Mambo ya Walawi BSB

Mambo ya Walawi 3

Leviticus Chapter 3

1
Na matoleo yake kwamba ni sadaka za amani; kwamba asongeza katika ng'ombe, mume au mke, atamtoa huyo aliye mkamilifu mbele ya Bwana.
“If one’s offering is a peace offering and he offers an animal from the herd, whether male or female, he must present it without blemish before the LORD.
2
Naye ataweka mkono wake kichwani mwake huyo aliyemtoa, na kumchinja mlangoni pa hema ya kukutania; na wana wa Haruni, hao makuhani, watainyunyiza damu yake katika madhabahu pande zote.
He is to lay his hand on the head of the offering and slaughter it at the entrance to the Tent of Meeting. Then Aaron’s sons the priests shall splatter the blood on all sides of the altar.
3
Naye atasongeza katika sadaka hiyo ya amani, dhabihu kwa Bwana itakayofanywa kwa njia ya moto; yaani, mafuta yafunikayo matumbo, na mafuta yote yaliyo juu ya matumbo,
From the peace offering he is to bring a food offering to the LORD: the fat that covers the entrails, all the fat that is on them,
4
na figo zake mbili, na mafuta yaliyoshikamana nazo, yaliyo karibu na kiuno, na hicho kitambi kilicho katika ini, pamoja na hizo figo; hayo yote atayaondoa.
both kidneys with the fat on them near the loins, and the lobe of the liver, which he is to remove with the kidneys.
5
Na wana wa Haruni watayateketeza kwa moto juu ya madhabahu, juu ya sadaka ya kuteketezwa, iliyo katika kuni zilizo juu ya moto; ni dhabihu ya kusongezwa kwa njia ya moto, harufu ya kupendeza kwa Bwana.
Then Aaron’s sons are to burn it on the altar atop the burnt offering that is on the burning wood, as a food offering, a pleasing aroma to the LORD.
6
Na matoleo yake kwa sadaka za amani atakayomchinjia Bwana, kwamba ni katika kundi la kondoo; mume au mke, atamtoa huyo aliye mkamilifu.
If, however, one’s peace offering to the LORD is from the flock, he must present a male or female without blemish.
7
Kama akimtoa mwana-kondoo kuwa matoleo yake, ndipo atakapomtolea Bwana;
If he is presenting a lamb for his offering, he must present it before the LORD.
8
naye ataweka mkono wake kichwani mwake huyo aliyemsongeza, na kumchinja mlangoni pa hema ya kukutania; na wana wa Haruni watainyunyiza damu yake katika madhabahu pande zote.
He is to lay his hand on the head of his offering and slaughter it in front of the Tent of Meeting. Then Aaron’s sons shall splatter its blood on all sides of the altar.
9
Naye atasongeza katika sadaka hiyo ya amani dhabihu kwa Bwana, itakayofanywa kwa njia ya moto; yaani, mafuta yake, na mkia wenye mafuta mzima, atauondoa kwa kuukata hapo karibu na mfupa wa maungoni; na mafuta yafunikayo matumbo, na mafuta yote yaliyo katika matumbo,
And from the peace offering he shall bring a food offering to the LORD consisting of its fat: the entire fat tail cut off close to the backbone, the fat that covers the entrails, all the fat that is on them,
10
na figo zake mbili, na mafuta yaliyoshikamana nazo, yaliyo karibu na kiuno chake, na kitambi kilicho katika ini, pamoja na hizo figo; hayo yote atayaondoa.
both kidneys with the fat on them near the loins, and the lobe of the liver, which he is to remove with the kidneys.
11
Naye kuhani atayateketeza kwa moto juu ya madhabahu; ni chakula cha dhabihu ya kusongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto.
Then the priest is to burn them on the altar as food, a food offering to the LORD.
12
Na matoleo yake, kwamba ni mbuzi, ndipo atakapomtoa mbele za Bwana;
If one’s offering is a goat, he is to present it before the LORD.
13
naye ataweka mkono wake kichwani mwake, na kumchinja hapo mbele ya hema ya kukutania; na wana wa Haruni watainyunyiza damu yake katika madhabahu pande zote.
He must lay his hand on its head and slaughter it in front of the Tent of Meeting. Then Aaron’s sons shall splatter its blood on all sides of the altar.
14
Naye atasongeza katika sadaka hiyo matoleo yake, dhabihu kwa Bwana kwa njia ya moto; yaani, mafuta yafunikayo matumbo, na mafuta yote yaliyo katika matumbo,
And from his offering he shall present a food offering to the LORD: the fat that covers the entrails, all the fat that is on them,
15
na figo zake mbili, na mafuta yaliyoshikamana nazo, yaliyo karibu na kiuno chake, na kitambi kilicho katika ini pamoja na hizo figo mbili; hayo yote atayaondoa.
both kidneys with the fat on them near the loins, and the lobe of the liver, which he is to remove with the kidneys.
16
Naye kuhani atayateketeza kwa moto juu ya madhabahu; ni chakula cha dhabihu ya kusongezwa kwa njia ya moto, iwe harufu ya kupendeza; mafuta yote ni ya Bwana.
Then the priest is to burn the food on the altar as a food offering, a pleasing aroma. All the fat is the LORD’s.
17
Neno hili litakuwa amri ya daima, katika vizazi vyenu vyote, ndani ya nyumba zenu zote, ya kwamba hamtakula mafuta wala damu kabisa.</p>
This is a permanent statute for the generations to come, wherever you live: You must not eat any fat or any blood.”

Chagua Sura