1
Mara kulipokuwa asubuhi wakuu wa makuhani walifanya shauri pamoja na wazee na waandishi na baraza nzima, wakamfunga Yesu, wakamchukua, wakamleta mbele ya Pilato.
Early in the morning, the chief priests, elders, scribes, and the whole Sanhedrin devised a plan. They bound Jesus, led Him away, and handed Him over to Pilate.
2
Pilato akamwuliza, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu, akamwambia, Wewe wasema.
So Pilate questioned Him, “Are You the King of the Jews?” “You have said so,” Jesus replied.
3
Nao wakuu wa makuhani walikuwa wakimshitaki mambo mengi.
And the chief priests began to accuse Him of many things.
4
Pilato akamwuliza tena akisema, Hujibu neno? Tazama ni mambo mangapi wanayokushitaki!
Then Pilate questioned Him again, “Have You no answer? Look how many charges they are bringing against You!”
5
Wala Yesu hakujibu neno tena, hata Pilato akastaajabu.
But to Pilate’s amazement, Jesus made no further reply.
6
Basi wakati wa sikukuu huwafungulia mfungwa mmoja, wamwombaye.
Now it was Pilate’s custom at the feast to release to the people a prisoner of their choosing.
7
Palikuwa na mtu aitwaye Baraba, amefungwa pamoja na watu waliofanya fitina, na kufanya uuaji katika fitina ile.
And a man named Barabbas was imprisoned with the rebels who had committed murder during the insurrection.
8
Makutano wakaja, wakaanza kuomba awafanyie kama vile alivyozoea.
So the crowd went up and began asking Pilate to keep his custom.
9
Pilato akawajibu, akisema, Je! Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?
“Do you want me to release to you the King of the Jews?” Pilate asked.
10
Kwa maana alitambua ya kuwa wakuu wa makuhani wamemtoa kwa husuda.
For he knew it was out of envy that the chief priests had handed Jesus over.
11
Lakini wakuu wa makuhani wakawataharakisha makutano, kwamba afadhali awafungulie Baraba.
But the chief priests stirred up the crowd to have him release Barabbas to them instead.
12
Pilato akajibu tena akawaambia, Basi nimtendeje huyu mnayemnena kuwa ni mfalme wa Wayahudi?
So Pilate asked them again, “What then do you want me to do with the One you call the King of the Jews?”
13
Wakapiga kelele tena, Msulibishe.
And they shouted back, “Crucify Him!”
14
Pilato akawaambia, Kwani, ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, Msulibishe.
“Why?” asked Pilate. “What evil has He done?” But they shouted all the louder, “Crucify Him!”
15
Pilato akipenda kuwaridhisha makutano, akawafungulia Baraba; akamtoa Yesu, baada ya kumpiga mijeledi, ili asulibiwe.
And wishing to satisfy the crowd, Pilate released Barabbas to them. But he had Jesus flogged, and handed Him over to be crucified.
16
Nao askari wakamchukua ndani ya behewa, ndiyo Praitorio (yaani, nyumba ya uliwali), wakakusanya pamoja kikosi kizima.
Then the soldiers led Jesus away into the palace (that is, the Praetorium) and called the whole company together.
17
Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani;
They dressed Him in a purple robe, twisted together a crown of thorns, and set it on His head.
18
wakaanza kumsalimu, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!
And they began to salute Him: “Hail, King of the Jews!”
19
Wakampiga mwanzi wa kichwa, wakamtemea mate, wakapiga magoti, wakamsujudia.
They kept striking His head with a staff and spitting on Him. And they knelt down and bowed before Him.
20
Hata wakiisha kumdhihaki, wakamvua lile vazi la rangi ya zambarau, wakamvika mavazi yake mwenyewe; wakamchukua nje ili wamsulibishe.
After they had mocked Him, they removed the purple robe and put His own clothes back on Him. Then they led Him out to crucify Him.
21
Wakamshurutisha mtu aliyekuwa akipita, akitoka mashamba, Simoni Mkirene, baba yao Iskanda na Rufo, ili auchukue msalaba wake.
Now Simon of Cyrene, the father of Alexander and Rufus, was passing by on his way in from the country, and the soldiers forced him to carry the cross of Jesus.
22
Wakamleta mpaka mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa.
They brought Jesus to a place called Golgotha, which means The Place of the Skull.
23
Wakampa mvinyo iliyotiwa manemane, asiipokee.
There they offered Him wine mixed with myrrh, but He did not take it.
24
Wakamsulibisha, wakagawa mavazi yake, wakayapigia kura kila mtu atwae nini.
And they crucified Him. They also divided His garments by casting lots to decide what each of them would take.
25
Basi ilikuwa saa tatu, nao wakamsulibisha.
It was the third hour when they crucified Him.
26
Palikuwa na anwani ya mashitaka yake iliyoandikwa juu, MFALME WA WAYAHUDI.
And the charge inscribed against Him read: THE KING OF THE JEWS.
27
Na pamoja naye walisulibisha wanyang'anyi wawili, mmoja mkono wake wa kuume na mmoja mkono wake wa kushoto. [
Along with Jesus, they crucified two robbers, one on His right and one on His left.
28
Basi andiko likatimizwa linenalo, Alihesabiwa pamoja na waasi.]
29
Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakitikisa-tikisa vichwa, wakisema, Ahaa! Wewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga katika siku tatu,
And those who passed by heaped abuse on Him, shaking their heads and saying, “Aha! You who are going to destroy the temple and rebuild it in three days,
30
jiponye nafsi yako, ushuke msalabani.
come down from the cross and save Yourself!”
31
Kadhalika na wakuu wa makuhani wakamdhihaki wao kwa wao, pamoja na waandishi, wakisema, Aliponya wengine; hawezi kujiponya mwenyewe.
In the same way, the chief priests and scribes mocked Him among themselves, saying, “He saved others, but He cannot save Himself!
32
Kristo, mfalme wa Israeli, na ashuke sasa msalabani tupate kuona na kuamini. Hata wale waliosulibiwa pamoja naye wakamfyolea.
Let the Christ, the King of Israel, come down now from the cross, so that we may see and believe!” And even those who were crucified with Him berated Him.
33
Na ilipokuwa saa sita, palikuwa na giza juu ya nchi yote, hata saa tisa.
From the sixth hour until the ninth hour darkness came over all the land.
34
Na saa tisa Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Maana yake, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
At the ninth hour, Jesus cried out in a loud voice, “Eloi, Eloi, lema sabachthani?” which means, “My God, My God, why have You forsaken Me?”
35
Na baadhi yao waliosimama pale, walisema, Tazama, anamwita Eliya.
When some of those standing nearby heard this, they said, “Behold, He is calling Elijah.”
36
Na mmoja akaenda mbio, akajaza sifongo siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha, akisema, Acheni, na tuone kwamba Eliya anakuja kumtelemsha.
And someone ran and filled a sponge with sour wine. He put it on a reed and held it up for Jesus to drink, saying, “Leave Him alone. Let us see if Elijah comes to take Him down.”
37
Naye Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
But Jesus let out a loud cry and breathed His last.
38
Pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini.
And the veil of the temple was torn in two from top to bottom.
39
Basi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.
When the centurion standing there in front of Jesus saw how He had breathed His last, he said, “Truly this man was the Son of God!”
40
Palikuwako na wanawake wakitazama kwa mbali; miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo mdogo na Yose, na Salome;
And there were also women watching from a distance. Among them were Mary Magdalene, Mary the mother of James the younger and of Joses, and Salome.
41
hao ndio waliofuatana naye huko Galilaya, na kumtumikia; na wengine wengi waliopanda pamoja naye mpaka Yerusalemu.
These women had followed Jesus and ministered to Him while He was in Galilee, and there were many other women who had come up to Jerusalem with Him.
42
Hata ikiisha kuwa jioni, kwa sababu ni Maandalio, ndiyo siku iliyo kabla ya sabato,
Now it was already evening. Since it was Preparation Day (that is, the day before the Sabbath),
43
akaenda Yusufu, mtu wa Arimathaya, mstahiki, mtu wa baraza ya mashauri, naye mwenyewe anautazamia ufalme wa Mungu; akafanya ujasiri, akaingia mbele ya Pilato akauomba mwili wake Yesu.
Joseph of Arimathea, a prominent Council member who himself was waiting for the kingdom of God, boldly went to Pilate to ask for the body of Jesus.
44
Lakini Pilato akastaajabu, kwamba amekwisha kufa. Akamwita yule akida, akamwuliza kwamba amekufa kitambo.
Pilate was surprised to hear that Jesus was already dead, so he summoned the centurion to ask if this was so.
45
Hata alipokwisha kupata hakika kwa yule akida, alimpa Yusufu yule maiti.
When Pilate had confirmed it with the centurion, he granted the body to Joseph.
46
Naye akanunua sanda ya kitani, akamtelemsha, akamfungia ile sanda, akamweka katika kaburi lililochongwa mwambani; akavingirisha jiwe mbele ya mlango wa kaburi.
So Joseph bought a linen cloth, took down the body of Jesus, wrapped it in the cloth, and placed it in a tomb that had been cut out of the rock. Then he rolled a stone against the entrance to the tomb.
47
Nao Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yose wakapatazama mahali alipowekwa.
Mary Magdalene and Mary the mother of Joseph saw where His body was placed.