2 Wafalme 14 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Wafalme 14 (Swahili) 2nd Kings 14 (English)

Katika mwaka wa pili wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala. 2 Wafalme 14:1

In the second year of Joash son of Joahaz king of Israel began Amaziah the son of Joash king of Judah to reign.

Naye alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Yehoadani wa Yerusalemu. 2 Wafalme 14:2

He was twenty-five years old when he began to reign; and he reigned twenty-nine years in Jerusalem: and his mother's name was Jehoaddin of Jerusalem.

Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, ila si kama babaye Daudi; akafanya kama yote aliyoyafanya baba yake Yoashi. 2 Wafalme 14:3

He did that which was right in the eyes of Yahweh, yet not like David his father: he did according to all that Joash his father had done.

Walakini mahali pa juu hapakuondolewa; watu wakaendelea kutoa dhabihu na kufukiza uvumba katika mahali pa juu. 2 Wafalme 14:4

However the high places were not taken away: the people still sacrificed and burnt incense in the high places.

Ikawa, mara ufalme ulipokuwa imara mkononi mwake, aliwaua watumishi wale waliomwua mfalme baba yake; 2 Wafalme 14:5

It happened, as soon as the kingdom was established in his hand, that he killed his servants who had slain the king his father:

ila hakuwaua watoto wa hao wauaji; kama ilivyoandikwa katika kitabu cha torati ya Musa, kama alivyoamuru Bwana, akisema, Mababa wasife kwa makosa ya wana, wala wana wasife kwa makosa ya mababa; lakini kila mtu atakufa kwa kosa lake mwenyewe. 2 Wafalme 14:6

but the children of the murderers he didn't put to death; according to that which is written in the book of the law of Moses, as Yahweh commanded, saying, The fathers shall not be put to death for the children, nor the children be put to death for the fathers; but every man shall die for his own sin.

Akawaua Waedomi katika Bonde la Chumvi watu elfu kumi; akautwaa Sela vitani, akauita jina lake Yoktheeli hata leo. 2 Wafalme 14:7

He killed of Edom in the Valley of Salt ten thousand, and took Sela by war, and called the name of it Joktheel, to this day.

Ndipo Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, Njoo, tutazamane uso kwa uso. 2 Wafalme 14:8

Then Amaziah sent messengers to Jehoash, the son of Jehoahaz son of Jehu, king of Israel, saying, Come, let us look one another in the face.

Naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatuma kwa Amazia mfalme wa Yuda, akisema, Mbaruti uliokuwako Lebanoni ulituma kwa mwerezi uliokuwako Lebanoni, kusema, Umwoze mwanangu binti yako; kukapita hayawani aliyekuwako Lebanoni, akaukanyaga ule mbaruti. 2 Wafalme 14:9

Jehoash the king of Israel sent to Amaziah king of Judah, saying, The thistle that was in Lebanon sent to the cedar that was in Lebanon, saying, Give your daughter to my son as wife: and there passed by a wild animal that was in Lebanon, and trod down the thistle.

Kweli umepiga Edomu, na moyo wako umekutukuza; ujisifu basi, ukae nyumbani mwako. Mbona unataka kujitia bure katika madhara, hata uanguke, wewe na Yuda pamoja nawe? 2 Wafalme 14:10

You have indeed struck Edom, and your heart has lifted you up: glory of it, and abide at home; for why should you meddle to [your] hurt, that you should fall, even you, and Judah with you?

Lakini Amazia hakutaka kusikia. Basi Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea; wakatazamana uso kwa uso, yeye na Amazia mfalme wa Yuda, huko Beth-shemeshi ulio wa Yuda. 2 Wafalme 14:11

But Amaziah would not hear. So Jehoash king of Israel went up; and he and Amaziah king of Judah looked one another in the face at Beth-shemesh, which belongs to Judah.

Yuda wakashindwa mbele ya Israeli; wakakimbia kila mtu hemani kwake. 2 Wafalme 14:12

Judah was put to the worse before Israel; and they fled every man to his tent.

Yehoashi mfalme wa Israeli akamtwaa Amazia mfalme wa Yuda, mwanawe Yoashi mwana wa Ahazia, huko Beth-shemeshi, akaja Yerusalemu, akauvunja ukuta wa Yerusalemu toka lango la Efraimu hata lango la pembeni, mikono mia nne. 2 Wafalme 14:13

Jehoash king of Israel took Amaziah king of Judah, the son of Jehoash the son of Ahaziah, at Beth-shemesh, and came to Jerusalem, and broke down the wall of Jerusalem from the gate of Ephraim to the corner gate, four hundred cubits.

Akaitwaa dhahabu yote na fedha, na vyombo vyote vilivyoonekana katika nyumba ya Bwana, na katika hazina za nyumba ya mfalme, tena watu, kuwa amana; akarudi Samaria. 2 Wafalme 14:14

He took all the gold and silver, and all the vessels that were found in the house of Yahweh, and in the treasures of the king's house, the hostages also, and returned to Samaria.

Basi mambo yote ya Yehoashi yaliyosalia, aliyoyafanya, na ushujaa wake, na jinsi alivyopigana na Amazia mfalme wa Yuda, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli? 2 Wafalme 14:15

Now the rest of the acts of Jehoash which he did, and his might, and how he fought with Amaziah king of Judah, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Israel?

Yehoashi akalala na baba zake, akazikwa katika Samaria pamoja na wafalme wa Israeli; na Yeroboamu mwanawe akatawala mahali pake. 2 Wafalme 14:16

Jehoash slept with his fathers, and was buried in Samaria with the kings of Israel; and Jeroboam his son reigned in his place.

Naye Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda akaishi baada ya kufa kwake Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli miaka kumi na mitano. 2 Wafalme 14:17

Amaziah the son of Joash king of Judah lived after the death of Jehoash son of Jehoahaz king of Israel fifteen years.

Basi mambo yote ya Amazia yaliyosalia, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda? 2 Wafalme 14:18

Now the rest of the acts of Amaziah, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Judah?

Wakafanya fitina juu yake katika Yerusalemu, naye akakimbia mpaka Lakishi, lakini wakatuma watu kumfuata mpaka Lakishi, wakamwua huko. 2 Wafalme 14:19

They made a conspiracy against him in Jerusalem; and he fled to Lachish: but they sent after him to Lachish, and killed him there.

Wakamleta juu ya farasi; naye akazikwa huko Yerusalemu pamoja na babaze katika mji wa Daudi. 2 Wafalme 14:20

They brought him on horses; and he was buried at Jerusalem with his fathers in the city of David.

Na watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia aliyekuwa mwenye umri wa miaka kumi na sita,wakamfanya awe mfalme mahali pa baba yake Amazia. 2 Wafalme 14:21

All the people of Judah took Azariah, who was sixteen years old, and made him king in the room of his father Amaziah.

Huyo akajenga Elathi, akaurudisha kwa Yuda, baada ya kulala mfalme pamoja na babaze. 2 Wafalme 14:22

He built Elath, and restored it to Judah, after that the king slept with his fathers.

Katika mwaka wa kumi na tano wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala katika Samaria; akatawala miaka arobaini na mmoja. 2 Wafalme 14:23

In the fifteenth year of Amaziah the son of Joash king of Judah Jeroboam the son of Joash king of Israel began to reign in Samaria, [and reigned] forty-one years.

Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana; wala hakuyaacha makosa yote ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli. 2 Wafalme 14:24

He did that which was evil in the sight of Yahweh: he didn't depart from all the sins of Jeroboam the son of Nebat, with which he made Israel to sin.

Yeye akaurudisha mpaka wa Israeli toka kuingia kwa Hamathi hata bahari ya Araba, sawasawa na neno la Bwana, Mungu wa Israeli, alilolinena kwa mkono wa mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii, aliyekuwa wa Gath-heferi. 2 Wafalme 14:25

He restored the border of Israel from the entrance of Hamath to the sea of the Arabah, according to the word of Yahweh, the God of Israel, which he spoke by his servant Jonah the son of Amittai, the prophet, who was of Gath Hepher.

Kwani Bwana akayaona mateso ya Israeli, kwamba yalikuwa machungu sana; maana hakukuwa na mfungwa wala asiyefungwa, wala msaidizi kwa ajili ya Israeli. 2 Wafalme 14:26

For Yahweh saw the affliction of Israel, that it was very bitter; for there was none shut up nor left at large, neither was there any helper for Israel.

Wala Bwana hakusema ya kwamba atalifuta jina la Israeli litoke chini ya mbingu; lakini akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi. 2 Wafalme 14:27

Yahweh didn't say that he would blot out the name of Israel from under the sky; but he saved them by the hand of Jeroboam the son of Joash.

Basi mambo yote ya Yeroboamu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na ushujaa wake, na jinsi aliyvopigana, akawapatia tena Israeli Dameski na Hamathi, iliyokuwa kwanza ya Yuda, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli? 2 Wafalme 14:28

Now the rest of the acts of Jeroboam, and all that he did, and his might, how he warred, and how he recovered Damascus, and Hamath, [which had belonged] to Judah, for Israel, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Israel?

Yeroboamu akalala na babaze, yaani, na wafalme wa Israeli. Na Zekaria mwanawe akatawala mahali pake.

2 Wafalme 14:29

Jeroboam slept with his fathers, even with the kings of Israel; and Zechariah his son reigned in his place.