Zabron Singers - Atafanya Kitu Lyrics

Atafanya Kitu Lyrics

Ukihesabu utachoka kuna ya juzi jana na leo
Ya kesho Mungu kafanya
Huku kwetu hakunanga hofu, mashaka, wasiwasi
Twajiamini tuko na Mungu

Mimi si yule wa zamani wa kulialia
Mungu kanitoa huko namfurahia
Sasa nimehama kitengo cha kulialia
Nimehamia level zingine za kufurahia

Aliumba mchana, usiku
Lipi ngumu la kumishinda Mungu
Huyu Mungu hufanya zaidi ya mtu na mahitaji

Ametenda mengi kwangu
(Hebu subiri na wewe, Mungu atafanya kitu)
Usichoke ndugu yangu
(Subiri subiri na wewe, Huyu Yesu atafanya kitu)

Subiri, Subiri
Eeh Subiri

Huku kwa Yesu tupata shida mateso
Na Yesu anatatua
Twashukuru na kuimba sifa zake
Ni Yeye astahili kuinuliwa

Mungu katufanya tuimbe na kumtukuza
Tuvae tun'ngae tuishi na kufurahia
Siwezi hesabu mangapi kanisimamia
Mipaka nivuke na jina nikamtukuze

Kwa tiketi ya jina la Yesu
Hakuna jambo gumu kutushinda
Sifa zake zipande asante
Bwana umetuinua

Ametenda mengi kwangu
(Hebu subiri na wewe, Mungu atafanya kitu)
Usichoke ndugu yangu
(Subiri subiri na wewe, Huyu Yesu atafanya kitu)


Atafanya Kitu Video

Atafanya Kitu Lyrics -  Zabron Singers

Zabron Singers Songs

Related Songs