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseva, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya. Nehemia 11:7

These are the sons of Benjamin: Sallu the son of Meshullam, the son of Joed, the son of Pedaiah, the son of Kolaiah, the son of Maaseiah, the son of Ithiel, the son of Jeshaiah.

Na baada yake Gabai, Salai, watu mia kenda ishirini na wanane. Nehemia 11:8

After him Gabbai, Sallai, nine hundred twenty-eight.

Na Yoeli, mwana wa Zikri, alikuwa msimamizi wao; na Yuda, mwana wa Hasenua, alikuwa wa pili juu ya mji. Nehemia 11:9

Joel the son of Zichri was their overseer; and Judah the son of Hassenuah was second over the city.

Wa makuhani; Yedaya, Yoyaribu, Yakini, Nehemia 11:10

Of the priests: Jedaiah the son of Joiarib, Jachin,

na Seraya, mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi wa nyumba ya Mungu, Nehemia 11:11

Seraiah the son of Hilkiah, the son of Meshullam, the son of Zadok, the son of Meraioth, the son of Ahitub, the ruler of the house of God,

na ndugu zao waliofanya kazi ya nyumbani, watu mia nane ishirini na wawili; na Adaya, mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amzi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya, Nehemia 11:12

and their brothers who did the work of the house, eight hundred twenty-two; and Adaiah the son of Jeroham, the son of Pelaliah, the son of Amzi, the son of Zechariah, the son of Pashhur, the son of Malchijah,

na ndugu zake, wakuu wa mbari za mababa, watu mia mbili arobaini na wawili; na Maasai, mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri, Nehemia 11:13

and his brothers, chiefs of fathers' [houses], two hundred forty-two; and Amashsai the son of Azarel, the son of Ahzai, the son of Meshillemoth, the son of Immer,

na ndugu zao, waume mashujaa, watu mia na ishirini na wanane; na msimamizi wao alikuwa Zabdieli, mmojawapo wa hao wakuu. Nehemia 11:14

and their brothers, mighty men of valor, one hundred twenty-eight; and their overseer was Zabdiel, the son of Haggedolim.

Na wa Walawi; Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni; Nehemia 11:15

Of the Levites: Shemaiah the son of Hasshub, the son of Azrikam, the son of Hashabiah, the son of Bunni;

na Shabethai na Yozabadi, wa wakuu wa Walawi, walioisimamia kazi ya nje ya nyumba ya Mungu; Nehemia 11:16

and Shabbethai and Jozabad, of the chiefs of the Levites, who had the oversight of the outward business of the house of God;

na Matania, mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu, mkuu mwenye kuanzisha shukrani katika sala, na Bakbukia, wa pili wake miongoni mwa nduguze; na Obadia, mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Nehemia 11:17

and Mattaniah the son of Mica, the son of Zabdi, the son of Asaph, who was the chief to begin the thanksgiving in prayer, and Bakbukiah, the second among his brothers; and Abda the son of Shammua, the son of Galal, the son of Jeduthun.

Walawi wote waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu mia mbili themanini na wanne. Nehemia 11:18

All the Levites in the holy city were two hundred eighty-four.

Pamoja na hao, mabawabu; Akubu, Talmoni, na ndugu zao waliolinda malangoni, walikuwa watu mia na sabini na wawili. Nehemia 11:19

Moreover the porters, Akkub, Talmon, and their brothers, who kept watch at the gates, were one hundred seventy-two.

Na Israeli waliosalia, katika hao makuhani, na Walawi, walikuwamo mijini mwote mwa Yuda, kila mtu katika milki yake. Nehemia 11:20

The residue of Israel, of the priests, the Levites, were in all the cities of Judah, everyone in his inheritance.

Lakini Wanethini walikuwa wakikaa Ofeli; na juu ya Wanethini walikuwa Siha na Gishpa. Nehemia 11:21

But the Nethinim lived in Ophel: and Ziha and Gishpa were over the Nethinim.

Naye msimamizi wa Walawi huko Yerusalemu, ni Uzi, mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, hao waimbaji, alikuwa juu ya kazi ya nyumba ya Mungu. Nehemia 11:22

The overseer also of the Levites at Jerusalem was Uzzi the son of Bani, the son of Hashabiah, the son of Mattaniah, the son of Mica, of the sons of Asaph, the singers, over the business of the house of God.

Kwa kuwa palikuwa na amri ya mfalme juu yao, na agizo la hakika walilowekewa waimbaji, kama ilivyohusika na kila siku. Nehemia 11:23

For there was a commandment from the king concerning them, and a settled provision for the singers, as every day required.

Na Pethahia, mwana wa Meshezabeli, wa wana wa Zera, mwana wa Yuda, alikuwa wakili wa mfalme kwa habari ya mambo yote ya watu. Nehemia 11:24

Pethahiah the son of Meshezabel, of the children of Zerah the son of Judah, was at the king's hand in all matters concerning the people.

Na katika habari za vijiji na mashamba yake; wengine wa wana wa Yuda walikuwa wakikaa Kiriath-arba na vijiji vyake, na katika Diboni na vijiji vyake, na Yekabzeeli na vijiji vyake; Nehemia 11:25

As for the villages, with their fields, some of the children of Judah lived in Kiriath Arba and the towns of it, and in Dibon and the towns of it, and in Jekabzeel and the villages of it,

na katika Yeshua, na Molada, na Beth-peleti; Nehemia 11:26

and in Jeshua, and in Moladah, and Beth Pelet,

na Hazar-shuali, na Beer-sheba na vijiji vyake; Nehemia 11:27

and in Hazar Shual, and in Beersheba and the towns of it,

na katika Siklagi, na Mekona na vijiji vyake; Nehemia 11:28

and in Ziklag, and in Meconah and in the towns of it,

na katika Enrimoni, na Sora, na Yarmuthi; Nehemia 11:29

and in En-rimmon, and in Zorah, and in Jarmuth,

Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, Lakishi na mashamba yake, Azeka na vijiji vyake. Hivyo wakatua toka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu. Nehemia 11:30

Zanoah, Adullam, and their villages, Lachish and the fields of it, Azekah and the towns of it. So they encamped from Beersheba to the valley of Hinnom.

Wana wa Benyamini nao walikuwa wakikaa Geba, na Mikmashi, na Aiya, na Beth-eli na vijiji vyake; Nehemia 11:31

The children of Benjamin also [lived] from Geba [onward], at Michmash and Aija, and at Bethel and the towns of it,

Anathothi, Nobu, Anania; Nehemia 11:32

at Anathoth, Nob, Ananiah,

Hazori, Rama, Gitaimu; Nehemia 11:33

Hazor, Ramah, Gittaim,

Hadidi, Seboimu, Nebalati; Nehemia 11:34

Hadid, Zeboim, Neballat,

Lodi, na Ono, bonde la Wakarashi. Nehemia 11:35

Lod, and Ono, the valley of craftsmen.

Na wa Walawi, wengine walikaa katika Yuda na wengine katika Benyamini. Nehemia 11:36

Of the Levites, certain divisions in Judah [were joined] to Benjamin.