Zabron Singers - Atafanya Kitu Lyrics

Lyrics

Ukihesabu utachoka kuna ya juzi jana na leo

Ya kesho Mungu kafanya

Huku kwetu hakunanga hofu, mashaka, wasiwasi

Twajiamini tuko na Mungu


Mimi si yule wa zamani wa kulialia

Mungu kanitoa huko namfurahia

Sasa nimehama kitengo cha kulialia

Nimehamia level zingine za kufurahia


Aliumba mchana, usiku

Lipi ngumu la kumishinda Mungu

Huyu Mungu hufanya zaidi ya mtu na mahitaji


Ametenda mengi kwangu

(Hebu subiri na wewe, Mungu atafanya kitu)

Usichoke ndugu yangu

(Subiri subiri na wewe, Huyu Yesu atafanya kitu)


Subiri, Subiri

Eeh Subiri


Huku kwa Yesu tupata shida mateso

Na Yesu anatatua

Twashukuru na kuimba sifa zake

Ni Yeye astahili kuinuliwa


Mungu katufanya tuimbe na kumtukuza

Tuvae tun'ngae tuishi na kufurahia

Siwezi hesabu mangapi kanisimamia

Mipaka nivuke na jina nikamtukuze


Kwa tiketi ya jina la Yesu

Hakuna jambo gumu kutushinda

Sifa zake zipande asante

Bwana umetuinua


Ametenda mengi kwangu

(Hebu subiri na wewe, Mungu atafanya kitu)

Usichoke ndugu yangu

(Subiri subiri na wewe, Huyu Yesu atafanya kitu)


Video

ZABRON SINGERS-ATAFANYA KITU (Official Video)

Thumbnail for Atafanya Kitu video
Loading...
In Queue
View Lyrics