2 Wafalme 25 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Wafalme 25 (Swahili) 2nd Kings 25 (English)

Ikawa katika mwaka wa kenda wa kutawala kwake, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya mwezi huo, Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akaja, yeye na jeshi lake lote, kupigana na Yerusalemu, akapanga hema zake kuukabili; nao wakajenga ngome juu yake pande zote. 2 Wafalme 25:1

It happened in the ninth year of his reign, in the tenth month, in the tenth day of the month, that Nebuchadnezzar king of Babylon came, he and all his army, against Jerusalem, and encamped against it; and they built forts against it round about.

Basi mji huo ulihusuriwa hata mwaka wa kumi na moja wa mfalme Sedekia. 2 Wafalme 25:2

So the city was besieged to the eleventh year of king Zedekiah.

Siku ya kenda ya mwezi wa nne njaa ilikuwa nzito ndani ya mji, hata hapakuwa na chakula kwa watu wa nchi. 2 Wafalme 25:3

On the ninth day of the [fourth] month the famine was sore in the city, so that there was no bread for the people of the land.

Ndipo mahali pakabomolewa katika ukuta wa mji, watu wote wa vita wakakimbia usiku kwa njia ya lango lililokuwa kati ya zile kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme; (basi wale Wakaldayo walikuwa wakiuzuia mji pande zote;) mfalme akaenda kwa njia ya Araba. 2 Wafalme 25:4

Then a breach was made in the city, and all the men of war [fled] by night by the way of the gate between the two walls, which was by the king's garden (now the Chaldeans were against the city round about); and [the king] went by the way of the Arabah.

Lakini jeshi la Wakaldayo wakamfuatia mfalme, wakampata katika nchi tambarare ya Yeriko; na jeshi lake lote walikuwa wametawanyika na kumwacha. 2 Wafalme 25:5

But the army of the Chaldeans pursued after the king, and overtook him in the plains of Jericho; and all his army was scattered from him.

Ndipo wakamkamata mfalme, wakamchukua kwa mfalme wa Babeli huko Ribla; wakatoa hukumu juu yake. 2 Wafalme 25:6

Then they took the king, and carried him up to the king of Babylon to Riblah; and they gave judgment on him.

Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake, wakampofusha macho Sedekia, wakamfunga kwa pingu, wakamchukua mpaka Babeli. 2 Wafalme 25:7

They killed the sons of Zedekiah before his eyes, and put out the eyes of Zedekiah, and bound him in fetters, and carried him to Babylon.

Hata mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi, ndio mwaka wa kumi na kenda wa mfalme Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, mtumishi wa mfalme wa Babeli, akaingia Yerusalemu. 2 Wafalme 25:8

Now in the fifth month, on the seventh day of the month, which was the nineteenth year of king Nebuchadnezzar, king of Babylon, came Nebuzaradan the captain of the guard, a servant of the king of Babylon, to Jerusalem.

Akaiteketeza nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme; na nyumba zote za Yerusalemu, naam, kila nyumba kubwa aliiteketeza kwa moto. 2 Wafalme 25:9

He burnt the house of Yahweh, and the king's house; and all the houses of Jerusalem, even every great house, burnt he with fire.

Na jeshi lote la Wakaldayo, waliokuwa pamoja na huyo amiri wa askari walinzi, wakazibomoa kuta za Yerusalemu pande zote. 2 Wafalme 25:10

All the army of the Chaldeans, who were [with] the captain of the guard, broke down the walls of Jerusalem round about.

Na mabaki ya watu waliosalia katika mji, nao wale walioasi, na kumkimbilia mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu wote wengine, watu hao Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawachukua mateka. 2 Wafalme 25:11

The residue of the people who were left in the city, and those who fell away, who fell to the king of Babylon, and the residue of the multitude, did Nebuzaradan the captain of the guard carry away captive.

Lakini huyo amiri wa askari walinzi akawaacha watu walio maskini ili wawe watunza mizabibu na wakulima. 2 Wafalme 25:12

But the captain of the guard left of the poorest of the land to work the vineyards and fields.

Na zile nguzo za shaba zilizokuwako nyumbani mwa Bwana, na matako, na ile bahari ya shaba, iliyokuwamo nyumbani mwa Bwana, Wakaldayo wakavivunja vipande vipande, wakaichukua shaba yake yote mpaka Babeli. 2 Wafalme 25:13

The pillars of brass that were in the house of Yahweh, and the bases and the brazen sea that were in the house of Yahweh, did the Chaldeans break in pieces, and carried the brass of them to Babylon.

Nayo masufuria, na majembe, na makasi, na miiko, na vyombo vyote vya shaba walivyokuwa wakivitumia, wakavichukua vyote. 2 Wafalme 25:14

The pots, and the shovels, and the snuffers, and the spoons, and all the vessels of brass with which they ministered, took they away.

Na vyetezo, na mabakuli; vilivyokuwa vya dhahabu katika dhahabu, na vilivyokuwa vya fedha katika fedha, amiri wa askari walinzi akavichukua. 2 Wafalme 25:15

The fire pans, and the basins, that which was of gold, in gold, and that which was of silver, in silver, the captain of the guard took away.

Zile nguzo mbili, na ile bahari moja, na yale matako, Sulemani alivyoifanyia nyumba ya Bwana; shaba ya vyombo hivyo vyote haikuwa na uzani. 2 Wafalme 25:16

The two pillars, the one sea, and the bases, which Solomon had made for the house of Yahweh, the brass of all these vessels was without weight.

Urefu wa nguzo moja ulikuwa dhiraa kumi na nane, na kichwa cha shaba kilikuwa juu yake; na urefu wa kichwa ulikuwa dhiraa tatu; na mapambo ya wavu na makomamanga juu ya kichwa hicho kote kote, yote yalikuwa ya shaba. Nayo nguzo ya pili ilikuwa vivyo hivyo, pamoja na ule wavu. 2 Wafalme 25:17

The height of the one pillar was eighteen cubits, and a capital of brass was on it; and the height of the capital was three cubits, with network and pomegranates on the capital round about, all of brass: and like to these had the second pillar with network.

Na amiri wa askari walinzi akamtwaa Seraya, kuhani mkuu, na Sefania, kuhani wa pili, na wale walinzi watu wa mlango; 2 Wafalme 25:18

The captain of the guard took Seraiah the chief priest, and Zephaniah the second priest, and the three keepers of the threshold:

na katika mji akamtwaa towashi mmoja, aliyewasimamia watu wa vita; na watu watano katika wale waliosimama mbele ya mfalme, walioonekana mjini; na katibu wa jemadari wa jeshi, aliyewaandika watu wa nchi; na watu sitini katika watu wa nchi, walioonekana mjini. 2 Wafalme 25:19

and out of the city he took an officer who was set over the men of war; and five men of those who saw the king's face, who were found in the city; and the scribe, the captain of the host, who mustered the people of the land; and sixty men of the people of the land, who were found in the city.

Kisha Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawatwaa hao, akawaleta kwa mfalme wa Babeli huko Ribla. 2 Wafalme 25:20

Nebuzaradan the captain of the guard took them, and brought them to the king of Babylon to Riblah.

Naye mfalme wa Babeli akawapiga, na kuwaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Hivyo Yuda wakachukuliwa utumwani kutoka nchi yao. 2 Wafalme 25:21

The king of Babylon struck them, and put them to death at Riblah in the land of Hamath. So Judah was carried away captive out of his land.

Na kwa habari ya watu waliosalia katika nchi ya Yuda, aliowasaza Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akamweka Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani awe liwali juu yao. 2 Wafalme 25:22

As for the people who were left in the land of Judah, whom Nebuchadnezzar king of Babylon had left, even over them he made Gedaliah the son of Ahikam, the son of Shaphan, governor.

Kisha, wakuu wote wa majeshi, wao na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemweka Gedalia kuwa liwali, wakamwendea Gedalia huko Mispa; nao ni hawa, Ishmaeli mwana wa Nethania, na Yohana mwana wa Karea, na Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yezania mwana wa Mmaaka, wao na watu wao. 2 Wafalme 25:23

Now when all the captains of the forces, they and their men, heard that the king of Babylon had made Gedaliah governor, they came to Gedaliah to Mizpah, even Ishmael the son of Nethaniah, and Johanan the son of Kareah, and Seraiah the son of Tanhumeth the Netophathite, and Jaazaniah the son of the Maacathite, they and their men.

Na Gedalia akawaapia wao na watu wao, akawaambia, Msiogope kwa ajili ya watumishi wa Wakaldayo; kaeni katika nchi; mkamtumikie mfalme wa Babeli; itakuwa vyema kwenu. 2 Wafalme 25:24

Gedaliah swore to them and to their men, and said to them, Don't be afraid because of the servants of the Chaldeans: dwell in the land, and serve the king of Babylon, and it shall be well with you.

Lakini ikawa katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania, mwana wa Elishama, mmoja wa wazao wa kifalme, na watu kumi pamoja naye, wakamwendea Gedalia, wakampiga hata akafa, na hao Wayahudi na Wakaldayo waliokuwa pamoja naye huko Mispa. 2 Wafalme 25:25

But it happened in the seventh month, that Ishmael the son of Nethaniah, the son of Elishama, of the royal seed came, and ten men with him, and struck Gedaliah, so that he died, and the Jews and the Chaldeans that were with him at Mizpah.

Wakaondoka watu wote, wadogo kwa wakubwa, pamoja na wakuu wa majeshi, wakainuka kwenda Misri; kwa kuwa waliwaogopa Wakaldayo. 2 Wafalme 25:26

All the people, both small and great, and the captains of the forces, arose, and came to Egypt; for they were afraid of the Chaldeans.

Ikawa katika mwaka wa thelathini na saba wa kuhamishwa kwake Yekonia mfalme wa Yuda ,katika mwezi wa kumi na mbili ,siku ya ishirini na saba ya mwezi ,Evil-merodaki,mfalme wa Babeli ,katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake,akamwinua kichwa Yekonia,mfalme wa Yuda,akamtoa gerezani. 2 Wafalme 25:27

It happened in the seven and thirtieth year of the captivity of Jehoiachin king of Judah, in the twelfth month, on the seven and twentieth day of the month, that Evilmerodach king of Babylon, in the year that he began to reign, did lift up the head of Jehoiachin king of Judah out of prison;

Akasema naye maneno mazuri, akaweka kiti chake cha enzi juu ya viti vya enzi vya wafalme waliokuwa pamoja naye huko Babeli; 2 Wafalme 25:28

and he spoke kindly to him, and set his throne above the throne of the kings who were with him in Babylon,

naye akambadilishia mavazi yake ya gerezani, akala chakula mbele yake daima, siku zote za maisha yake. 2 Wafalme 25:29

and changed his prison garments. [Jehoiachin] ate bread before him continually all the days of his life:

Na kwa posho yake, alipewa posho ya daima na mfalme, siku kwa siku sehemu, siku zote za maisha yake. 2 Wafalme 25:30

and for his allowance, there was a continual allowance given him of the king, every day a portion, all the days of his life.